< Psalm 132 >

1 Gedenke, Jehovah, an David, an all sein Elend.
Wimbo wa kwenda juu. Ee Bwana, mkumbuke Daudi na taabu zote alizozistahimili.
2 An ihn, der Jehovah schwor, gelobte dem Gewaltigen Jakobs:
Aliapa kiapo kwa Bwana na akaweka nadhiri kwa Yule Mwenye Nguvu wa Yakobo:
3 Ich gehe nicht hinein in meines Hauses Zelt, steige nicht hinauf auf das Ruhebett meiner Lagerstätte.
“Sitaingia nyumbani mwangu au kwenda kitandani mwangu:
4 Ich gebe meinen Augen keinen Schlaf, den Augenwimpern keinen Schlummer;
sitaruhusu usingizi katika macho yangu, wala kope zangu kusinzia,
5 Bis ich gefunden habe einen Ort für Jehovah, Wohnungen für den Gewaltigen Jakobs.
mpaka nitakapompatia Bwana mahali, makao kwa ajili ya Yule Mwenye Nguvu wa Yakobo.”
6 Siehe, wir hörten von Ihm in Ephratha, wir fanden Ihn in dem Gefilde des Waldes.
Tulisikia habari hii huko Efrathi, tulikutana nayo katika mashamba ya Yaara:
7 Laßt uns zu Seinen Wohnungen eingehen, anbeten zu Seiner Füße Schemel.
“Twendeni kwenye makao yake, na tuabudu kwenye kiti cha kuwekea miguu yake;
8 Mache Dich auf, Jehovah, zu Deiner Ruhe, Du und die Lade Deiner Stärke.
inuka, Ee Bwana, uje mahali pako pa kupumzikia, wewe na Sanduku la nguvu zako.
9 Laß Deine Priester sich kleiden in Gerechtigkeit, und jubeln Deine Heiligen.
Makuhani wako na wavikwe haki, watakatifu wako na waimbe kwa furaha.”
10 Um Davids, Deines Knechtes willen wende nicht zurück das Angesicht Deines Gesalbten.
Kwa ajili ya Daudi mtumishi wako, usimkatae mpakwa mafuta wako.
11 Jehovah hat dem David Wahrheit geschworen. Nimmer wird Er davon zurückgehen: Von deines Leibes Frucht will Ich dir setzen auf den Thron.
Bwana alimwapia Daudi kiapo, kiapo cha uhakika ambacho hatakitangua: “Nitamweka mmoja wa wazao wako mwenyewe katika kiti chako cha enzi,
12 Wenn deine Söhne halten Meinen Bund und Mein Zeugnis, das Ich sie lehre, sollen auch ihre Söhne fort und fort sitzen auf deinem Thron.
kama wanao watashika Agano langu na sheria ninazowafundisha, ndipo wana wao watarithi kiti chako cha enzi milele na milele.”
13 Denn Jehovah hat Sich Zion erwählt, zum Wohnsitz für Sich ersehnt.
Kwa maana Bwana ameichagua Sayuni, amepaonea shauku pawe maskani yake:
14 Dies ist Meine Ruhe fort und fort, hier will Ich wohnen; denn Ich habe es ersehnt.
“Hapa ni mahali pangu pa kupumzika milele na milele; hapa ndipo nitakapoketi nikitawala, kwa sababu nimepaonea shauku:
15 Ich werde seine Zehrung mit Segen segnen; werde seine Dürftigen sättigen mit Brot.
Nitambariki kwa kumpa mahitaji tele: nitashibisha maskini wake kwa chakula.
16 Und seine Priester will Ich Heil anziehen lassen, und seine Heiligen sollen jubeln.
Nitawavika makuhani wake wokovu, nao watakatifu wake watadumu wakiimba kwa furaha.
17 Da will Ich David sprossen lassen ein Horn, will Meinem Gesalbten eine Leuchte zurichten.
“Hapa nitamchipushia Daudi pembe, na kuweka taa kwa ajili ya masiya wangu.
18 Seine Feinde will Ich Scham anziehen lassen, aber auf ihm soll erblühen sein Diadem.
Adui zake nitawavika aibu, bali taji kichwani pake itangʼaa sana.”

< Psalm 132 >