< דברי הימים א 6 >

בני לוי גרשון קהת ומררי 1
Wana wa Lawi walikuwa: Gershoni, Kohathi na Merari.
ובני קהת--עמרם יצהר וחברון ועזיאל 2
Wana wa Kohathi walikuwa: Amramu, Ishari, Hebroni na Uzieli.
ובני עמרם אהרן ומשה ומרים ובני אהרן--נדב ואביהוא אלעזר ואיתמר 3
Amramu alikuwa na wana: Aroni, Mose, na Miriamu. Aroni alikuwa na wana: Nadabu, Abihu, Eleazari na Ithamari.
אלעזר הוליד את פינחס פינחס הליד את אבישוע 4
Eleazari akamzaa Finehasi, Finehasi akamzaa Abishua,
ואבישוע הוליד את בקי ובקי הוליד את עזי 5
Abishua akamzaa Buki, Buki akamzaa Uzi,
ועזי הוליד את זרחיה וזרחיה הוליד את מריות 6
Uzi akamzaa Zerahia, Zerahia akamzaa Merayothi,
מריות הוליד את אמריה ואמריה הוליד את אחיטוב 7
Merayothi akamzaa Amaria, Amaria akamzaa Ahitubu,
ואחיטוב הוליד את צדוק וצדוק הוליד את אחימעץ 8
Ahitubu akamzaa Sadoki, Sadoki akamzaa Ahimaasi,
ואחימעץ הוליד את עזריה ועזריה הוליד את יוחנן 9
Ahimaasi akamzaa Azaria, Azaria akamzaa Yohanani,
ויוחנן הוליד את עזריה הוא אשר כהן בבית אשר בנה שלמה בירושלם 10
Yohanani akamzaa Azaria (ndiye alifanya kazi ya ukuhani katika Hekalu alilojenga Mfalme Solomoni huko Yerusalemu),
ויולד עזריה את אמריה ואמריה הוליד את אחיטוב 11
Azaria akamzaa Amaria, Amaria akamzaa Ahitubu,
ואחיטוב הוליד את צדוק וצדוק הוליד את שלום 12
Ahitubu akamzaa Sadoki, Sadoki akamzaa Shalumu,
ושלום הוליד את חלקיה וחלקיה הוליד את עזריה 13
Shalumu akamzaa Hilkia, Hilkia akamzaa Azaria,
ועזריה הוליד את שריה ושריה הוליד את יהוצדק 14
Azaria akamzaa Seraya, Seraya akamzaa Yehosadaki.
ויהוצדק הלך--בהגלות יהוה את יהודה וירושלם ביד נבכדנאצר 15
Yehosadaki alihamishwa wakati Bwana aliwapeleka uhamishoni watu wa Yuda na Yerusalemu kwa mkono wa Mfalme Nebukadneza.
בני לוי גרשם קהת ומררי 16
Wana wa Lawi walikuwa: Gershoni, Kohathi na Merari.
ואלה שמות בני גרשום לבני ושמעי 17
Haya ndiyo majina ya wana wa Gershoni: Libni na Shimei.
ובני קהת--עמרם ויצהר וחברון ועזיאל 18
Wana wa Kohathi walikuwa: Amramu, Ishari, Hebroni na Uzieli.
בני מררי מחלי ומשי ואלה משפחות הלוי לאבתיהם 19
Wana wa Merari walikuwa: Mahli na Mushi. Zifuatazo ni koo za Walawi zilizoorodheshwa kufuatana na baba zao:
לגרשום--לבני בנו יחת בנו זמה בנו 20
Wazao wa Gershoni: Gershoni akamzaa Libni, Libni akamzaa Yahathi, Yahathi akamzaa Zima,
יואח בנו עדו בנו זרח בנו יאתרי בנו 21
Zima akamzaa Yoa, Yoa akamzaa Ido, Ido akamzaa Zera, Zera akamzaa Yeatherai.
בני קהת--עמינדב בנו קרח בנו אסיר בנו 22
Wazao wa Kohathi: Kohathi akamzaa Aminadabu, Aminadabu akamzaa Kora, Kora akamzaa Asiri,
אלקנה בנו ואביסף בנו ואסיר בנו 23
Asiri akamzaa Elikana, Elikana akamzaa Ebiasafu, Ebiasafu akamzaa Asiri,
תחת בנו אוריאל בנו עזיה בנו ושאול בנו 24
Asiri akamzaa Tahathi, Tahathi akamzaa Urieli, Urieli akamzaa Uzia, Uzia akamzaa Shauli.
ובני אלקנה--עמשי ואחימות 25
Wazao wa Elikana walikuwa: Amasai na Ahimothi,
אלקנה--בנו (בני) אלקנה צופי בנו ונחת בנו 26
Ahimothi akamzaa Elikana, Elikana akamzaa Sofai, Sofai akamzaa Nahathi,
אליאב בנו ירחם בנו אלקנה בנו 27
Nahathi akamzaa Eliabu, Eliabu akamzaa Yerohamu, Yerohamu akamzaa Elikana, Elikana akamzaa Samweli.
ובני שמואל הבכר ושני ואביה 28
Wana wa Samweli walikuwa: Yoeli mzaliwa wake wa kwanza, na Abiya mwanawe wa pili.
בני מררי מחלי לבני בנו שמעי בנו עזה בנו 29
Wafuatao ndio wazao wa Merari: Merari akamzaa Mahli, Mahli akamzaa Libni, Libni akamzaa Shimei, Shimei akamzaa Uza,
שמעא בנו חגיה בנו עשיה בנו 30
Uza akamzaa Shimea, Shimea akamzaa Hagia, Hagia akamzaa Asaya.
ואלה אשר העמיד דויד על ידי שיר--בית יהוה ממנוח הארון 31
Hawa ndio watu ambao Daudi aliwaweka kuwa viongozi wa uimbaji katika nyumba ya Bwana, baada ya Sanduku la Agano kuletwa ili kukaa huko.
ויהיו משרתים לפני משכן אהל מועד בשיר עד בנות שלמה את בית יהוה בירושלם ויעמדו כמשפטם על עבודתם 32
Walihudumu kwa kuimba mbele ya Maskani, Hema la Kukutania, mpaka hapo Mfalme Solomoni alipojenga Hekalu la Bwana huko Yerusalemu. Walitimiza wajibu wao kulingana na taratibu walizokuwa wamewekewa.
ואלה העמדים ובניהם מבני הקהתי--הימן המשורר בן יואל בן שמואל 33
Wafuatao ni watu waliohudumu pamoja na wana wao: Kutoka ukoo wa Kohathi walikuwa: Hemani, mpiga kinanda, alikuwa mwana wa Yoeli, mwana wa Samweli,
בן אלקנה בן ירחם בן אליאל בן תוח 34
mwana wa Elikana, mwana wa Yerohamu, mwana wa Elieli, mwana wa Toa,
בן ציף (צוף) בן אלקנה בן מחת בן עמשי 35
mwana wa Sufu, mwana wa Elikana, mwana wa Mahathi, mwana wa Amasai,
בן אלקנה בן יואל בן עזריה בן צפניה 36
mwana wa Elikana, mwana wa Yoeli, mwana wa Azaria, mwana wa Sefania,
בן תחת בן אסיר בן אביסף בן קרח 37
mwana wa Tahathi, mwana wa Asiri, mwana wa Ebiasafu, mwana wa Kora,
בן יצהר בן קהת בן לוי בן ישראל 38
mwana wa Ishari, mwana wa Kohathi, mwana wa Lawi, mwana wa Israeli;
ואחיו אסף העמד על ימינו--אסף בן ברכיהו בן שמעא 39
na msaidizi wa Hemani alikuwa Asafu, aliyesimama mkono wa kuume: Asafu mwana wa Berekia, mwana wa Shimea,
בן מיכאל בן בעשיה בן מלכיה 40
mwana wa Mikaeli, mwana wa Baaseya, mwana wa Malkiya,
בן אתני בן זרח בן עדיה 41
mwana wa Ethni, mwana wa Zera, mwana wa Adaya,
בן איתן בן זמה בן שמעי 42
mwana wa Ethani, mwana wa Zima, mwana wa Shimei,
בן יחת בן גרשם בן לוי 43
mwana wa Yahathi, mwana wa Gershoni, mwana wa Lawi.
ובני מררי אחיהם על השמאול--איתן בן קישי בן עבדי בן מלוך 44
Na kutoka kwa walioshirikiana nao, Wamerari, mkono wake wa kushoto: Ethani mwana wa Kishi, mwana wa Abdi, mwana wa Maluki,
בן חשביה בן אמציה בן חלקיה 45
mwana wa Hashabia, mwana wa Amazia, mwana wa Hilkia,
בן אמצי בן בני בן שמר 46
mwana wa Amsi, mwana wa Bani, mwana wa Shemeri,
בן מחלי בן מושי בן מררי בן לוי 47
mwana wa Mahli, mwana wa Mushi, mwana wa Merari, mwana wa Lawi.
ואחיהם הלוים נתונים--לכל עבודת משכן בית האלהים 48
Ndugu zao wengine Walawi walipewa huduma nyingine za kuhudumia hema takatifu, nyumba ya Mungu.
ואהרן ובניו מקטירים על מזבח העולה ועל מזבח הקטרת לכל מלאכת קדש הקדשים ולכפר על ישראל ככל אשר צוה משה עבד האלהים 49
Lakini Aroni na uzao wake ndio waliokuwa na wajibu wa kutoa sadaka katika madhabahu ya sadaka ya kuteketezwa na kwenye madhabahu ya kufukizia uvumba pamoja na yote yaliyofanyika pa Patakatifu, wakifanya upatanisho kwa ajili ya Israeli, sawasawa na yale yote aliyoagiza Mose mtumishi wa Mungu.
ואלה בני אהרן--אלעזר בנו פינחס בנו אבישוע בנו 50
Hawa ndio waliokuwa wazao wa Aroni: Aroni akamzaa Eleazari, Eleazari akamzaa Finehasi, Finehasi akamzaa Abishua,
בקי בנו עזי בנו זרחיה בנו 51
Abishua akamzaa Buki, Buki akamzaa Uzi, Uzi akamzaa Zerahia,
מריות בנו אמריה בנו אחיטוב בנו 52
Zerahia akamzaa Merayothi, Merayothi akamzaa Amaria, Amaria akamzaa Ahitubu,
צדוק בנו אחימעץ בנו 53
Ahitubu akamzaa Sadoki, Sadoki akamzaa Ahimaasi.
ואלה מושבותם לטירותם בגבולם--לבני אהרן למשפחת הקהתי כי להם היה הגורל 54
Zifuatazo ni sehemu walizopewa ziwe nchi yao kwa ajili ya makazi yao (walipewa wazao wa Aroni waliotoka katika ukoo wa Wakohathi, kwa sababu kura ya kwanza iliwaangukia):
ויתנו להם את חברון בארץ יהודה ואת מגרשיה סביבתיה 55
Walipewa Hebroni katika nchi ya Yuda pamoja na sehemu ya malisho inayouzunguka.
ואת שדה העיר ואת חצריה--נתנו לכלב בן יפנה 56
Lakini mashamba pamoja na vijiji vilivyouzunguka mji alipewa Kalebu mwana wa Yefune.
ולבני אהרן נתנו את ערי המקלט--את חברון ואת לבנה ואת מגרשיה ואת יתר ואת אשתמע ואת מגרשיה 57
Kwa hiyo wazao wa Aroni walipewa miji ifuatayo pamoja na eneo la malisho: Hebroni (mji wa makimbilio), Libna, Yatiri, Eshtemoa,
ואת חילז ואת מגרשיה את דביר ואת מגרשיה 58
Hileni, Debiri,
ואת עשן ואת מגרשיה ואת בית שמש ואת מגרשיה 59
Ashani, Yuta na Beth-Shemeshi pamoja na maeneo yake ya malisho.
וממטה בנימן את גבע ואת מגרשיה ואת עלמת ואת מגרשיה ואת ענתות ואת מגרשיה כל עריהם שלש עשרה עיר במשפחותיהם 60
Kutoka kabila la Benyamini walipewa Gibeoni, Geba, Alemethi na Anathothi, pamoja na maeneo yake ya malisho. Miji hii kumi na mitatu iligawanywa miongoni mwa koo za Wakohathi.
ולבני קהת הנותרים ממשפחת המטה ממחצית מטה חצי מנשה בגורל--ערים עשר 61
Wazao waliobaki wa Wakohathi walipewa miji kumi kutoka koo za nusu ya kabila la Manase.
ולבני גרשום למשפחותם ממטה יששכר וממטה אשר וממטה נפתלי וממטה מנשה בבשן--ערים שלש עשרה 62
Wazao wa Gershoni, ukoo kwa ukoo, walipewa miji kumi na mitatu kutoka kwa makabila ya Isakari, Asheri na Naftali kutoka sehemu ya kabila la Manase huko Bashani.
לבני מררי למשפחותם ממטה ראובן וממטה גד וממטה זבלון בגורל--ערים שתים עשרה 63
Wazao wa Merari, ukoo kwa ukoo walipewa miji kumi na miwili kutoka makabila ya Reubeni, Gadi na Zabuloni.
ויתנו בני ישראל ללוים את הערים ואת מגרשיהם 64
Kwa hiyo Waisraeli waliwapa Walawi miji hii pamoja na maeneo yake ya malisho.
ויתנו בגורל ממטה בני יהודה וממטה בני שמעון וממטה בני בנימן--את הערים האלה אשר יקראו אתהם בשמות 65
Kutoka makabila ya Yuda, Simeoni na Benyamini walipewa miji iliyotajwa hapo juu.
וממשפחות בני קהת--ויהי ערי גבולם ממטה אפרים 66
Baadhi ya koo za Wakohathi walipewa kama nchi yao miji kutoka kabila la Efraimu.
ויתנו להם את ערי המקלט את שכם ואת מגרשיה--בהר אפרים ואת גזר ואת מגרשיה 67
Katika nchi ya vilima ya Efraimu walipewa Shekemu (mji wa makimbilio) na Gezeri,
ואת יקמעם ואת מגרשיה ואת בית חורון ואת מגרשיה 68
Yokmeamu, Beth-Horoni,
ואת אילון ואת מגרשיה ואת גת רמון ואת מגרשיה 69
Aiyaloni na Gath-Rimoni, pamoja na maeneo yake ya malisho.
וממחצית מטה מנשה את ענר ואת מגרשיה ואת בלעם ואת מגרשיה--למשפחת לבני קהת הנותרים 70
Kutoka nusu ya kabila la Manase, Waisraeli waliwapa koo za Wakohathi waliobaki miji ya Aneri na Bileamu pamoja na maeneo yake ya malisho.
לבני גרשום--ממשפחת חצי מטה מנשה את גולן בבשן ואת מגרשיה ואת עשתרות ואת מגרשיה 71
Wagershoni walipokea miji ifuatayo pamoja na maeneo yake ya malisho: Katika nusu ya kabila la Manase: walipewa Golani katika Bashani na pia Ashtarothi.
וממטה יששכר את קדש ואת מגרשיה את דברת ואת מגרשיה 72
Kutoka kabila la Isakari walipokea Kedeshi, Daberathi,
ואת ראמות ואת מגרשיה ואת ענם ואת מגרשיה 73
Ramothi na Anemu, pamoja na maeneo yake ya malisho.
וממטה אשר את משל ואת מגרשיה ואת עבדון ואת מגרשיה 74
Kutoka kabila la Asheri walipokea Mashali, Abdoni,
ואת חוקק ואת מגרשיה ואת רחב ואת מגרשיה 75
Hukoki na Rehobu, pamoja na maeneo yake ya malisho.
וממטה נפתלי את קדש בגליל ואת מגרשיה ואת חמון ואת מגרשיה ואת קריתים ואת מגרשיה 76
Kutoka kabila la Naftali walipokea Kedeshi katika Galilaya, Hamoni na Kiriathaimu pamoja na maeneo yake ya malisho.
לבני מררי הנותרים--ממטה זבלון את רמונו ואת מגרשיה את תבור ואת מגרשיה 77
Wamerari (Walawi waliobakia) walipokea miji ifuatayo: kutoka kabila la Zabuloni walipokea Yokneamu, Karta, Rimoni na Tabori pamoja na maeneo yake ya malisho.
ומעבר לירדן ירחו למזרח הירדן--ממטה ראובן את בצר במדבר ואת מגרשיה ואת יהצה ואת מגרשיה 78
Kutoka kabila la Reubeni, ngʼambo ya Yordani mashariki mwa Yeriko walipokea Bezeri ulioko jangwani, Yahasa,
ואת קדמות ואת מגרשיה ואת מיפעת ואת מגרשיה 79
Kedemothi na Mefaathi pamoja na maeneo yake ya malisho.
וממטה גד--את ראמות בגלעד ואת מגרשיה ואת מחנים ואת מגרשיה 80
Na kutoka kabila la Gadi walipokea Ramothi huko Gileadi, Mahanaimu,
ואת חשבון ואת מגרשיה ואת יעזיר ואת מגרשיה 81
Heshboni na Yazeri, pamoja na maeneo yake ya malisho.

< דברי הימים א 6 >