< Psalm 78 >
1 Nimm zu Ohren, mein Volk, mein Gesetz, zu meines Mundes Reden neigt euer Ohr!
Utenzi wa Asafu. Enyi watu wangu, sikieni mafundisho yangu, sikilizeni maneno ya kinywa changu.
2 Ich will in Sprüchen meinen Mund auftun, ich lasse aus der Vorzeit Rätsel hervorquellen.
Nitafungua kinywa changu kwa mafumbo, nitazungumza mambo yaliyofichika, mambo ya kale:
3 Was wir gehört und erkannt, und unsere Väter uns erzählt,
yale ambayo tuliyasikia na kuyajua, yale ambayo baba zetu walituambia.
4 Nicht wollen wir es verhehlen ihren Söhnen, wollen dem späteren Geschlecht Jehovahs Lob erzählen, und Seine Stärke und Seine Wunder, die Er getan hat.
Hatutayaficha kwa watoto wao; tutakiambia kizazi kijacho matendo yastahiliyo sifa ya Bwana, uweza wake, na maajabu aliyoyafanya.
5 Und Er richtete ein Zeugnis auf in Jakob und setzte ein Gesetz in Israel ein, das unseren Vätern Er gebot, sie ihren Söhnen zu wissen zu tun.
Aliagiza amri kwa Yakobo na akaweka sheria katika Israeli, ambazo aliwaamuru baba zetu wawafundishe watoto wao,
6 Auf daß es erkennete das spätere Geschlecht, die Söhne, die geboren werden, daß sie aufstünden und es ihren Söhnen erzähleten.
ili kizazi kijacho kizijue, pamoja na watoto ambao watazaliwa, nao pia wapate kuwaeleza watoto wao.
7 Und daß sie auf Gott ihr Zutrauen setzeten, und nicht der Taten Gottes vergäßen, und Seine Gebote bewahrten.
Ndipo wangeweka tumaini lao kwa Mungu, nao wasingesahau matendo yake, bali wangalizishika amri zake.
8 Und nicht wie ihre Väter würden ein aufrührerisches und widerspenstiges Geschlecht, dessen Herz nicht fest war, und dessen Geist nicht treu war mit Gott.
Ili wasifanane na baba zao, waliokuwa kizazi cha ukaidi na uasi, ambao roho zao hazikuwa na uaminifu kwake, ambao roho zao hazikumwamini.
9 Die Söhne Ephraims waren bewaffnete Bogenschützen, die am Tage des Kampfes sich umkehrten.
Watu wa Efraimu, ingawa walijifunga pinde, walikimbia siku ya vita.
10 Sie hielten den Bund Gottes nicht, und weigerten sich, in Seinem Gesetz zu wandeln.
Hawakulishika agano la Mungu na walikataa kuishi kwa sheria yake.
11 Und sie vergaßen Seiner Taten und Seiner Wunder, die Er sie sehen ließ.
Walisahau aliyokuwa ameyatenda, maajabu aliyokuwa amewaonyesha.
12 Vor ihren Vätern tat Er Wunder im Lande Ägypten, in Zoans Gefilde.
Alitenda miujiza machoni mwa baba zao, huko Soani, katika nchi ya Misri.
13 Er spaltete das Meer und führte sie hindurch, und stellte die Wasser wie einen Haufen auf.
Aliigawanya bahari akawapitisha, alifanya maji yasimame imara kama ukuta.
14 Und Er führte sie am Tag in einer Wolke, und die ganze Nacht im Lichte des Feuers.
Aliwaongoza kwa wingu mchana na kwa nuru kutoka kwenye moto usiku kucha.
15 Er spaltete in der Wüste Felsen, und tränkte sie viel wie aus Abgründen.
Alipasua miamba jangwani na akawapa maji tele kama bahari,
16 Und Bächlein ließ Er aus der Felsklippe ausgehen, und Wasser wie Flüsse herabflie-ßen.
alitoa vijito kutoka kwenye jabali lililochongoka, akayafanya maji yatiririke kama mito.
17 Und noch fuhren sie fort zu sündigen gegen Ihn, sich in der Dürre dem Höchsten zu widersetzen.
Lakini waliendelea kutenda dhambi dhidi yake, wakiasi jangwani dhidi ya Aliye Juu Sana.
18 Und sie versuchten Gott in ihrem Herzen, und fragten um Speise für ihre Seele.
Kwa makusudi walimjaribu Mungu, wakidai vyakula walivyovitamani.
19 Und sie redeten wider Gott, sie sagten: Kann Gott in der Wüste einen Tisch zurichten?
Walinena dhidi ya Mungu, wakisema, “Je, Mungu aweza kuandaa meza jangwani?
20 Siehe, Er schlug den Felsen und Wasser floß und Bäche fluteten; wird Er auch Brot geben können? wird Er Fleisch bereiten Seinem Volk?
Alipopiga mwamba, maji yalitoka kwa nguvu, vijito vikatiririka maji mengi. Lakini je, aweza kutupa chakula pia? Je, anaweza kuwapa watu wake nyama?”
21 Darum hörte Jehovah, und Er wütete, und Feuer loderte auf gegen Jakob, und Zorn stieg auch auf wider Israel.
Bwana alipowasikia, alikasirika sana, moto wake ukawa dhidi ya Yakobo, na ghadhabu yake ikawaka dhidi ya Israeli,
22 Weil sie an Gott nicht glaubten und auf Sein Heil nicht vertrauten.
kwa kuwa hawakumwamini Mungu, wala kuutumainia ukombozi wake.
23 Und Er gebot den Ätherkreisen oben und öffnete des Himmels Türen.
Hata hivyo alitoa amri kwa anga zilizo juu na kufungua milango ya mbingu,
24 Und Er ließ Manna auf sie regnen, zu essen, und gab ihnen Korn des Himmels.
akawanyeshea mana ili watu wale; aliwapa nafaka ya mbinguni.
25 Brot der Gewaltigen aß der Mann, Zehrung sandte Er ihnen zur Sättigung.
Watu walikula mkate wa malaika, akawatumia chakula chote ambacho wangeliweza kula.
26 Und Er ließ herfahren am Himmel den Ostwind, und trieb in Seiner Stärke den Südwind her.
Aliachia upepo wa mashariki kutoka kwenye mbingu na kuuongoza upepo wa kusini kwa uwezo wake.
27 Und ließ Fleisch regnen auf sie wie Staub, und wie Sand der Meere das geflügelte Gevögel.
Aliwanyeshea nyama kama mavumbi, ndege warukao kama mchanga wa pwani.
28 Und ließ sie fallen mitten in sein Lager, rings um seine Wohnungen.
Aliwafanya washuke ndani ya kambi yao, kuzunguka mahema yao yote.
29 Und sie aßen und wurden sehr satt. Er brachte ihnen, wonach sie gelüsteten.
Walikula na kusaza, kwa maana alikuwa amewapa kile walichotamani.
30 Sie waren ihren Gelüsten nicht entfremdet, ihre Speise war noch in ihrem Munde,
Kabla hawajamaliza kula walichokitamani, hata kilipokuwa kingali bado vinywani mwao,
31 Da stieg auf wider sie der Zorn Gottes. Und Er würgte unter ihren Fetten, und streckte nieder Israels Jünglinge.
hasira ya Mungu ikawaka juu yao, akawaua wale waliokuwa na nguvu zaidi miongoni mwao, akiwaangusha vijana wa Israeli.
32 Bei all dem sündigten sie noch und glaubten nicht an Seine Wunder.
Licha ya haya yote, waliendelea kutenda dhambi, licha ya maajabu yake, hawakuamini.
33 Und Er ließ ihre Tage sich verzehren in Nichtigkeit, und ihre Jahre in Bestürzung.
Kwa hiyo akamaliza siku zao katika ubatili na miaka yao katika vitisho.
34 Wenn Er sie würgte, fragen sie nach Ihm, und kehrten zurück und verlangten frühe nach Gott.
Kila mara Mungu alipowaua baadhi yao, waliosalia walimtafuta, walimgeukia tena kwa shauku.
35 Und sie gedachten, daß Gott ihr Fels und Gott, der Allerhöchste, ihr Erlöser sei.
Walikumbuka kwamba Mungu alikuwa Mwamba wao, kwamba Mungu Aliye Juu Sana alikuwa Mkombozi wao.
36 Und sie beredeten Ihn mit ihrem Munde und redeten Ihm Falsches mit ihrer Zunge.
Lakini walimdanganya kwa vinywa vyao, wakisema uongo kwa ndimi zao,
37 Ihr Herz aber war nicht fest bei Ihm und waren nicht treu in Seinem Bund.
mioyo yao haikuwa thabiti kwake, wala hawakuwa waaminifu katika agano lake.
38 Er aber ist erbarmungsvoll, Er sühnte die Missetat und verdarb sie nicht, und kehrte vielmals zurück von Seinem Zorn und erweckte nicht all Seinen Grimm.
Hata hivyo alikuwa na huruma, alisamehe maovu yao na hakuwaangamiza. Mara kwa mara alizuia hasira yake, wala hakuchochea ghadhabu yake yote.
39 Und Er gedachte, daß Fleisch sie sind, ein Hauch, der hingeht und nicht zurückkehrt.
Alikumbuka kwamba wao walikuwa nyama tu, upepo upitao ambao haurudi.
40 Wie oft waren sie widerspenstig wider Ihn in der Wüste, machten Ihm Schmerzen im Wüstenland.
Mara ngapi walimwasi jangwani na kumhuzunisha nyikani!
41 Und sie versuchten wieder Gott, und machten Kummer dem Heiligen Israels.
Walimjaribu Mungu mara kwa mara, wakamkasirisha yeye Aliye Mtakatifu wa Israeli.
42 Sie gedachten nicht Seiner Hand des Tages, da Er aus der Drangsal sie einlöste.
Hawakukumbuka uwezo wake, siku aliyowakomboa kutoka kwa mtesi,
43 Wie Er tat Seine Zeichen in Ägypten und Seine Wahrzeichen in Zoans Gefilde.
siku aliyoonyesha ishara zake za ajabu huko Misri, maajabu yake huko Soani.
44 Und Er verwandelte in Blut ihre Ströme und ihre Bächlein, daß sie nicht trinken konnten.
Aligeuza mito yao kuwa damu, hawakuweza kunywa maji kutoka vijito vyao.
45 Er sandte wider sie das Ungeziefer und es fraß sie, und den Frosch und er verdarb sie.
Aliwapelekea makundi ya mainzi yakawala, na vyura wakawaharibu.
46 Und Er gab dem Käfer ihr Gewächs und ihren Erwerb der Heuschrecke.
Aliruhusu tunutu kuharibu mimea yao, mazao yao kwa nzige.
47 Er zerschlug mit Hagel ihren Weinstock und mit Schloßen ihre Maulbeerfeigenbäume.
Aliharibu mizabibu yao kwa mvua ya mawe na mikuyu yao kwa mvua iliyochangamana na theluji.
48 Und ihr Getier gab Er dem Hagel preis und ihre Viehherden den Glühkohlen.
Aliwaachia mifugo yao mvua ya mawe, akayapiga makundi ya wanyama wao kwa radi.
49 Er sandte wider sie Seines Zornes Glut, Wut und Unwille und Drangsal, eine Entsendung böser Engel.
Aliwafungulia hasira yake kali, ghadhabu yake, hasira na uadui, na kundi la malaika wa kuharibu.
50 Er ebnete Seinem Zorn den Steig, und hielt ihre Seele nicht zurück vom Tod, und gab der Pest ihr Leben preis.
Aliitengenezea njia hasira yake, hakuwaepusha na kifo, bali aliwaachia tauni.
51 Und Er schlug alle Erstgeburt in Ägypten, die Erstlinge der Vollkraft in den Zelten Chams.
Aliwapiga wazaliwa wote wa kwanza wa Misri, matunda ya kwanza ya ujana katika mahema ya Hamu.
52 Und wie Schafe ließ Er aufbrechen Sein Volk und geleitete es wie eine Herde in der Wüste.
Lakini aliwatoa watu wake kama kundi, akawaongoza kama kondoo kupitia jangwani.
53 Und Er führte sie sicher, daß sie vor nichts schauderten; und ihre Feinde deckte das Meer.
Aliwaongoza salama, wala hawakuogopa, bali bahari iliwameza adui zao.
54 Und brachte sie zur Grenze Seines Heiligtums, zum Berge da, den Seine Rechte hat erworben.
Hivyo akawaleta hadi kwenye mpaka wa nchi yake takatifu, hadi nchi ya vilima ambayo mkono wake wa kuume ulikuwa umeitwaa.
55 Und trieb die Völkerschaften aus vor ihnen, und ließ es ihnen zufallen, nach dem Stricke als Erbe, und ließ die Stämme Israels in ihren Zelten wohnen.
Aliyafukuza mataifa mbele yao, na kuwagawia nchi zao kama urithi, aliwakalisha makabila ya Israeli katika makao yao.
56 Sie aber versuchten und erbitterten Gott, den Allerhöchsten, und hielten nicht Seine Zeugnisse.
Lakini wao walimjaribu Mungu, na kuasi dhidi ya Yeye Aliye Juu Sana, wala hawakuzishika sheria zake.
57 Und wichen zurück und wurden treulos wie ihre Väter, und kehrten sich ab wie ein trüglicher Bogen;
Kama baba zao, hawakuwa thabiti wala waaminifu, wakawa wasioweza kutegemewa kama upinde wenye kasoro.
58 Und reizten Ihn durch ihre Opferhöhen, und erregten Ihn zum Eifer mit ihren Schnitzbildern.
Wakamkasirisha Mungu kwa mahali pao pa juu pa kuabudia miungu, wakachochea wivu wake kwa sanamu zao.
59 Gott hörte es und wütete, und verschmähte Israel sehr;
Wakati Mungu alipowasikia, alikasirika sana, akamkataa Israeli kabisa.
60 Er gab dahin die Wohnung Schilos, das Zelt, darin unter Menschen Er wohnte,
Akaiacha hema ya Shilo, hema aliyokuwa ameiweka katikati ya wanadamu.
61 Und gab Seine Stärke in Gefangenschaft, und Seinen Schmuck in des Drängers Hand;
Akalipeleka Sanduku la nguvu zake utumwani, utukufu wake mikononi mwa adui.
62 Er überantwortete Sein Volk dem Schwerte und wütete wider Sein Erbe.
Aliachia watu wake wauawe kwa upanga, akaukasirikia sana urithi wake.
63 Es fraß das Feuer Seine Jünglinge, und Seine Jungfrauen wurden nicht gefreit.
Moto uliwaangamiza vijana wao, na wanawali wao hawakuimbiwa nyimbo za arusi,
64 Es fielen Seine Priester durch das Schwert, und Seine Witwen weinten nicht.
makuhani wao waliuawa kwa upanga, wala wajane wao hawakuweza kulia.
65 Aber der Herr erwachte, wie ein Schlafender, wie ein Held aufjauchzt vom Wein.
Ndipo Bwana alipoamka kama vile kuamka usingizini, kama vile mtu aamkavyo kutoka kwenye bumbuazi la mvinyo.
66 Und schlug Seine Dränger von hinten, und ewige Schmach legte Er auf sie.
Aliwapiga na kuwashinda adui zake, akawatia katika aibu ya milele.
67 Aber Er verschmähte Josephs Zelt, und wählte den Stamm Ephraim nicht.
Ndipo alipozikataa hema za Yosefu, hakulichagua kabila la Efraimu,
68 Und Er erwählte Jehudahs Stamm, den Berg Zion, den Er liebte.
lakini alilichagua kabila la Yuda, Mlima Sayuni, ambao aliupenda.
69 Und baute wie die Höhen Sein Heiligtum, wie die Erde, die auf ewig Er gegründet hat.
Alijenga patakatifu pake kama vilele, kama dunia ambayo aliimarisha milele.
70 Und erwählte David, Seinen Knecht, und nahm ihn von der Schafe Hürden.
Akamchagua Daudi mtumishi wake na kumtoa kwenye mazizi ya kondoo.
71 Hinter den Milchschafen weg brachte Er ihn, daß er weide Jakob, Sein Volk, und Israel, Sein Erbe.
Kutoka kuchunga kondoo alimleta kuwa mchungaji wa watu wake Yakobo, wa Israeli urithi wake.
72 Und er weidete sie nach der Rechtschaffenheit seines Herzens, und führte sie nach der Einsicht seiner Hände.
Naye Daudi aliwachunga kwa uadilifu wa moyo, kwa mikono ya ustadi aliwaongoza.