< מלכים א 4 >

ויהי המלך שלמה מלך על כל ישראל 1
Basi Mfalme Solomoni akatawala Israeli yote.
ואלה השרים אשר לו עזריהו בן צדוק הכהן 2
Hawa ndio waliokuwa maafisa wake wakuu: Kuhani: Azaria mwana wa Sadoki;
אליחרף ואחיה בני שישא ספרים יהושפט בן אחילוד המזכיר 3
Elihorefu na Ahiya, wana wa Shisha: waandishi; Yehoshafati mwana wa Ahiludi: karani;
ובניהו בן יהוידע על הצבא וצדוק ואביתר כהנים 4
Benaya mwana wa Yehoyada: jemadari mkuu wa jeshi; Sadoki na Abiathari: makuhani;
ועזריהו בן נתן על הנצבים וזבוד בן נתן כהן רעה המלך 5
Azaria mwana wa Nathani: kiongozi wa maafisa wa wilaya; Zabudi mwana wa Nathani: kuhani na mshauri binafsi wa mfalme;
ואחישר על הבית ואדנירם בן עבדא על המס 6
Ahishari: msimamizi wa jumba la kifalme; Adoniramu mwana wa Abda: msimamizi wa kazi za kulazimisha.
ולשלמה שנים עשר נצבים על כל ישראל וכלכלו את המלך ואת ביתו חדש בשנה יהיה על אחד (האחד) לכלכל 7
Pia Solomoni alikuwa na watawala kumi na wawili wa wilaya katika Israeli yote, walioleta mahitaji kwa mfalme na kwa watu wa nyumbani kwa mfalme. Kila mmoja alitoa chakula kwa mwezi mmoja katika mwaka.
ואלה שמותם בן חור בהר אפרים 8
Majina yao ni haya: Ben-Huri: katika nchi ya vilima ya Efraimu;
בן דקר במקץ ובשעלבים ובית שמש ואילון בית חנן 9
Ben-Dekeri: katika Makasi, Shaalbimu, Beth-Shemeshi na Elon-Bethhanani;
בן חסד בארבות לו שכה וכל ארץ חפר 10
Ben-Hesedi: katika Arubothi (Soko na nchi yote ya Heferi zilikuwa zake);
בן אבינדב כל נפת דאר טפת בת שלמה היתה לו לאשה 11
Ben-Abinadabu: katika Nafoth-Dori (alimwoa Tafathi binti Solomoni);
בענא בן אחילוד תענך ומגדו וכל בית שאן אשר אצל צרתנה מתחת ליזרעאל מבית שאן עד אבל מחולה עד מעבר ליקמעם 12
Baana mwana wa Ahiludi: katika Taanaki na Megido, na katika Beth-Shani yote karibu na Sarethani chini ya Yezreeli, kuanzia Beth-Shani hadi Abel-Mehola kupita hadi Yokmeamu;
בן גבר ברמת גלעד לו חות יאיר בן מנשה אשר בגלעד לו חבל ארגב אשר בבשן--ששים ערים גדלות חומה ובריח נחשת 13
Ben-Geberi: katika Ramoth-Gileadi (makao ya Yairi mwana wa Manase katika Gileadi ilikuwa miji yake, pamoja na wilaya ya Argobu katika Bashani na miji yake mikubwa sitini yenye kuzungukwa na kuta zenye makomeo ya shaba);
אחינדב בן עדא מחנימה 14
Ahinadabu mwana wa Ido: katika Mahanaimu;
אחימעץ בנפתלי גם הוא לקח את בשמת בת שלמה--לאשה 15
Ahimaasi: katika Naftali (alikuwa amemwoa Basemathi binti Solomoni);
בענא בן חושי באשר ובעלות 16
Baana mwana wa Hushai: katika Asheri na katika Bealothi;
יהושפט בן פרוח ביששכר 17
Yehoshafati mwana wa Parua: katika Isakari;
שמעי בן אלא בבנימן 18
Shimei mwana wa Ela: katika Benyamini;
גבר בן ארי בארץ גלעד--ארץ סיחון מלך האמרי ועג מלך הבשן ונציב אחד אשר בארץ 19
Geberi mwana wa Uri: katika Gileadi (nchi ya Sihoni mfalme wa Waamori na nchi ya Ogu mfalme wa Bashani). Naye alikuwa ndiye mtawala pekee katika eneo hilo.
יהודה וישראל רבים כחול אשר על הים לרב אכלים ושתים ושמחים 20
Watu wa Yuda na Israeli walikuwa wengi kama mchanga wa pwani; walikula, wakanywa na kufurahi.
ושלמה היה מושל בכל הממלכות--מן הנהר ארץ פלשתים ועד גבול מצרים מגשים מנחה ועבדים את שלמה כל ימי חייו 21
Mfalme Solomoni akatawala katika falme zote kuanzia Mto Frati hadi nchi ya Wafilisti, hadi kwenye mpaka wa Misri. Nchi hizi zilileta ushuru na zilikuwa chini ya Solomoni, siku zote za maisha yake.
ויהי לחם שלמה ליום אחד שלשים כר סלת וששים כר קמח 22
Mahitaji ya Solomoni ya kila siku yalikuwa kori thelathini za unga laini, kori sitini za unga wa kawaida.
עשרה בקר בראים ועשרים בקר רעי--ומאה צאן לבד מאיל וצבי ויחמור וברברים אבוסים 23
Ngʼombe kumi wa zizini, ngʼombe ishirini wa malisho, kondoo na mbuzi mia moja, pamoja na ayala, paa, kulungu na kuku wazuri sana.
כי הוא רדה בכל עבר הנהר מתפסח ועד עזה--בכל מלכי עבר הנהר ושלום היה לו מכל עבריו--מסביב 24
Kwa kuwa Solomoni alitawala falme zote magharibi ya mto, kuanzia Tifsa hadi Gaza, naye akawa na amani pande zote.
וישב יהודה וישראל לבטח איש תחת גפנו ותחת תאנתו מדן ועד באר שבע--כל ימי שלמה 25
Wakati wa maisha ya Solomoni Yuda na Israeli, kuanzia Dani mpaka Beer-Sheba, wakaishi salama kila mtu chini ya mzabibu wake na chini ya mtini wake.
ויהי לשלמה ארבעים אלף ארות סוסים--למרכבו ושנים עשר אלף פרשים 26
Solomoni alikuwa na mabanda 4,000 ya magari ya vita, na farasi 12,000.
וכלכלו הנצבים האלה את המלך שלמה ואת כל הקרב אל שלחן המלך שלמה--איש חדשו לא יעדרו דבר 27
Maafisa wa eneo hilo, kila mmoja katika mwezi wake, walileta mahitaji kwa ajili ya Mfalme Solomoni na wote waliokula mezani mwa mfalme. Walihakikisha kuwa hakuna chochote kilichopungua.
והשערים והתבן לסוסים ולרכש--יבאו אל המקום אשר יהיה שם איש כמשפטו 28
Pia walileta sehemu walizopangiwa za shayiri na majani kwa ajili ya farasi wavutao magari na farasi wengine mahali palipostahili.
ויתן אלהים חכמה לשלמה ותבונה הרבה מאד ורחב לב--כחול אשר על שפת הים 29
Mungu akampa Solomoni hekima na akili kubwa, pia ufahamu mpana usiopimika kama mchanga ulioko pwani ya bahari.
ותרב חכמת שלמה מחכמת כל בני קדם ומכל חכמת מצרים 30
Hekima ya Solomoni ilikuwa kubwa kuliko hekima ya watu wote wa Mashariki na kubwa kuliko hekima yote ya Misri.
ויחכם מכל האדם מאיתן האזרחי והימן וכלכל ודרדע בני מחול ויהי שמו בכל הגוים סביב 31
Alikuwa na hekima kuliko kila mwandishi, akiwemo Ethani Mwezrahi: kuliko Hemani, Kalkoli na Darda, wana wa Maholi. Umaarufu wake ukaenea kwa mataifa yote yaliyomzunguka.
וידבר שלשת אלפים משל ויהי שירו חמשה ואלף 32
Akanena mithali 3,000 na nyimbo zake zilikuwa 1,005.
וידבר על העצים מן הארז אשר בלבנון ועד האזוב אשר יצא בקיר וידבר על הבהמה ועל העוף ועל הרמש ועל הדגים 33
Akaelezea maisha ya mimea kuanzia mwerezi wa Lebanoni hadi hisopo iotayo ukutani. Pia akafundisha kuhusu wanyama na ndege, wanyama wenye damu baridi, wakiwemo samaki.
ויבאו מכל העמים לשמע את חכמת שלמה--מאת כל מלכי הארץ אשר שמעו את חכמתו 34
Watu wa mataifa yote wakaja kusikiliza hekima ya Solomoni, waliotumwa na wafalme wote wa ulimwengu, waliokuwa wamesikia juu ya hekima yake.

< מלכים א 4 >