< Psalm 73 >

1 Ein Psalm Asaphs. Nur gut ist Gott gegen Israel, gegen die, welche reinen Herzens sind.
Zaburi ya Asafu. Hakika Mungu ni mwema kwa Israeli, kwa wale ambao mioyo yao ni safi.
2 Ich aber hätte schier gestrauchelt mit meinen Füßen, wie leicht hätte ich einen Mißtritt getan!
Bali kwangu mimi, miguu yangu ilikuwa karibu kuteleza; nilikuwa karibu mguu wangu kuachia uliposimama.
3 Denn ich beneidete die Übermütigen, als ich den Frieden der Gottlosen sah.
Kwa maana niliwaonea wivu wenye kujivuna nilipoona kufanikiwa kwa waovu.
4 Denn sie leiden keine Qual bis zu ihrem Tod, und ihr Leib ist wohlgenährt.
Wao hawana taabu, miili yao ina afya na nguvu.
5 Sie werden nicht bemüht wie andere Leute und nicht geschlagen wie andere Menschen.
Hawapati shida zinazowataabisha watu wengine, wala hawapati mapigo kama wanadamu wengine.
6 Darum schmücken sie sich stolz und kleiden sich frech.
Kwa hiyo kiburi ni mkufu wao, wamejivika jeuri.
7 Ihr Gesicht strotzt von Fett, sie bilden sich sehr viel ein.
Uovu hutoka katika mioyo yao iliyokufa ganzi, majivuno maovu kutoka mioyoni mwao hauna kikomo.
8 Sie reden höhnisch und boshaft, drohen mit höherer Gewalt.
Hudhihaki na kusema kwa ukorofi, katika majivuno yao wanatishia kutesa.
9 Sie reden, als käme es vom Himmel; ihre Worte haben Geltung auf Erden.
Vinywa vyao huweka madai hata kwa mbingu, nazo ndimi zao humiliki duniani.
10 Darum wendet sich auch das Volk ihnen zu, und es wird von ihnen viel Wasser aufgesogen.
Kwa hiyo watu wao huwageukia na kunywa maji tele.
11 Und sie sagen: «Was merkt Gott? Weiß der Höchste überhaupt etwas?»
Wanasema, “Mungu awezaje kujua? Je, Yeye Aliye Juu Sana anayo maarifa?”
12 Siehe, das sind die Gottlosen; denen geht es immer gut, und sie werden reich!
Hivi ndivyo walivyo waovu: siku zote hawajali, wanaongezeka katika utajiri.
13 Ganz umsonst habe ich mein Herz rein erhalten und meine Hände in Unschuld gewaschen;
Hakika nimeuweka moyo wangu safi bure, ni bure nimenawa mikono yangu nisiwe na hatia.
14 denn ich bin doch täglich geschlagen worden, und meine Strafe ist alle Morgen da!
Mchana kutwa nimetaabika, nimeadhibiwa kila asubuhi.
15 Wollte ich auch so rechnen, siehe, so würde ich das Geschlecht deiner Kinder verraten.
Kama ningesema, “Nitasema hivi,” ningelikuwa nimewasaliti watoto wako.
16 So sann ich denn nach, um dies zu verstehen; aber es schien mir vergebliche Mühe zu sein,
Nilipojaribu kuelewa haya yote, yalikuwa magumu kwangu kuelewa.
17 bis ich in das Heiligtum Gottes ging und auf ihr Ende merkte.
Mpaka nilipoingia patakatifu pa Mungu, ndipo nilipotambua mwisho wao.
18 Nur auf schlüpfrigen Boden setzest du sie; du lässest sie fallen, daß sie in Trümmer sinken.
Hakika unawaweka mahali pa utelezi, unawaangusha chini kwa uharibifu.
19 Wie geschah das so plötzlich und entsetzlich! Sie gingen unter und nahmen ein Ende mit Schrecken.
Tazama jinsi wanavyoangamizwa ghafula, wanatoweshwa kabisa na vitisho!
20 Wie einen Traum nach dem Erwachen, so wirst du, o Herr, wenn du dich aufmachst, ihr Bild verächtlich machen.
Kama ndoto mtu aamkapo, hivyo wakati uinukapo, Ee Bwana, utawatowesha kama ndoto.
21 Als mein Herz verbittert war und es mir in den Nieren wehe tat,
Wakati moyo wangu ulipohuzunishwa, na roho yangu ilipotiwa uchungu,
22 da war ich dumm und verstand nichts; ich benahm mich wie ein Vieh gegen dich.
nilikuwa mpumbavu na mjinga, nilikuwa mnyama mkatili mbele yako.
23 Und doch bleibe ich stets bei dir; du hältst mich bei meiner rechten Hand.
Hata hivyo niko pamoja nawe siku zote, umenishika mkono wangu wa kuume.
24 Leite mich auch ferner nach deinem Rat und nimm mich hernach mit Ehren auf!
Unaniongoza kwa shauri lako, hatimaye utaniingiza katika utukufu.
25 Wen habe ich im Himmel? Und dir ziehe ich gar nichts auf Erden vor!
Nani niliye naye mbinguni ila wewe? Dunia haina chochote ninachokitamani ila wewe.
26 Schwinden auch mein Fleisch und mein Herz dahin, so bleibt doch Gott ewiglich meines Herzens Fels und mein Teil.
Mwili na moyo wangu vyaweza kushindwa, bali Mungu ni nguvu ya moyo wangu na fungu langu milele.
27 Denn siehe, die fern von dir sind, kommen um; du vertilgst alle, die dir untreu werden.
Wale walio mbali nawe wataangamia, unawaangamiza wote wasio waaminifu kwako.
28 Mir aber ist die Nähe Gottes köstlich; ich habe Gott, den HERRN, zu meiner Zuflucht gemacht, um zu erzählen alle deine Werke.
Lakini kwangu mimi, ni vyema kuwa karibu na Mungu. Nimemfanya Bwana Mwenyezi kimbilio langu; nami nitayasimulia matendo yako yote.

< Psalm 73 >