< Psalm 130 >

1 Aus den Tiefen rufe ich zu Dir, Jehovah.
Wimbo wa kwenda juu. Kutoka vilindini ninakulilia, Ee Bwana.
2 Herr, höre auf meine Stimme, es mögen Deine Ohren aufmerken auf die Stimme meines Flehens.
Ee Bwana, sikia sauti yangu. Masikio yako na yawe masikivu kwa kilio changu unihurumie.
3 Wenn Du, Jah, Missetaten behältst, wer wird, o Herr, bestehen?
Kama wewe, Ee Bwana, ungeweka kumbukumbu ya dhambi, Ee Bwana, ni nani angeliweza kusimama?
4 Doch ist bei Dir Vergebung, daß man Dich fürchte.
Lakini kwako kuna msamaha, kwa hiyo wewe unaogopwa.
5 Ich hoffe auf Jehovah, meine Seele hofft, und Seines Wortes warte ich.
Namngojea Bwana, nafsi yangu inangojea, katika neno lake naweka tumaini langu.
6 Meine Seele ist auf den Herrn, mehr als die Hüter auf den Morgen.
Nafsi yangu inamngojea Bwana kuliko walinzi waingojeavyo asubuhi, naam, kuliko walinzi waingojeavyo asubuhi.
7 Warte auf Jehovah, Israel; denn bei Jehovah ist Barmherzigkeit und mit Ihm viel Erlösung.
Ee Israeli, mtumaini Bwana, maana kwa Bwana kuna upendo usiokoma, na kwake kuna ukombozi kamili.
8 Und Er wird Israel lösen von allen seinen Missetaten.
Yeye mwenyewe ataikomboa Israeli kutoka dhambi zao zote.

< Psalm 130 >