< Psalm 149 >

1 Hallelujah! Singet Jehovah ein neues Lied, Sein Lob in der Versammlung der Heiligen.
Msifuni Bwana. Mwimbieni Bwana wimbo mpya, sifa zake katika kusanyiko la watakatifu.
2 Israel, sei fröhlich in Dem, so Ihn gemacht hat! Die Söhne Zions sollen frohlocken in ihrem König!
Israeli na washangilie katika Muumba wao, watu wa Sayuni na wafurahi katika Mfalme wao.
3 Sie sollen loben Seinen Namen in Reigen, singt Ihm Psalmen auf Pauke und Harfe!
Na walisifu jina lake kwa kucheza na wampigie muziki kwa matari na kinubi.
4 Denn Wohlgefallen hat Jehovah an Seinem Volke. Die Elenden schmückt Er mit Heil.
Kwa maana Bwana anapendezwa na watu wake, anawavika wanyenyekevu taji ya wokovu.
5 Jauchzen sollen in Herrlichkeit die Heiligen, auf ihren Lagern jubeln.
Watakatifu washangilie katika heshima hii, na waimbe kwa shangwe vitandani mwao.
6 Mit ihren Kehlen Gott erhöhen, und in ihrer Hand das zweischneidige Schwert,
Sifa za Mungu na ziwe vinywani mwao na upanga ukatao kuwili mikononi mwao,
7 Zu üben Rache an den Völkerschaften, an den Volksstämmen Strafen.
ili walipize mataifa kisasi na adhabu juu ya mataifa,
8 Zu binden ihre Könige mit Ketten, und ihre Herrlichen mit eisernen Fußschellen.
wawafunge wafalme wao kwa minyororo, wakuu wao kwa pingu za chuma,
9 An ihnen das geschriebene Gericht zu tun. Solche Ehre haben alle Seine Heiligen. Hallelujah!
ili kuwafanyia hukumu iliyoandikwa dhidi yao. Huu ndio utukufu wa watakatifu wake wote. Msifuni Bwana.

< Psalm 149 >