< Amos 9 >

1 Ich sah den Herrn auf dem Altare stehen, und Er sprach: Schlag auf den Knauf, daß die Schwellen beben, und zertrümmere sie auf ihrer aller Haupt, und ihre Nachkommen will Ich mit dem Schwert erwürgen, und kein Flüchtling soll von ihnen entfliehen, und kein Entrinnender von ihnen wird entkommen.
Nilimwona Bwana akiwa amesimama kando ya madhabahu, naye akasema: “Piga vichwa vya nguzo ili vizingiti vitikisike. Viangushe juu ya vichwa vya watu wote; na wale watakaosalia nitawaua kwa upanga. Hakuna awaye yote atakayekimbia, hakuna atakayetoroka.
2 Bohrten sie durch in die Hölle, so holte meine Hand sie von da; und stiegen sie auf in den Himmel, so würde Ich sie von da herniederbringen. (Sheol h7585)
Wajapojichimbia chini mpaka kwenye vina vya kuzimu, kutoka huko mkono wangu utawatoa. Wajapopanda juu hadi kwenye mbingu, kutoka huko nitawashusha. (Sheol h7585)
3 Und versteckten sie sich auf Karmels Spitze, Ich forschte sie von da heraus und holte sie; und verbärgen sie sich vor meinen Augen in des Meeres Grund, so geböte Ich von da der Schlange, daß sie sie beiße.
Wajapojificha juu ya kilele cha Karmeli, huko nitawawinda na kuwakamata. Wajapojificha kutoka kwenye uso wangu katika vilindi vya bahari, huko nako nitaamuru joka kuwauma.
4 Und wenn sie vor ihren Feinden her in die Gefangenschaft ziehen, werde Ich von da dem Schwert gebieten, daß es sie erwürge, und setze Mein Auge auf sie zum Bösen und nicht zum Guten.
Wajapopelekwa uhamishoni na adui zao, huko nako nitaamuru upanga uwaue. Nitawakazia macho yangu kwa mabaya wala si kwa mazuri.”
5 Und der Herr Jehovah der Heerscharen ist es, Der die Erde anrührt und sie zerfließt, und alle trauern, die darauf wohnen; und es soll ganz über sie aufsteigen wie ein Strom, und versinken wie vom Strome Ägyptens.
Bwana, Bwana Mwenye Nguvu Zote, yeye agusaye dunia nayo ikayeyuka, na wote wakaao ndani mwake wakaomboleza: nayo nchi yote huinuka kama Naili, kisha hushuka kama mto wa Misri;
6 Er baut in den Himmeln Seine Stufen, und Sein Gewölbe, über der Erde gründet Er es. Er ruft des Meeres Wassern und gießt sie aus über der Erde Flächen! Jehovah ist Sein Name.
yeye ambaye hujenga jumba lake la kifalme katika mbingu na kuisimika misingi yake juu ya dunia, yeye aitaye maji ya bahari na kuyamwaga juu ya uso wa nchi: Bwana ndilo jina lake.
7 Seid ihr Mir nicht gleich der Kuschiter Söhne, ihr Söhne Israels, spricht Jehovah. Habe Ich nicht Israel heraufgebracht aus dem Lande Ägypten, und aus Kaphthor die Philister, und Aram aus Kir?
“Je, Waisraeli, ninyi si sawa kwangu kama Wakushi?” asema Bwana. “Je, sikuleta Israeli kutoka Misri, Wafilisti kutoka Kaftori, na Washamu kutoka Kiri?
8 Siehe, die Augen des Herrn Jehovah sind wider das sündhafte Königreich, daß Ich es vernichte vom Angesicht des Bodens; nur will Ich nicht ganz vernichten Jakobs Haus, spricht Jehovah.
“Hakika macho ya Bwana Mwenyezi yako juu ya ufalme wenye dhambi. Nami nitauangamiza kutoka kwenye uso wa dunia: hata hivyo sitaiangamiza kabisa nyumba ya Yakobo,” asema Bwana.
9 Denn siehe, Ich gebiete und lasse umherwandern unter allen Völkerschaften das Haus Israel, wie man im Siebe umherschwingt, und kein Körnchen soll auf die Erde fallen.
“Kwa kuwa nitatoa amri, na nitaipepeta nyumba ya Israeli miongoni mwa mataifa yote, kama vile nafaka ipepetwavyo katika ungo, na hakuna hata punje moja itakayoanguka chini.
10 Durch das Schwert sollen sterben alle Sünder Meines Volkes, die sprechen: Nicht erreicht, nicht begegnet uns das Böse.
Watenda dhambi wote miongoni mwa watu wangu watauawa kwa upanga, wale wote wasemao, ‘Maafa hayatatupata wala kutukuta.’
11 An demselben Tage werde Ich Davids Hütte aufrichten, die gefallen; und vermauern ihre Durchbrüche, aufrichten, was daran eingerissen ist, und sie bauen wie in den Tagen der Ewigkeit.
“Katika siku ile nitaisimamisha hema ya Daudi iliyoanguka. Nitakarabati mahali palipobomoka na kujenga upya magofu yake, na kuijenga kama ilivyokuwa awali,
12 Auf daß sie in Erbbesitz nehmen den Überrest Edoms und alle Völkerschaften, über die Mein Name wird gerufen, spricht Jehovah, Der solches tut.
ili wapate kuyamiliki mabaki ya Edomu, na mataifa yote yale yanayobeba Jina langu,” asema Bwana ambaye atafanya mambo haya.
13 Siehe, spricht Jehovah, die Tage kommen, da der Pflüger an den Schnitter reicht, und der Weinbeeren tritt an den, der Samen sät, und von süßem Most die Berge triefen und alle Hügel zerfließen.
“Siku zinakuja,” asema Bwana, “wakati mvunaji atatanguliwa na mkulima, naye mpanzi atatanguliwa na yeye akamuaye zabibu. Divai mpya itadondoka kutoka milimani, na kutiririka kutoka vilima vyote.
14 Und Ich wende zurück die Gefangenschaft Meines Volkes Israel; und sie werden die verwüsteten Städte bauen und darin wohnen, und Weingärten pflanzen und deren Wein trinken, und Gärten machen und essen ihre Frucht.
Nitawarejesha tena watu wangu Israeli waliohamishwa; wataijenga tena miji iliyoachwa magofu, nao wataishi ndani mwake. Watapanda mizabibu na kunywa divai yake; watalima bustani na kula matunda yake.
15 Und Ich werde sie pflanzen auf ihren Boden; und sie sollen nicht mehr ausgerissen werden aus ihrem Boden, den Ich ihnen gab, spricht Jehovah, dein Gott.
Nitaipanda Israeli katika nchi yao wenyewe, hawatangʼolewa tena kutoka nchi ambayo nimewapa,” asema Bwana Mungu wenu.

< Amos 9 >