< Psalm 48 >

1 Ein Lied; ein Psalm. Von den Kindern Korahs. Groß ist der HERR und hoch gelobt in der Stadt unsres Gottes, auf seinem heiligen Berge.
Yahwe ndiye aliye mkuu na mwenyekusifiwa sana, katika mji wa Mungu wetu kwenye mlima wake mtakatifu.
2 Schön erhebt sich der Berg Zion, die Freude des ganzen Landes; auf der Seite gegen Mitternacht ist die Stadt des großen Königs.
Ni mzuri katika mwinuko wake, furaha ya nchi yote, ni mlima Sayuni, kwenye upande wa kaskazini, mji wa Mfalme mkuu.
3 Gott ist in ihren Palästen bekannt als eine feste Burg.
Mungu amejifunua mwenyewe katika jumba lake la kifahari kama kimbilio la usalama.
4 Denn siehe, Könige haben sich verbündet und sind miteinander vorübergezogen.
Maana, tazama, wafalme walikusanyika wenyewe; wote pamoja walipita.
5 Sie haben sich verwundert, als sie solches sahen; sie erschraken und flohen davon.
Nao waliuona, wakashangaa; walifadhaika, na wakaharakisha kuondoka.
6 Zittern ergriff sie daselbst, Angst wie eine Gebärende.
Pale pale tetemeko liliwashikilia, maumivu makali kama mwanamke anaye zaa.
7 Durch den Ostwind zerbrichst du Tarsisschiffe.
Kwa upepo wa mashariki wewe huivunja meli ya Tarshishi.
8 Wie wir's gehört, so haben wir's gesehen in der Stadt des HERRN der Heerscharen, in der Stadt unsres Gottes. Gott wird sie erhalten bis in Ewigkeit. (Pause)
Kama tulivyo sikia, vivyo hivyo tumeona katika mji wa Yahwe wa majeshi, katika mji wa Mungu wetu; Mungu atautunza milele. (Selah)
9 Wir gedenken, o Gott, deiner Gnade inmitten deines Tempels.
Tumeutafakari uaminifu wa agano lako, Mungu, katikati ya hekalu lako.
10 O Gott, wie dein Name, also reicht auch dein Ruhm bis an die Enden der Erde; deine Rechte ist voller Gerechtigkeit.
Kama lilivyo jina lako, Mungu, hivyo ndivyo zilivyo sifa zako mpaka miisho ya dunia; mkono wako wa kuume umejaa haki.
11 Der Berg Zion freut sich, die Töchter Judas frohlocken um deiner Gerichte willen.
Milma Sayuni na ufurahi, nao wana wa Yuda washangilie kwa sababu ya amri ya haki yako.
12 Geht rings um Zion, umwandelt sie, zählt ihre Türme!
Tembeeni katika Mlima Sayuni, muuzungukie mji,
13 Beachtet ihre Bollwerke, durchgehet ihre Paläste, auf daß ihr es den Nachkommen erzählet,
mzitazame kwa makini nguzo zake, na mtazame majumba yake ya kifahari ili kwamba muweze kuwasimulia kizazi kijacho.
14 daß dieser Gott unser Gott ist immer und ewig; er führt uns über den Tod hinweg!
Kwa kuwa huyu Mungu ni Mungu wetu milele na milele; naye atakuwa kiongozi wetu mpaka kufa.

< Psalm 48 >