< הושע 8 >
אל חכך שפר כנשר על בית יהוה--יען עברו בריתי ועל תורתי פשעו | 1 |
“Weka tarumbeta katika midomo yako! Tai anakuja juu ya nyumba ya Bwana kwa sababu watu wamevunja agano langu na waliasi dhidi ya sheria yangu.
לי יזעקו אלהי ידענוך ישראל | 2 |
Wananililia,'Mungu wangu, sisi katika Israeli tunakujua.'
זנח ישראל טוב אויב ירדפו | 3 |
Lakini Israeli amekataa mema, na adui atamfuata.
הם המליכו ולא ממני השירו ולא ידעתי כספם וזהבם עשו להם עצבים למען יכרת | 4 |
Wameweka wafalme, lakini sio kwa shauri langu. Wamewafanya wakuu, lakini sikuwa na habari. Kwa fedha zao na dhahabu wamejifanyia sanamu wenyewe, ili wakatiliwe mbali.”
זנח עגלך שמרון חרה אפי בם עד מתי לא יוכלו נקין | 5 |
“Ndama yako imekataliwa, Samaria. Hasira yangu inawaka juu ya watu hawa. Kwa muda gani watakuwa na hatia?
כי מישראל והוא--חרש עשהו ולא אלהים הוא כי שבבים יהיה עגל שמרון | 6 |
Kwa maana sanamu hii ilitoka Israeli; fundi aliifanya; si Mungu! Ndama ya Samaria itavunjwa vipande vipande.
כי רוח יזרעו וסופתה יקצרו קמה אין לו צמח בלי יעשה קמח--אולי יעשה זרים יבלעהו | 7 |
Kwa maana watu hupanda upepo na kuvuna kimbunga. Mbegu zilizosimama hazina vichwa; haitoi unga. Ikiwa itakomaa, wageni watakula.
נבלע ישראל עתה היו בגוים ככלי אין חפץ בו | 8 |
Israeli imemezwa; sasa wanalala kati ya mataifa kama kitu kisicho na maana.
כי המה עלו אשור פרא בודד לו אפרים התנו אהבים | 9 |
Kwa maana walikwenda Ashuru kama punda wa mwitu pekee. Efraimu ameajiri wapenzi kwa ajili yake mwenyewe.
גם כי יתנו בגוים עתה אקבצם ויחלו מעט ממשא מלך שרים | 10 |
Hata ingawa wameajiri wapenzi kati ya mataifa, sasa nitawakusanya pamoja. Wao wataanza kupotea kwa sababu ya unyanyasaji wa mfalme wa wakuu.
כי הרבה אפרים מזבחות לחטא היו לו מזבחות לחטא | 11 |
Kwa maana Efraimu imeongeza madhabahu kwa sadaka za dhambi, lakini zimekuwa madhabahu kwa kufanya dhambi.
אכתוב (אכתב) לו--רבו (רבי) תורתי כמו זר נחשבו | 12 |
Niliweza kuandika sheria yangu kwao mara elfu kumi, lakini wangeiona kama kitu cha ajabu kwao.
זבחי הבהבי יזבחו בשר ויאכלו--יהוה לא רצם עתה יזכר עונם ויפקד חטאותם--המה מצרים ישובו | 13 |
Kwa ajili ya dhabihu za sadaka zangu, hutoa nyama na kuila, lakini mimi, Bwana, siwakubali. Sasa nitafikiri juu ya uovu wao na kuadhibu dhambi zao. Watarudi Misri.
וישכח ישראל את עשהו ויבן היכלות ויהודה הרבה ערים בצרות ושלחתי אש בעריו ואכלה ארמנתיה | 14 |
Israeli amenisahau mimi, Muumba wake, na amejenga majumba. Yuda ameimarisha miji mingi, lakini nitatuma moto juu ya miji yake; itaharibu ngome zake.