< Jesaja 43 >

1 Und nun, so spricht Jehovah, dein Schöpfer, o Jakob, und dein Bildner, o Israel. Fürchte nicht; denn Ich habe dich erlöst, gerufen bei deinem Namen. Mein bist du.
Lakini sasa hili ndilo asemalo Bwana, yeye aliyekuumba, ee Yakobo, yeye aliyekuhuluku, ee Israeli: “Usiogope kwa maana nimekukomboa, nimekuita wewe kwa jina lako, wewe u wangu.
2 Wenn du durch das Wasser hindurchgehst, will Ich bei dir sein, und durch die Flüsse, so werden sie dich nicht überfluten. So du durch das Feuer gehst, sollst du nicht versengt werden, noch soll die Flamme an dir brennen.
Unapopita kwenye maji makuu, nitakuwa pamoja nawe, unapopita katika mito ya maji, hayatakugharikisha. Utakapopita katika moto, hutaungua, miali ya moto haitakuunguza.
3 Denn Ich bin Jehovah, dein Gott, der Heilige Israels, dein Heiland; Ich habe als deine Sühne Ägypten, Kusch und Seba an deiner Statt gegeben.
Kwa kuwa Mimi ndimi Bwana, Mungu wako, yeye Aliye Mtakatifu wa Israeli, Mwokozi wako. Ninaitoa Misri kuwa fidia yako, Kushi na Seba badala yako.
4 Weil du kostbar bist in Meinen Augen, bist du verherrlicht, und Ich liebe dich, und gebe den Menschen hin statt deiner, und Volksstämme statt deiner Seele.
Kwa kuwa wewe ni wa thamani na wa kuheshimiwa machoni pangu, nami kwa kuwa ninakupenda, nitatoa watu badala yako na mataifa badala ya maisha yako.
5 Fürchte dich nicht, denn Ich bin mit dir; vom Aufgang lasse Ich deinen Samen kommen und bringe dich zusammen vom Abend;
Usiogope, kwa kuwa mimi nipo pamoja nawe, nitawaleta watoto wako kutoka mashariki, na kukukusanya kutoka magharibi.
6 Zur Mitternacht spreche Ich: Gib her! und zum Süden: Wehre nicht! Bringe herein Meine Söhne von der Ferne und Meine Töchter vom Ende der Erde!
Nitaiambia kaskazini, ‘Watoe!’ nayo kusini, ‘Usiwazuie.’ Walete wana wangu kutoka mbali, na binti zangu kutoka miisho ya dunia:
7 Jeglichen, der genannt ist nach Meinem Namen, den habe Ich zu Meiner Herrlichkeit geschaffen, ihn gebildet und ihn gemacht.
kila mmoja ambaye ameitwa kwa Jina langu, niliyemuumba kwa utukufu wangu, niliyemhuluku na kumfanya.”
8 Bringe heraus das Volk, das blind ist und hat Augen, und die Tauben, die Ohren haben.
Uwaongoze wale wenye macho lakini hawaoni, wenye masikio lakini hawasikii.
9 Kommt zusammen alle Völkerschaften zumal, und sammelt euch ihr Volksstämme. Wer unter ihnen saget solches an, und läßt uns Früheres hören? Sie mögen ihre Zeugen geben und sich rechtfertigen, und sie werden hören und sagen: Wahrheit ist es!
Mataifa yote yanakutanika pamoja, na makabila yanakusanyika. Ni nani miongoni mwao aliyetangulia kutuambia haya, na kututangazia mambo yaliyopita? Walete mashahidi wao ili kuwathibitisha kuwa walikuwa sahihi, ili wengine waweze kusikia, waseme, “Ni kweli.”
10 Ihr seid Mir Zeugen, spricht Jehovah, und Mein Knecht, Den Ich erwählt, auf daß ihr wisset und Mir glaubet und einsehet, daß Ich es bin. Vor Mir ward kein Gott gebildet, und nach Mir wird keiner sein.
“Ninyi ni mashahidi wangu,” asema Bwana, “na mtumishi wangu niliyemchagua, ili mpate kunijua na kuniamini, na kutambua kwamba Mimi ndiye. Kabla yangu hakuna mungu aliyefanyizwa, wala hatakuwepo mwingine baada yangu.
11 Ich, Ich bin Jehovah, und kein Heiland ist außer Mir.
Mimi, naam mimi, ndimi Bwana, zaidi yangu hakuna mwokozi.
12 Ich habe es angesagt und habe gerettet und hören lassen, und kein Fremder war unter euch; und ihr seid Meine Zeugen, spricht Jehovah, und Ich bin Gott.
Nimedhihirisha, kuokoa na kutangaza: Mimi, wala si mungu mgeni katikati yenu. Ninyi ni mashahidi wangu,” asema Bwana, “kwamba Mimi ndimi Mungu.
13 Auch seit ein Tag ist, bin Ich. Und niemand errettet aus Meiner Hand. Ich tue, wer wendet es zurück?
Naam, tangu siku za kale, Mimi ndiye. Hakuna hata mmoja awezaye kuokoa kutoka mkononi wangu. Mimi ninapotenda, ni nani awezaye kutangua?”
14 So spricht Jehovah, euer Erlöser, der Heilige Israels: Um euretwillen habe Ich gen Babel gesandt und alle Riegel heruntergebracht, und die Chaldäer, deren Jubel ist in den Schiffen.
Hili ndilo Bwana asemalo, Mkombozi wako, yeye Aliye Mtakatifu wa Israeli: “Kwa ajili yenu nitatumana Babeli na kuwaleta Wakaldayo wote kama wakimbizi, katika meli walizozionea fahari.
15 Ich, Jehovah, bin euer Heiliger, der Israel erschaffen, euer König.
Mimi ndimi Bwana, yeye Aliye Mtakatifu wako, Muumba wa Israeli, Mfalme wako.”
16 So spricht Jehovah, Der einen Weg gibt in dem Meer und Steige in starken Wassern.
Hili ndilo asemalo Bwana, yeye aliyefanya njia baharini, mahali pa kupita kwenye maji mengi,
17 Der Streitwagen und Roß läßt herauskommen, die Streitmacht und den Starken; da liegen sie beisammen, sie stehen nimmer auf, sie sind verloschen; wie der Flachs erlöschen sie.
aliyeyakokota magari ya vita na farasi, jeshi pamoja na askari wa msaada, nao wakalala huko, wala hawatainuka tena kamwe, wakakomeshwa, na wakazimika kama utambi:
18 Gedenkt nicht an das Frühere, und auf die Vorzeit merket nicht!
“Msiyakumbuke mambo yaliyopita, wala msiyatafakari mambo ya zamani.
19 Siehe, Neues tue Ich, nun wird es emporsprossen. Werdet ihr es nicht erkennen? Ich mache in der Wüste einen Weg, im Wüstenland Flüsse.
Tazama, nitafanya jambo jipya! Sasa litachipuka, je, hamtalitambua? Nitafanya njia jangwani na vijito vya maji katika nchi kame.
20 Mich wird verherrlichen des Feldes Wild, Drachen und Käuzlein, daß Wasser Ich gegeben in der Wüste, Flüsse im Wüstenland, zu tränken Mein auserwähltes Volk.
Wanyama wa mwituni wataniheshimu, mbweha na bundi, kwa sababu ninawapatia maji jangwani, na vijito katika nchi kame, ili kuwapa watu wangu maji, wale niliowachagua,
21 Dies Volk habe Ich Mir gebildet, es soll Mein Lob erzählen.
watu wale niliowaumba kwa ajili yangu, ili wapate kutangaza sifa zangu.
22 Und nicht, daß du Mich hättest gerufen, Jakob, daß du um Mich dich gemüht hättest, Israel.
“Hata hivyo hukuniita mimi, ee Yakobo, hujajitaabisha kwa ajili yangu, ee Israeli.
23 Du hast Mir nicht Schafe zu deinen Brandopfern hereingebracht, noch Mich durch Schlachtopfer verherrlicht. Ich habe dich nicht mit Speiseopfern dienen lassen, nicht mit Weihrauch dich ermüdet.
Hujaniletea kondoo kwa ajili ya sadaka za kuteketezwa, wala kuniheshimu kwa dhabihu zako. Sikukulemea kwa sadaka za nafaka wala kukuchosha kwa kuhitaji uvumba.
24 Du hast Mir nicht für Silber Kalmus gekauft, hast Mich nicht in dem Fette deiner Opfer schwelgen lassen; du ließest Mich dienen mit deinen Sünden, und Mich hast du ermüdet mit deinen Missetaten.
Hukuninunulia uvumba wowote wenye manukato, wala hukunipa kwa ukarimu mafuta ya wanyama wa dhabihu zako. Lakini umenilemea kwa dhambi zako, na kunitaabisha kwa makosa yako.
25 Ich, Ich bin es, Der deine Übertretungen ausgewischt, wegen Meiner, und habe deiner Sünden nicht gedacht.
“Mimi, naam mimi, ndimi nizifutaye dhambi zako, kwa ajili yangu mwenyewe, wala sizikumbuki dhambi zako tena.
26 Gedenke Meiner, laß uns zusammen rechten; erzähle du, daß du dich rechtfertigst.
Tafakari mambo yaliyopita, njoo na tuhojiane, leta shauri lako uweze kupewa haki yako.
27 Dein erster Vater hat gesündigt, und deine Dolmetscher sind abgefallen von Mir.
Baba yako wa kwanza alitenda dhambi, wasemaji wako wameasi dhidi yangu.
28 Und Ich entweihe die Obersten der Heiligkeit, und gebe Jakob zum Bann und Israel der Verhöhnung.
Kwa hiyo nitawaaibisha wakuu wa Hekalu lako, nami nitamtoa Yakobo aangamizwe, na Israeli adhihakiwe.

< Jesaja 43 >