< Psalm 78 >
1 Eine Unterweisung; von Asaph. Höre, mein Volk, meine Lehre, neiget eure Ohren zu den Reden meines Mundes!
Utenzi wa Asafu. Enyi watu wangu, sikieni mafundisho yangu, sikilizeni maneno ya kinywa changu.
2 Ich will meinen Mund zu einem Spruche öffnen, will Rätsel vortragen aus alter Zeit,
Nitafungua kinywa changu kwa mafumbo, nitazungumza mambo yaliyofichika, mambo ya kale:
3 was wir gehört und gelernt und was unsre Väter uns erzählt haben.
yale ambayo tuliyasikia na kuyajua, yale ambayo baba zetu walituambia.
4 Es wurde ihren Söhnen nicht vorenthalten, sondern sie haben dem spätern Geschlecht den Ruhm des HERRN erzählt, seine Macht und seine Wunder, die er getan,
Hatutayaficha kwa watoto wao; tutakiambia kizazi kijacho matendo yastahiliyo sifa ya Bwana, uweza wake, na maajabu aliyoyafanya.
5 nämlich, daß er ein Zeugnis aufstellte in Jakob und ein Gesetz gab in Israel, von welchem er unsern Vätern befahl, es ihren Kindern kundzutun,
Aliagiza amri kwa Yakobo na akaweka sheria katika Israeli, ambazo aliwaamuru baba zetu wawafundishe watoto wao,
6 damit das spätere Geschlecht es wisse, die Kinder, die noch sollten geboren werden, und damit auch sie, wenn sie aufgewachsen wären, es ihren Kindern erzählten;
ili kizazi kijacho kizijue, pamoja na watoto ambao watazaliwa, nao pia wapate kuwaeleza watoto wao.
7 daß diese auf Gott ihr Vertrauen setzten und nicht vergäßen die Taten Gottes und seine Gebote befolgten
Ndipo wangeweka tumaini lao kwa Mungu, nao wasingesahau matendo yake, bali wangalizishika amri zake.
8 und nicht würden wie ihre Väter, ein abtrünniges und widerspenstiges Geschlecht, ein Geschlecht, das kein festes Herz hatte, und dessen Geist nicht treu war gegen Gott.
Ili wasifanane na baba zao, waliokuwa kizazi cha ukaidi na uasi, ambao roho zao hazikuwa na uaminifu kwake, ambao roho zao hazikumwamini.
9 Die Kinder Ephraims, geübte Bogenschützen, wandten um am Tage der Schlacht.
Watu wa Efraimu, ingawa walijifunga pinde, walikimbia siku ya vita.
10 Sie bewahrten den Bund Gottes nicht und wollten nicht nach seinem Gesetze wandeln.
Hawakulishika agano la Mungu na walikataa kuishi kwa sheria yake.
11 Und sie vergaßen seine Taten und seine Wunder, die er ihnen erzeigt.
Walisahau aliyokuwa ameyatenda, maajabu aliyokuwa amewaonyesha.
12 Vor ihren Vätern hatte er Wunder getan im Lande Ägypten, im Gefilde Zoan.
Alitenda miujiza machoni mwa baba zao, huko Soani, katika nchi ya Misri.
13 Er spaltete das Meer und führte sie hindurch und türmte die Wasser auf wie einen Damm,
Aliigawanya bahari akawapitisha, alifanya maji yasimame imara kama ukuta.
14 und leitete sie bei Tag mit einer Wolke und während der ganzen Nacht mit einem hellen Feuer.
Aliwaongoza kwa wingu mchana na kwa nuru kutoka kwenye moto usiku kucha.
15 Er spaltete Felsen in der Wüste und tränkte sie wie mit großen Fluten,
Alipasua miamba jangwani na akawapa maji tele kama bahari,
16 und ließ Bäche aus dem Felsen hervorspringen und Wasser herabfließen in Strömen.
alitoa vijito kutoka kwenye jabali lililochongoka, akayafanya maji yatiririke kama mito.
17 Dennoch fuhren sie fort, wider ihn zu sündigen und den Höchsten zu erzürnen in der Wüste.
Lakini waliendelea kutenda dhambi dhidi yake, wakiasi jangwani dhidi ya Aliye Juu Sana.
18 Und sie versuchten Gott in ihrem Herzen, indem sie Speise forderten nach ihrem Gelüste.
Kwa makusudi walimjaribu Mungu, wakidai vyakula walivyovitamani.
19 Und sie redeten wider Gott und sprachen: «Kann Gott einen Tisch bereiten in der Wüste?
Walinena dhidi ya Mungu, wakisema, “Je, Mungu aweza kuandaa meza jangwani?
20 Siehe, er hat den Felsen geschlagen, daß Wasser flossen und Bäche sich ergossen. Kann er aber auch Brot geben? Wird er seinem Volke Fleisch verschaffen?»
Alipopiga mwamba, maji yalitoka kwa nguvu, vijito vikatiririka maji mengi. Lakini je, aweza kutupa chakula pia? Je, anaweza kuwapa watu wake nyama?”
21 Darum, als der HERR das hörte, ward er entrüstet, und Feuer entbrannte wider Jakob, ja, Zorn stieg auf über Israel,
Bwana alipowasikia, alikasirika sana, moto wake ukawa dhidi ya Yakobo, na ghadhabu yake ikawaka dhidi ya Israeli,
22 weil sie Gott nicht glaubten und nicht auf seine Hilfe vertrauten.
kwa kuwa hawakumwamini Mungu, wala kuutumainia ukombozi wake.
23 Und er gebot den Wolken droben und öffnete die Türen des Himmels;
Hata hivyo alitoa amri kwa anga zilizo juu na kufungua milango ya mbingu,
24 und er ließ Manna auf sie regnen zum Essen und gab ihnen Himmelskorn.
akawanyeshea mana ili watu wale; aliwapa nafaka ya mbinguni.
25 Der Mensch aß Engelsbrot; er sandte ihnen Speise genug.
Watu walikula mkate wa malaika, akawatumia chakula chote ambacho wangeliweza kula.
26 Er erregte den Ostwind am Himmel und führte durch seine Kraft den Südwind herbei,
Aliachia upepo wa mashariki kutoka kwenye mbingu na kuuongoza upepo wa kusini kwa uwezo wake.
27 ließ Fleisch auf sie regnen wie Staub und beschwingte Vögel wie Sand am Meer,
Aliwanyeshea nyama kama mavumbi, ndege warukao kama mchanga wa pwani.
28 und ließ sie fallen mitten in ihr Lager, rings um ihre Wohnung her.
Aliwafanya washuke ndani ya kambi yao, kuzunguka mahema yao yote.
29 Da aßen sie und wurden allzu satt; was sie gewünscht hatten, gewährte er ihnen.
Walikula na kusaza, kwa maana alikuwa amewapa kile walichotamani.
30 Sie hatten sich ihres Gelüstes noch nicht entschlagen, und ihre Speise war noch in ihrem Munde,
Kabla hawajamaliza kula walichokitamani, hata kilipokuwa kingali bado vinywani mwao,
31 als der Zorn Gottes sich wider sie erhob und die Fetten unter ihnen erwürgte und die Jungmannschaft Israels darniederstürzte.
hasira ya Mungu ikawaka juu yao, akawaua wale waliokuwa na nguvu zaidi miongoni mwao, akiwaangusha vijana wa Israeli.
32 Trotz alledem sündigten sie weiter und glaubten nicht an seine Wunder.
Licha ya haya yote, waliendelea kutenda dhambi, licha ya maajabu yake, hawakuamini.
33 Darum ließ er ihre Tage wie einen Hauch vergehen und ihre Jahre durch plötzlichen Untergang.
Kwa hiyo akamaliza siku zao katika ubatili na miaka yao katika vitisho.
34 Wenn er sie tötete, so suchten sie ihn und kehrten sich wieder zu Gott
Kila mara Mungu alipowaua baadhi yao, waliosalia walimtafuta, walimgeukia tena kwa shauku.
35 und dachten daran, daß Gott ihr Fels sei, und Gott, der Höchste, ihr Erlöser.
Walikumbuka kwamba Mungu alikuwa Mwamba wao, kwamba Mungu Aliye Juu Sana alikuwa Mkombozi wao.
36 Aber sie heuchelten ihm mit ihrem Munde und logen mit ihren Zungen;
Lakini walimdanganya kwa vinywa vyao, wakisema uongo kwa ndimi zao,
37 denn ihr Herz war nicht aufrichtig gegen ihn, und sie hielten nicht treu an seinem Bund.
mioyo yao haikuwa thabiti kwake, wala hawakuwa waaminifu katika agano lake.
38 Er aber war barmherzig und vergab die Schuld und vertilgte sie nicht und hat oftmals seinen Zorn abgewandt und nicht allen seinen Grimm erweckt;
Hata hivyo alikuwa na huruma, alisamehe maovu yao na hakuwaangamiza. Mara kwa mara alizuia hasira yake, wala hakuchochea ghadhabu yake yote.
39 denn er dachte daran, daß sie Fleisch seien, ein Wind, der hinfährt und nicht wiederkehrt.
Alikumbuka kwamba wao walikuwa nyama tu, upepo upitao ambao haurudi.
40 Wie oft empörten sie sich wider ihn in der Wüste und betrübten ihn in der Einöde!
Mara ngapi walimwasi jangwani na kumhuzunisha nyikani!
41 Und sie versuchten Gott immer wieder und kränkten den Heiligen Israels.
Walimjaribu Mungu mara kwa mara, wakamkasirisha yeye Aliye Mtakatifu wa Israeli.
42 Sie sind seiner Hand nicht eingedenk gewesen, des Tages, da er sie vom Feinde erlöste;
Hawakukumbuka uwezo wake, siku aliyowakomboa kutoka kwa mtesi,
43 da er seine Zeichen tat in Ägypten und seine Wunder im Gefilde Zoan;
siku aliyoonyesha ishara zake za ajabu huko Misri, maajabu yake huko Soani.
44 als er ihre Ströme in Blut verwandelte und ihre Bäche, so daß man nicht trinken konnte;
Aligeuza mito yao kuwa damu, hawakuweza kunywa maji kutoka vijito vyao.
45 da er Ungeziefer unter sie sandte, das sie fraß, und Frösche, die sie verderbten;
Aliwapelekea makundi ya mainzi yakawala, na vyura wakawaharibu.
46 da er den Fressern ihre Früchte gab und den Heuschrecken ihre Erzeugnisse;
Aliruhusu tunutu kuharibu mimea yao, mazao yao kwa nzige.
47 da er ihre Weinstöcke mit Hagel schlug und ihre Maulbeerbäume mit Schlossen
Aliharibu mizabibu yao kwa mvua ya mawe na mikuyu yao kwa mvua iliyochangamana na theluji.
48 und ihr Vieh dem Hagel preisgab und ihre Herden den Wetterstrahlen;
Aliwaachia mifugo yao mvua ya mawe, akayapiga makundi ya wanyama wao kwa radi.
49 da er gegen sie die Glut seines Zornes entsandte, Grimm und Ungnade und Drangsal, Scharen von Unglücksengeln;
Aliwafungulia hasira yake kali, ghadhabu yake, hasira na uadui, na kundi la malaika wa kuharibu.
50 da er seinem Zorn den Lauf ließ, ihre Seele nicht vor dem Tod bewahrte, sondern ihr Leben der Pest preisgab;
Aliitengenezea njia hasira yake, hakuwaepusha na kifo, bali aliwaachia tauni.
51 da er alle Erstgeburt in Ägypten schlug, die Erstlinge ihrer Kraft in den Hütten Hams.
Aliwapiga wazaliwa wote wa kwanza wa Misri, matunda ya kwanza ya ujana katika mahema ya Hamu.
52 Und er ließ sein Volk ausziehen wie Schafe und leitete sie wie eine Herde in der Wüste
Lakini aliwatoa watu wake kama kundi, akawaongoza kama kondoo kupitia jangwani.
53 und führte sie sicher, daß sie sich nicht fürchteten; ihre Feinde aber bedeckte das Meer.
Aliwaongoza salama, wala hawakuogopa, bali bahari iliwameza adui zao.
54 Und er brachte sie in die Grenzen seines Heiligtums; zu diesem Berg, den seine Rechte erworben.
Hivyo akawaleta hadi kwenye mpaka wa nchi yake takatifu, hadi nchi ya vilima ambayo mkono wake wa kuume ulikuwa umeitwaa.
55 Und er vertrieb vor ihnen her die Heiden und teilte ihnen das Erbe aus mit der Meßschnur und ließ in ihren Zelten die Stämme Israels wohnen.
Aliyafukuza mataifa mbele yao, na kuwagawia nchi zao kama urithi, aliwakalisha makabila ya Israeli katika makao yao.
56 Aber sie versuchten und erzürnten den höchsten Gott und hielten seine Zeugnisse nicht,
Lakini wao walimjaribu Mungu, na kuasi dhidi ya Yeye Aliye Juu Sana, wala hawakuzishika sheria zake.
57 sondern wichen zurück und fielen ab wie ihre Väter; sie gingen fehl wie ein trügerischer Bogen.
Kama baba zao, hawakuwa thabiti wala waaminifu, wakawa wasioweza kutegemewa kama upinde wenye kasoro.
58 Und sie reizten ihn zum Zorn durch ihre Höhen und zur Eifersucht durch ihre Götzen.
Wakamkasirisha Mungu kwa mahali pao pa juu pa kuabudia miungu, wakachochea wivu wake kwa sanamu zao.
59 Gott hörte es und entrüstete sich und verabscheute Israel sehr.
Wakati Mungu alipowasikia, alikasirika sana, akamkataa Israeli kabisa.
60 Und er verließ seine Wohnung zu Silo, das Zelt, wo er unter den Menschen wohnte,
Akaiacha hema ya Shilo, hema aliyokuwa ameiweka katikati ya wanadamu.
61 und gab seine Macht in Gefangenschaft und seine Herrlichkeit in Feindeshand,
Akalipeleka Sanduku la nguvu zake utumwani, utukufu wake mikononi mwa adui.
62 und überlieferte sein Volk dem Schwert und war entrüstet über sein Erbe.
Aliachia watu wake wauawe kwa upanga, akaukasirikia sana urithi wake.
63 Seine Jünglinge hat das Feuer verzehrt, und seine Jungfrauen mußten ohne Brautlied bleiben.
Moto uliwaangamiza vijana wao, na wanawali wao hawakuimbiwa nyimbo za arusi,
64 Seine Priester sind durchs Schwert gefallen, und seine Witwen konnten nicht weinen.
makuhani wao waliuawa kwa upanga, wala wajane wao hawakuweza kulia.
65 Da erwachte der Herr wie ein Schlafender, wie ein Starker, der sich Mut zugetrunken.
Ndipo Bwana alipoamka kama vile kuamka usingizini, kama vile mtu aamkavyo kutoka kwenye bumbuazi la mvinyo.
66 Und er schlug seine Feinde zurück, ewige Schande fügte er ihnen zu.
Aliwapiga na kuwashinda adui zake, akawatia katika aibu ya milele.
67 Und er verwarf das Zelt Josephs und erwählte nicht den Stamm Ephraim,
Ndipo alipozikataa hema za Yosefu, hakulichagua kabila la Efraimu,
68 sondern erwählte den Stamm Juda, den Berg Zion, welchen er liebt.
lakini alilichagua kabila la Yuda, Mlima Sayuni, ambao aliupenda.
69 Und er baute sein Heiligtum wie Himmelshöhen, gleich der Erde, die er auf ewig gegründet hat.
Alijenga patakatifu pake kama vilele, kama dunia ambayo aliimarisha milele.
70 Und er erwählte seinen Knecht David und nahm ihn von den Schafhürden weg.
Akamchagua Daudi mtumishi wake na kumtoa kwenye mazizi ya kondoo.
71 Da er den tragenden Schafen nachging, holte er ihn, daß er weiden sollte Jakob, sein Volk, und Israel, sein Erbe.
Kutoka kuchunga kondoo alimleta kuwa mchungaji wa watu wake Yakobo, wa Israeli urithi wake.
72 Und er weidete sie mit aller Treue seines Herzens und leitete sie mit geschickter Hand.
Naye Daudi aliwachunga kwa uadilifu wa moyo, kwa mikono ya ustadi aliwaongoza.