< Zabura 148 >

1 Yabi Ubangiji. Yabi Ubangiji daga sammai, yabe shi a bisa sammai.
Msifuni Yahwe. Msifuni Yahwe, ninyi mlio katika mbingu; msifuni yeye, ninyi mlio juu.
2 Yabe shi, dukanku mala’ikunsa, yabe shi, dukanku rundunarsa na sama.
Msifuni yeye, enyi malaika wake wote; msifuni yeye, majeshi ya malaika wake wote.
3 Yabe shi, rana da wata, yabe shi, dukanku taurari masu haskakawa.
Msifuni yeye, enyi jua na mwezi; msifuni yeye, nyota zote zing'aazo.
4 Yabe shi, ku bisa sammai da kuma ku ruwan bisa sarari.
Msifuni yeye, enyi mbingu zilizo juu zaidi na maji yaliyo juu ya anga.
5 Bari su yabi sunan Ubangiji, gama ya umarta aka kuwa halicce su.
Na vilisifu jina la Yahwe, maana aliamuru, navyo vikaumbwa.
6 Ya sa su a wurarensu har abada abadin; ya ba da umarnin da ba zai taɓa shuɗe ba.
Pia ameviimrisha milele na milele; naye alitoa amri ambayo haitabadilika.
7 Yabi Ubangiji daga duniya, ku manyan halittun teku da kuma dukan zurfafan teku,
Msifuni yeye kutoka nchi, ninyi viumbe wa baharini na viumbe vyote katika kina cha bahari,
8 walƙiya da ƙanƙara, dusar ƙanƙara da gizagizai, hadirin iskar da suke biyayya da umarnansa,
moto na mvua ya mawe, theluji na mawingu, upepo wa dhoruba ukitimiza neno lake.
9 ku duwatsu da dukan tuddai, itatuwa masu’ya’ya da dukan al’ul,
Msifuni yeye, enyi milima na vilima, miti ya matunda na mierezi yote,
10 namun jeji da dukan dabbobin gida, ƙanana halittu da tsuntsaye masu firiya,
wanyama pori na wanyama wafugwao, viumbe vitambaavyo na ndege.
11 sarakunan duniya da dukan al’ummai, ku sarakuna da dukan masu mulkin duniya,
Msifuni Yahwe, wafalme wa nchi na mataifa yote, wakuu na watawala wote wa nchi,
12 samari da’yan mata, tsofaffi da yara.
wote vijana wa kiume na vijana wa kike, wazee na watoto.
13 Bari su yabi sunan Ubangiji, gama sunansa ne kaɗai mafi ɗaukaka; darajarsa ta fi ƙarfin duniya da sammai.
Na walisifu jina la Yahwe, kwa kuwa jina lake pekee limetukuka na utukufu wake umeongezwa juu ya nchi na mbingu.
14 Ya tayar wa mutanensa ƙaho, yabon dukan tsarkakansa, na Isra’ila, mutanen da suke kurkusa da zuciyarsa. Yabi Ubangiji.
Naye ameyainua mapembe ya watu wake kwa ajili ya sifa kutoka kwa waaminifu wake wote, Waisraeli, watu wa karibu naye. Msifuni Yahwe.

< Zabura 148 >