< 1 Tarihi 3 >

1 Waɗannan su ne’ya’yan Dawuda maza da aka haifa masa a Hebron. Ɗan farinsa shi ne Amnon ɗan Ahinowam mutuniyar Yezireyel; na biyun, Daniyel ɗan Abigiyel mutuniyar Karmel;
Hawa ndio waliokuwa wana wa Daudi waliozaliwa huko Hebroni: Mzaliwa wa kwanza alikuwa Amnoni ambaye mama yake aliitwa Ahinoamu wa Yezreeli; wa pili, Danieli ambaye mama yake alikuwa Abigaili wa Karmeli;
2 na ukun, Absalom ɗan Ma’aka’yar Talmai sarkin Geshur; na huɗun, Adoniya ɗan Haggit;
wa tatu alikuwa Absalomu, ambaye mama yake alikuwa Maaka, binti Talmai mfalme wa Geshuri; wa nne, Adoniya, ambaye mama yake alikuwa Hagithi;
3 na biyar, Shefatiya ɗan Abital; da kuma na shida, Itireyam ta wurin matarsa Egla.
wa tano alikuwa Shefatia ambaye mama yake alikuwa Abitali; wa sita alikuwa Ithreamu, aliyezaliwa na mke wake Egla.
4 Waɗannan su ne aka haifa wa Dawuda a Hebron, inda ya yi mulki shekaru bakwai da wata shida. Dawuda ya yi mulki a Urushalima shekaru talatin da uku,
Hawa sita walizaliwa huko Hebroni ambako Daudi alitawala kwa miaka saba na miezi sita. Daudi alitawala Yerusalemu kwa miaka thelathini na mitatu,
5 kuma waɗannan su ne yaran da aka haifa masa a can. Shimeya, Shobab, Natan da Solomon. Waɗannan huɗu ne Bat-shuwa’yar Ammiyel ta haifa.
nao hawa ndio watoto wa Daudi waliozaliwa huko Yerusalemu: mkewe Bathsheba, binti Amieli, alimzalia Shamua, Shobabu, Nathani na Solomoni.
6 Akwai kuma Ibhar, Elishama, Elifelet,
Pia kulikuwa na wana wengine: Ibihari, Elishua, Elifeleti,
7 Noga, Nefeg, Yafiya,
Noga, Nefegi, Yafia,
8 Elishama, Eliyada da Elifelet, su tara ne duka.
Elishama, Eliada na Elifeleti; wote walikuwa tisa.
9 Dukan waɗannan’ya’yan Dawuda ne maza, ban da’ya’yansa maza ta wurin ƙwarƙwaransa. Tamar ita ce’yar’uwarsu.
Hawa wote walikuwa wana wa Daudi, mbali na wale wana waliozaliwa na masuria. Naye Tamari alikuwa dada yao.
10 Zuriyar Solomon su ne Rehobowam, da Abiya, da Asa, da Yehoshafat,
Mwana wa Solomoni alikuwa Rehoboamu, mwanawe huyo alikuwa Abiya, mwanawe huyo alikuwa Yehoshafati, mwanawe huyo alikuwa Asa,
11 da Yoram, da Ahaziya, da Yowash,
mwanawe huyo alikuwa Yehoramu, mwanawe huyo alikuwa Ahazia, mwanawe huyo alikuwa Yoashi,
12 da Amaziya, da Azariya, da Yotam,
mwanawe huyo alikuwa Amazia, mwanawe huyo alikuwa Azaria, mwanawe huyo alikuwa Yothamu,
13 da Ahaz, da Hezekiya da Manasse,
mwanawe huyo alikuwa Ahazi, mwanawe huyo alikuwa Hezekia, mwanawe huyo alikuwa Manase,
14 da Amon, da Yosiya.
mwanawe huyo alikuwa Amoni na mwanawe huyo alikuwa Yosia.
15 ’Ya’yan Yosiya maza su ne, Yohanan ɗan fari, Yehohiyakim ɗa na biyu, Zedekiya ɗa na uku Shallum ɗa na huɗu.
Wana wa Yosia walikuwa: Yohanani mzaliwa wake wa kwanza, Yehoyakimu mwanawe wa pili, wa tatu Sedekia, wa nne Shalumu.
16 Magādan Yehohiyakim su ne, Yekoniya ɗansa, da Zedekiya.
Walioingia mahali pa Yehoyakimu kama wafalme ni: Yekonia mwanawe, na Sedekia.
17 Zuriyar Yekoniya kamamme su ne, Sheyaltiyel,
Hawa ndio waliokuwa wazao wa Yekonia aliyekuwa mateka: Shealtieli mwanawe,
18 Malkiram, Fedahiya, Shenazzar, Yekamiya, Hoshama da Nedabiya.
Malkiramu, Pedaya, Shenasari, Yekamia, Hoshama na Nedabia.
19 ’Ya’yan Fedahiya su ne, Zerubbabel da Shimeyi.’Ya’yan Zerubbabel maza su ne, Meshullam da Hananiya. Shelomit ce’yar’uwarsu.
Wana wa Pedaya walikuwa: Zerubabeli na Shimei. Wana wa Zerubabeli walikuwa: Meshulamu na Hanania. Shelomithi alikuwa dada yao.
20 Akwai kuma waɗansu biyar, Hashuba, Ohel, Berekiya, Hasadiya da Yushab-Hesed.
Pia walikuwepo wengine watano: Hashuba, Oheli, Berekia, Hasadia na Yushab-Hesedi.
21 Zuriyar Hananiya su ne, Felatiya da Yeshahiya, Refahiya, Arnan, Obadiya da Shekaniya.
Wazao wa Hanania walikuwa: Pelatia na Yeshaya, na wana wa Refaya, na wana wa Arnani, na wana wa Obadia, na wana wa Shekania.
22 Zuriyar Shekaniya su ne, Shemahiya da’ya’yansa maza. Hattush, Igal, Bariya, Neyariya da Shafat, su shida ne duka.
Wazao wa Shekania: Shemaya na wanawe: Hatushi, Igali, Baria, Nearia na Shafati; jumla yao walikuwa sita.
23 ’Ya’yan Neyariya maza su ne, Eliyohenai, Hezekiya da Azrikam, su uku ne duka.
Wana wa Nearia walikuwa: Elioenai, Hizkia na Azrikamu; jumla yao watatu.
24 ’Ya’yan Eliyohenai su ne, Hodawiya, Eliyashib, Felahiya, Akkub, Yohanan, Delahiya da Anani, su bakwai ne duka.
Wana wa Elioenai walikuwa: Hodavia, Eliashibu, Pelaya, Akubu, Yohanani, Delaya na Anani; jumla yao wote saba.

< 1 Tarihi 3 >