< בראשית 36 >
ואלה תלדות עשו הוא אדום | 1 |
Hivi ndivyo vizazi vya Esau (yaani Edomu).
עשו לקח את נשיו מבנות כנען את עדה בת אילון החתי ואת אהליבמה בת ענה בת צבעון החוי | 2 |
Esau akaoa wake kutoka miongoni mwa wanawake wa Kanaani: Ada binti wa Eloni Mhiti, Oholibama binti wa Ana, mjukuu wa kike wa Sibeoni Mhivi,
ואת בשמת בת ישמעאל אחות נביות | 3 |
pia akaoa Basemathi binti wa Ishmaeli, dada yake Nebayothi.
ותלד עדה לעשו את אליפז ובשמת ילדה את רעואל | 4 |
Ada akamzalia Esau Elifazi, Basemathi akamzaa Reueli,
ואהליבמה ילדה את יעיש (יעוש) ואת יעלם ואת קרח אלה בני עשו אשר ילדו לו בארץ כנען | 5 |
Oholibama akamzaa Yeushi, Yalamu na Kora. Hawa ndio wana wa Esau waliozaliwa kwake huko Kanaani.
ויקח עשו את נשיו ואת בניו ואת בנתיו ואת כל נפשות ביתו ואת מקנהו ואת כל בהמתו ואת כל קנינו אשר רכש בארץ כנען וילך אל ארץ מפני יעקב אחיו | 6 |
Esau akawachukua wake zake, watoto wake wa kiume na wa kike na wote wa nyumbani mwake, mifugo yake pamoja na wanyama wake wengine wote na mali yake yote ambayo alikuwa ameipata akiwa Kanaani, akahamia katika nchi iliyo mbali na Yakobo ndugu yake.
כי היה רכושם רב משבת יחדו ולא יכלה ארץ מגוריהם לשאת אתם--מפני מקניהם | 7 |
Mali zao zilikuwa nyingi sana kiasi kwamba haikuwa rahisi wao kuishi pamoja, nchi waliyokuwa wakiishi isingewatosha wote kwa ajili ya mifugo yao.
וישב עשו בהר שעיר עשו הוא אדום | 8 |
Kwa hiyo Esau (ambaye ni Edomu) aliishi katika nchi ya kilima huko Seiri.
ואלה תלדות עשו אבי אדום בהר שעיר | 9 |
Hawa ndio wazao wa Esau, baba wa Waedomu, katika nchi ya kilima cha Seiri.
אלה שמות בני עשו אליפז בן עדה אשת עשו רעואל בן בשמת אשת עשו | 10 |
Haya ndiyo majina ya wana wa Esau: Elifazi, mwana wa Esau ambaye mkewe Ada alimzalia; na Reueli, mwana wa Esau ambaye mkewe Basemathi alimzalia.
ויהיו בני אליפז--תימן אומר צפו וגעתם וקנז | 11 |
Wana wa Elifazi ni: Temani, Omari, Sefo, Gatamu na Kenazi.
ותמנע היתה פילגש לאליפז בן עשו ותלד לאליפז את עמלק אלה בני עדה אשת עשו | 12 |
Elifazi mwana wa Esau alikuwa pia na suria aliyeitwa Timna, ambaye alimzalia Amaleki. Hawa ndio waliokuwa wajukuu wa Ada mke wa Esau.
ואלה בני רעואל נחת וזרח שמה ומזה אלה היו בני בשמת אשת עשו | 13 |
Wana wa Reueli ni: Nahathi, Zera, Shama na Miza. Hawa ndio waliokuwa wajukuu wa Basemathi mkewe Esau.
ואלה היו בני אהליבמה בת ענה בת צבעון--אשת עשו ותלד לעשו את יעיש (יעוש) ואת יעלם ואת קרח | 14 |
Wana wa Oholibama binti Ana, mkewe Esau, aliyekuwa mjukuu wa Sibeoni, aliomzalia Esau ni: Yeushi, Yalamu na Kora.
אלה אלופי בני עשו בני אליפז בכור עשו--אלוף תימן אלוף אומר אלוף צפו אלוף קנז | 15 |
Hawa ndio waliokuwa wakuu miongoni mwa wazao wa Esau: Wakuu wa wana wa Elifazi, mzaliwa wa kwanza wa Esau ni: Temani, Omari, Sefo, Kenazi,
אלוף קרח אלוף געתם אלוף עמלק אלה אלופי אליפז בארץ אדום אלה בני עדה | 16 |
Kora, Gatamu na Amaleki. Hawa ndio waliokuwa wakuu waliotoka kwa Elifazi huko Edomu, waliokuwa wajukuu wa kiume wa Ada.
ואלה בני רעואל בן עשו--אלוף נחת אלוף זרח אלוף שמה אלוף מזה אלה אלופי רעואל בארץ אדום--אלה בני בשמת אשת עשו | 17 |
Wakuu wa wana wa Reueli, mwana wa Esau ni: Nahathi, Zera, Shama na Miza. Hawa ndio wakuu waliotoka kwa Reueli huko Edomu, waliokuwa wajukuu wa kiume wa Basemathi mkewe Esau.
ואלה בני אהליבמה אשת עשו--אלוף יעוש אלוף יעלם אלוף קרח אלה אלופי אהליבמה בת ענה--אשת עשו | 18 |
Wakuu wa wana wa Esau ambao mkewe Oholibama alimzalia ni: Yeushi, Yalamu na Kora. Hawa ndio wakuu waliotoka kwa mke wa Esau, Oholibama binti Ana.
אלה בני עשו ואלה אלופיהם הוא אדום | 19 |
Hawa ndio waliokuwa wana wa Esau (ndiye Edomu), na hawa ndio waliokuwa wakuu wao.
אלה בני שעיר החרי ישבי הארץ לוטן ושובל וצבעון וענה | 20 |
Hawa ndio walikuwa wana wa Seiri, Mhori, waliokuwa wakiishi katika nchi ile: Lotani, Shobali, Sibeoni, Ana,
ודשון ואצר ודישן אלה אלופי החרי בני שעיר בארץ אדום | 21 |
Dishoni, Eseri na Dishani. Hawa ndio wana wa Seiri huko Edomu waliokuwa wakuu kwa Wahori.
ויהיו בני לוטן חרי והימם ואחות לוטן תמנע | 22 |
Wana wa Lotani walikuwa: Hori na Homamu. Timna alikuwa dada yake Lotani.
ואלה בני שובל עלון ומנחת ועיבל שפו ואונם | 23 |
Wana wa Shobali walikuwa: Alvani, Manahathi, Ebali, Shefo na Onamu.
ואלה בני צבעון ואיה וענה הוא ענה אשר מצא את הימם במדבר ברעתו את החמרים לצבעון אביו | 24 |
Wana wa Sibeoni walikuwa: Aiya na Ana. Huyu Ana ndiye aligundua chemchemi ya maji moto jangwani alipokuwa akichunga punda za Sibeoni baba yake.
ואלה בני ענה דשן ואהליבמה בת ענה | 25 |
Watoto wa Ana walikuwa: Dishoni na Oholibama binti wa Ana.
ואלה בני דישן--חמדן ואשבן ויתרן וכרן | 26 |
Wana wa Dishoni walikuwa: Hemdani, Eshbani, Ithrani na Kerani.
אלה בני אצר--בלהן וזעון ועקן | 27 |
Wana wa Eseri walikuwa: Bilhani, Zaavani na Akani.
Wana wa Dishani walikuwa: Usi na Arani.
אלה אלופי החרי אלוף לוטן אלוף שובל אלוף צבעון אלוף ענה | 29 |
Hawa ndio waliokuwa wakuu wa Wahori: Lotani, Shobali, Sibeoni, Ana,
אלוף דשן אלוף אצר אלוף דישן אלה אלופי החרי לאלפיהם בארץ שעיר | 30 |
Dishoni, Eseri na Dishani. Hawa ndio walikuwa wakuu wa Wahori, kufuatana na makundi yao, katika nchi ya Seiri.
ואלה המלכים אשר מלכו בארץ אדום--לפני מלך מלך לבני ישראל | 31 |
Wafuatao ni wafalme waliotawala Edomu kabla ya mfalme yeyote wa Israeli kutawala:
וימלך באדום בלע בן בעור ושם עירו דנהבה | 32 |
Bela mwana wa Beori alikuwa mfalme wa Edomu. Mji wake uliitwa Dinhaba.
וימת בלע וימלך תחתיו יובב בן זרח מבצרה | 33 |
Bela alipofariki, Yobabu mwana wa Zera kutoka Bosra akawa mfalme baada yake.
וימת יובב וימלך תחתיו חשם מארץ התימני | 34 |
Yobabu alipofariki, Hushamu kutoka nchi ya Watemani akawa mfalme baada yake.
וימת חשם וימלך תחתיו הדד בן בדד המכה את מדין בשדה מואב ושם עירו עוית | 35 |
Hushamu alipofariki, Hadadi mwana wa Bedadi, aliyeshinda Midiani katika nchi ya Moabu, akawa mfalme baada yake. Mji wake uliitwa Avithi.
וימת הדד וימלך תחתיו שמלה ממשרקה | 36 |
Hadadi alipofariki, Samla kutoka Masreka akawa mfalme baada yake.
וימת שמלה וימלך תחתיו שאול מרחבות הנהר | 37 |
Samla alipofariki, Shauli kutoka Rehobothi ngʼambo ya Mto Frati akawa mfalme baada yake.
וימת שאול וימלך תחתיו בעל חנן בן עכבור | 38 |
Shauli alipofariki, Baal-Hanani mwana wa Akbori akawa mfalme baada yake.
וימת בעל חנן בן עכבור וימלך תחתיו הדר ושם עירו פעו ושם אשתו מהיטבאל בת מטרד בת מי זהב | 39 |
Baal-Hanani mwana wa Akbori alipofariki, Hadadi akawa mfalme baada yake. Mji wake uliitwa Pau, na mkewe aliitwa Mehetabeli binti Matredi, binti Me-Zahabu.
ואלה שמות אלופי עשו למשפחתם למקמתם בשמתם אלוף תמנע אלוף עלוה אלוף יתת | 40 |
Hawa ndio wakuu waliotokana na Esau, kwa majina, kufuatana na koo zao na nchi zao: Timna, Alva, Yethethi,
אלוף אהליבמה אלוף אלה אלוף פינן | 41 |
Oholibama, Ela, Pinoni,
אלוף קנז אלוף תימן אלוף מבצר | 42 |
Kenazi, Temani, Mibsari,
אלוף מגדיאל אלוף עירם אלה אלופי אדום למשבתם בארץ אחזתם--הוא עשו אבי אדום | 43 |
Magdieli na Iramu. Hawa ndio walikuwa wakuu wa Edomu, kufuatana na makazi yao katika nchi waliyoimiliki. Huyu ndiye alikuwa Esau, baba wa Waedomu.