< קֹהֶלֶת 3 >

לכל זמן ועת לכל חפץ תחת השמים 1
Kuna wakati kwa ajili ya kila jambo, nayo majira kwa kila tendo chini ya mbingu:
עת ללדת ועת למות עת לטעת ועת לעקור נטוע 2
wakati wa kuzaliwa na wakati wa kufa, wakati wa kupanda na wakati wa kungʼoa yaliyopandwa,
עת להרוג ועת לרפוא עת לפרוץ ועת לבנות 3
wakati wa kuua na wakati wa kuponya, wakati wa kubomoa, na wakati wa kujenga,
עת לבכות ועת לשחוק עת ספוד ועת רקוד 4
wakati wa kulia na wakati wa kucheka, wakati wa kuomboleza na wakati wa kucheza,
עת להשליך אבנים ועת כנוס אבנים עת לחבוק ועת לרחק מחבק 5
wakati wa kutawanya mawe na wakati wa kukusanya mawe, wakati wa kukumbatia na wakati wa kutokumbatia,
עת לבקש ועת לאבד עת לשמור ועת להשליך 6
wakati wa kutafuta na wakati wa kupoteza, wakati wa kuweka na wakati wa kutupa,
עת לקרוע ועת לתפור עת לחשות ועת לדבר 7
wakati wa kurarua na wakati wa kushona, wakati wa kunyamaza na wakati wa kuzungumza,
עת לאהב ועת לשנא עת מלחמה ועת שלום 8
wakati wa kupenda na wakati wa kuchukia, wakati wa vita na wakati wa amani.
מה יתרון העושה באשר הוא עמל 9
Mfanyakazi anapata faida gani kutokana na taabu yake?
ראיתי את הענין אשר נתן אלהים לבני האדם--לענות בו 10
Nimeona mzigo Mungu alioweka juu ya wanadamu.
את הכל עשה יפה בעתו גם את העלם נתן בלבם--מבלי אשר לא ימצא האדם את המעשה אשר עשה האלהים מראש ועד סוף 11
Amefanya kila kitu kiwe kizuri kwa wakati wake. Pia ameiweka hiyo milele katika mioyo ya wanadamu, wala hawawezi kutambua kwa kina yale ambayo Mungu amefanya tangu mwanzo hadi mwisho.
ידעתי כי אין טוב בם--כי אם לשמוח ולעשות טוב בחייו 12
Ninajua kwamba hakuna kitu bora kwa wanadamu kuliko kuwa na furaha na kutenda mema wakati wanapoishi.
וגם כל האדם שיאכל ושתה וראה טוב בכל עמלו--מתת אלהים היא 13
Tena ni karama ya Mungu kila mtu apate kula na kunywa na kujiburudisha kwa mema katika kazi yake yote.
ידעתי כי כל אשר יעשה האלהים הוא יהיה לעולם--עליו אין להוסיף וממנו אין לגרע והאלהים עשה שיראו מלפניו 14
Ninajua kwamba kila kitu anachokifanya Mungu kitadumu milele, hakuna kinachoweza kuongezwa au kupunguzwa. Mungu hufanya hivyo ili watu wamche yeye.
מה שהיה כבר הוא ואשר להיות כבר היה והאלהים יבקש את נרדף 15
Chochote kilichopo kilishakuwepo, na kitakachokuwepo kimekwishakuwepo kabla; naye Mungu huyaita yale yaliyopita yarudi tena.
ועוד ראיתי תחת השמש מקום המשפט שמה הרשע ומקום הצדק שמה הרשע 16
Pia nikaona kitu kingine tena chini ya jua: Mahali pa kutolea hukumu, uovu ulikuwepo, mahali pa kupatia haki, uovu ulikuwepo.
אמרתי אני בלבי--את הצדיק ואת הרשע ישפט האלהים כי עת לכל חפץ ועל כל המעשה שם 17
Nikafikiri moyoni mwangu, “Mungu atawaleta hukumuni wote wawili wenye haki na waovu, kwa maana kutakuwako na wakati kwa ajili ya kila jambo, wakati kwa ajili ya kila tendo.”
אמרתי אני בלבי--על דברת בני האדם לברם האלהים ולראות שהם בהמה המה להם 18
Pia nikafikiri, “Kuhusu wanadamu, Mungu huwajaribu ili wajione kwamba wao ni kama wanyama.
כי מקרה בני האדם ומקרה הבהמה ומקרה אחד להם--כמות זה כן מות זה ורוח אחד לכל ומותר האדם מן הבהמה אין כי הכל הבל 19
Hatima ya mwanadamu ni kama ile ya wanyama; wote wana mwisho unaofanana: Jinsi anavyokufa mnyama, ndivyo anavyokufa mwanadamu. Wote wana pumzi inayofanana; mwanadamu hana cha zaidi kuliko mnyama. Kila kitu ni ubatili.
הכל הולך אל מקום אחד הכל היה מן העפר והכל שב אל העפר 20
Wote huenda mahali panapofanana; wote hutoka mavumbini, mavumbini wote hurudi.
מי יודע רוח בני האדם--העלה היא למעלה ורוח הבהמה--הירדת היא למטה לארץ 21
Ni nani ajuaye kama roho ya mtu huenda juu na roho ya mnyama hushuka chini ardhini?”
וראיתי כי אין טוב מאשר ישמח האדם במעשיו--כי הוא חלקו כי מי יביאנו לראות במה שיהיה אחריו 22
Kwa hiyo nikaona kwamba hakuna kitu kilicho bora zaidi kwa mwanadamu kuliko kuifurahia kazi yake, kwa sababu hilo ndilo fungu lake. Kwa maana ni nani awezaye kumrudisha ili aje kuona kile kitakachotendeka baada yake?

< קֹהֶלֶת 3 >