< Θρῆνοι 3 >
1 ἐγὼ ἀνὴρ ὁ βλέπων πτωχείαν ἐν ῥάβδῳ θυμοῦ αὐτοῦ ἐπ’ ἐμέ
Mimi ndiye mtu aliyeona mateso kwa fimbo ya ghadhabu yake.
2 παρέλαβέν με καὶ ἀπήγαγεν εἰς σκότος καὶ οὐ φῶς
Amenifukuzia mbali na kunifanya nitembee gizani wala si katika nuru;
3 πλὴν ἐν ἐμοὶ ἐπέστρεψεν χεῖρα αὐτοῦ ὅλην τὴν ἡμέραν
hakika, amegeuza mkono wake dhidi yangu tena na tena, mchana kutwa.
4 ἐπαλαίωσεν σάρκας μου καὶ δέρμα μου ὀστέα μου συνέτριψεν
Amefanya ngozi yangu na nyama yangu kuchakaa na ameivunja mifupa yangu.
5 ἀνῳκοδόμησεν κατ’ ἐμοῦ καὶ ἐκύκλωσεν κεφαλήν μου καὶ ἐμόχθησεν
Amenizingira na kunizunguka kwa uchungu na taabu.
6 ἐν σκοτεινοῖς ἐκάθισέν με ὡς νεκροὺς αἰῶνος
Amenifanya niishi gizani kama wale waliokufa.
7 ἀνῳκοδόμησεν κατ’ ἐμοῦ καὶ οὐκ ἐξελεύσομαι ἐβάρυνεν χαλκόν μου
Amenizungushia ukuta ili nisiweze kutoroka, amenifunga kwa minyororo mizito.
8 καί γε κεκράξομαι καὶ βοήσω ἀπέφραξεν προσευχήν μου
Hata ninapoita au kulia ili kuomba msaada, anakataa kupokea maombi yangu.
9 ἀνῳκοδόμησεν ὁδούς μου ἐνέφραξεν τρίβους μου ἐτάραξεν
Ameizuia njia yangu kwa mapande ya mawe, amepotosha njia zangu.
10 ἄρκος ἐνεδρεύουσα αὐτός μοι λέων ἐν κρυφαίοις
Kama dubu aviziaye, kama simba mafichoni,
11 κατεδίωξεν ἀφεστηκότα καὶ κατέπαυσέν με ἔθετό με ἠφανισμένην
ameniburuta kutoka njia, akanirarua na kuniacha bila msaada.
12 ἐνέτεινεν τόξον αὐτοῦ καὶ ἐστήλωσέν με ὡς σκοπὸν εἰς βέλος
Amevuta upinde wake na kunifanya mimi niwe lengo kwa ajili ya mishale yake.
13 εἰσήγαγεν τοῖς νεφροῖς μου ἰοὺς φαρέτρας αὐτοῦ
Alinichoma moyo wangu kwa mishale iliyotoka kwenye podo lake.
14 ἐγενήθην γέλως παντὶ λαῷ μου ψαλμὸς αὐτῶν ὅλην τὴν ἡμέραν
Nimekuwa kichekesho kwa watu wangu wote, wananidhihaki kwa wimbo mchana kutwa.
15 ἐχόρτασέν με πικρίας ἐμέθυσέν με χολῆς
Amenijaza kwa majani machungu na kunishibisha kwa nyongo.
16 καὶ ἐξέβαλεν ψήφῳ ὀδόντας μου ἐψώμισέν με σποδόν
Amevunja meno yangu kwa changarawe, amenikanyagia mavumbini.
17 καὶ ἀπώσατο ἐξ εἰρήνης ψυχήν μου ἐπελαθόμην ἀγαθὰ
Amani yangu imeondolewa, nimesahau kufanikiwa ni nini.
18 καὶ εἶπα ἀπώλετο νεῖκός μου καὶ ἡ ἐλπίς μου ἀπὸ κυρίου
Kwa hiyo nasema, “Fahari yangu imeondoka na yale yote niliyokuwa nimetarajia kutoka kwa Bwana.”
19 ἐμνήσθην ἀπὸ πτωχείας μου καὶ ἐκ διωγμοῦ μου πικρίας καὶ χολῆς μου
Nayakumbuka mateso yangu na kutangatanga kwangu, uchungu na nyongo.
20 μνησθήσεται καὶ καταδολεσχήσει ἐπ’ ἐμὲ ἡ ψυχή μου
Ninayakumbuka vyema, nayo nafsi yangu imezimia ndani yangu.
21 ταύτην τάξω εἰς τὴν καρδίαν μου διὰ τοῦτο ὑπομενῶ
Hata hivyo najikumbusha neno hili na kwa hiyo ninalo tumaini.
Kwa sababu ya upendo mkuu wa Bwana, hatuangamii, kwa kuwa huruma zake hazikomi kamwe.
Ni mpya kila asubuhi, uaminifu wako ni mkuu.
Nimeiambia nafsi yangu, “Bwana ni fungu langu, kwa hiyo nitamngojea.”
25 ἀγαθὸς κύριος τοῖς ὑπομένουσιν αὐτόν ψυχῇ ἣ ζητήσει αὐτὸν ἀγαθὸν
Bwana ni mwema kwa wale ambao tumaini lao ni kwake, kwa yule ambaye humtafuta;
26 καὶ ὑπομενεῖ καὶ ἡσυχάσει εἰς τὸ σωτήριον κυρίου
ni vyema kungojea kwa utulivu kwa ajili ya wokovu wa Bwana.
27 ἀγαθὸν ἀνδρὶ ὅταν ἄρῃ ζυγὸν ἐν νεότητι αὐτοῦ
Ni vyema mtu kuchukua nira bado angali kijana.
28 καθήσεται κατὰ μόνας καὶ σιωπήσεται ὅτι ἦρεν ἐφ’ ἑαυτῷ
Na akae peke yake awe kimya, kwa maana Bwana ameiweka juu yake.
Na azike uso wake mavumbini bado panawezekana kuwa na matumaini.
30 δώσει τῷ παίοντι αὐτὸν σιαγόνα χορτασθήσεται ὀνειδισμῶν
Na atoe shavu lake kwa yule ampigaye, na ajazwe na aibu.
31 ὅτι οὐκ εἰς τὸν αἰῶνα ἀπώσεται κύριος
Kwa kuwa watu hawakatiliwi mbali na Bwana milele.
32 ὅτι ὁ ταπεινώσας οἰκτιρήσει κατὰ τὸ πλῆθος τοῦ ἐλέους αὐτοῦ
Ingawa huleta huzuni, ataonyesha huruma, kwa kuwa upendo wake usiokoma ni mkuu.
33 ὅτι οὐκ ἀπεκρίθη ἀπὸ καρδίας αὐτοῦ καὶ ἐταπείνωσεν υἱοὺς ἀνδρός
Kwa maana hapendi kuwaletea mateso au huzuni watoto wa wanadamu.
34 τοῦ ταπεινῶσαι ὑπὸ τοὺς πόδας αὐτοῦ πάντας δεσμίους γῆς
Kuwaponda chini ya nyayo wafungwa wote katika nchi,
35 τοῦ ἐκκλῖναι κρίσιν ἀνδρὸς κατέναντι προσώπου ὑψίστου
Kumnyima mtu haki zake mbele za Aliye Juu Sana,
36 καταδικάσαι ἄνθρωπον ἐν τῷ κρίνεσθαι αὐτὸν κύριος οὐκ εἶπεν
kumnyima mtu haki: Je, Bwana asione mambo kama haya?
37 τίς οὕτως εἶπεν καὶ ἐγενήθη κύριος οὐκ ἐνετείλατο
Nani awezaye kusema nalo likatendeka kama Bwana hajaamuru?
38 ἐκ στόματος ὑψίστου οὐκ ἐξελεύσεται τὰ κακὰ καὶ τὸ ἀγαθόν
Je, si ni kwenye kinywa cha Aliye Juu Sana ndiko yatokako maafa na mambo mema?
39 τί γογγύσει ἄνθρωπος ζῶν ἀνὴρ περὶ τῆς ἁμαρτίας αὐτοῦ
Mwanadamu yeyote aliye hai aweza kulalamika wakati anapoadhibiwa kwa ajili ya dhambi zake?
40 ἐξηρευνήθη ἡ ὁδὸς ἡμῶν καὶ ἠτάσθη καὶ ἐπιστρέψωμεν ἕως κυρίου
Tuzichunguze njia zetu na kuzijaribu, na tumrudie Bwana Mungu.
41 ἀναλάβωμεν καρδίας ἡμῶν ἐπὶ χειρῶν πρὸς ὑψηλὸν ἐν οὐρανῷ
Tuinue mioyo yetu pamoja na mikono yetu kwa Mungu mbinguni, na tuseme:
42 ἡμαρτήσαμεν ἠσεβήσαμεν καὶ οὐχ ἱλάσθης
“Tumetenda dhambi na kuasi nawe hujasamehe.
43 ἐπεσκέπασας ἐν θυμῷ καὶ ἀπεδίωξας ἡμᾶς ἀπέκτεινας οὐκ ἐφείσω
“Umejifunika mwenyewe kwa hasira na kutufuatilia; umetuchinja bila huruma.
44 ἐπεσκέπασας νεφέλην σεαυτῷ εἵνεκεν προσευχῆς
Unajifunika mwenyewe kwa wingu, ili pasiwe na ombi litakaloweza kupenya.
45 καμμύσαι με καὶ ἀπωσθῆναι ἔθηκας ἡμᾶς ἐν μέσῳ τῶν λαῶν
Umetufanya takataka na uchafu miongoni mwa mataifa.
46 διήνοιξαν ἐφ’ ἡμᾶς τὸ στόμα αὐτῶν πάντες οἱ ἐχθροὶ ἡμῶν
“Adui zetu wote wamefumbua vinywa vyao wazi dhidi yetu.
47 φόβος καὶ θυμὸς ἐγενήθη ἡμῖν ἔπαρσις καὶ συντριβή
Tumeteseka kwa hofu kuu na shida ya ghafula, uharibifu na maangamizi.”
48 ἀφέσεις ὑδάτων κατάξει ὁ ὀφθαλμός μου ἐπὶ τὸ σύντριμμα τῆς θυγατρὸς τοῦ λαοῦ μου
Vijito vya machozi vinatiririka kutoka machoni mwangu, kwa sababu watu wangu wameangamizwa.
49 ὁ ὀφθαλμός μου κατεπόθη καὶ οὐ σιγήσομαι τοῦ μὴ εἶναι ἔκνηψιν
Macho yangu yatatiririka machozi bila kukoma, bila kupata nafuu,
50 ἕως οὗ διακύψῃ καὶ ἴδῃ κύριος ἐξ οὐρανοῦ
hadi Bwana atazame chini kutoka mbinguni na kuona.
51 ὁ ὀφθαλμός μου ἐπιφυλλιεῖ ἐπὶ τὴν ψυχήν μου παρὰ πάσας θυγατέρας πόλεως
Lile ninaloliona huniletea huzuni nafsini kwa sababu ya wanawake wote wa mji wangu.
52 θηρεύοντες ἐθήρευσάν με ὡς στρουθίον οἱ ἐχθροί μου δωρεάν
Wale waliokuwa adui zangu bila sababu wameniwinda kama ndege.
53 ἐθανάτωσαν ἐν λάκκῳ ζωήν μου καὶ ἐπέθηκαν λίθον ἐπ’ ἐμοί
Walijaribu kukomesha maisha yangu ndani ya shimo na kunitupia mawe;
54 ὑπερεχύθη ὕδωρ ἐπὶ κεφαλήν μου εἶπα ἀπῶσμαι
maji yalifunika juu ya kichwa changu, nami nikafikiri nilikuwa karibu kukatiliwa mbali.
55 ἐπεκαλεσάμην τὸ ὄνομά σου κύριε ἐκ λάκκου κατωτάτου
Nililiitia jina lako, Ee Bwana, kutoka vina vya shimo.
56 φωνήν μου ἤκουσας μὴ κρύψῃς τὰ ὦτά σου εἰς τὴν δέησίν μου
Ulisikia ombi langu: “Usikizibie masikio yako kilio changu nikuombapo msaada.”
57 εἰς τὴν βοήθειάν μου ἤγγισας ἐν ᾗ σε ἡμέρᾳ ἐπεκαλεσάμην εἶπάς μοι μὴ φοβοῦ
Ulikuja karibu nilipokuita, nawe ukasema, “Usiogope.”
58 ἐδίκασας κύριε τὰς δίκας τῆς ψυχῆς μου ἐλυτρώσω τὴν ζωήν μου
Ee Bwana, ulichukua shauri langu, ukaukomboa uhai wangu.
59 εἶδες κύριε τὰς ταραχάς μου ἔκρινας τὴν κρίσιν μου
Umeona, Ee Bwana, ubaya niliotendewa. Tetea shauri langu!
60 εἶδες πᾶσαν τὴν ἐκδίκησιν αὐτῶν εἰς πάντας διαλογισμοὺς αὐτῶν ἐν ἐμοί
Umeona kina cha kisasi chao, mashauri yao yote mabaya dhidi yangu.
61 ἤκουσας τὸν ὀνειδισμὸν αὐτῶν πάντας τοὺς διαλογισμοὺς αὐτῶν κατ’ ἐμοῦ
Ee Bwana, umesikia matukano yao, mashauri yao yote mabaya dhidi yangu:
62 χείλη ἐπανιστανομένων μοι καὶ μελέτας αὐτῶν κατ’ ἐμοῦ ὅλην τὴν ἡμέραν
kile adui zangu wanachonongʼona na kunungʼunikia dhidi yangu mchana kutwa.
63 καθέδραν αὐτῶν καὶ ἀνάστασιν αὐτῶν ἐπίβλεψον ἐπὶ τοὺς ὀφθαλμοὺς αὐτῶν
Watazame! Wakiwa wameketi au wamesimama, wananidhihaki katika nyimbo zao.
64 ἀποδώσεις αὐτοῖς ἀνταπόδομα κύριε κατὰ τὰ ἔργα τῶν χειρῶν αὐτῶν
Uwalipe kile wanachostahili, Ee Bwana, kwa yale ambayo mikono yao imetenda.
65 ἀποδώσεις αὐτοῖς ὑπερασπισμὸν καρδίας μόχθον σου αὐτοῖς
Weka pazia juu ya mioyo yao, laana yako na iwe juu yao!
66 καταδιώξεις ἐν ὀργῇ καὶ ἐξαναλώσεις αὐτοὺς ὑποκάτω τοῦ οὐρανοῦ κύριε
Wafuatilie katika hasira na uwaangamize kutoka chini ya mbingu za Bwana.