< Psalm 48 >

1 Ein Lied; ein Psalm. Von den Kindern Korahs. Groß ist der HERR und hoch gelobt in der Stadt unsres Gottes, auf seinem heiligen Berge.
Wimbo. Zaburi ya wana wa Kora. Bwana ni mkuu, anayestahili kusifiwa sana, katika mji wa Mungu wetu, mlima wake mtakatifu.
2 Schön erhebt sich der Berg Zion, die Freude des ganzen Landes; auf der Seite gegen Mitternacht ist die Stadt des großen Königs.
Ni mzuri katika kuinuka kwake juu sana, furaha ya dunia yote. Kama vilele vya juu sana vya Safoni ni Mlima Sayuni, mji wa Mfalme Mkuu.
3 Gott ist in ihren Palästen bekannt als eine feste Burg.
Mungu yuko katika ngome zake; amejionyesha mwenyewe kuwa ngome yake.
4 Denn siehe, Könige haben sich verbündet und sind miteinander vorübergezogen.
Wakati wafalme walipounganisha nguvu, waliposonga mbele pamoja,
5 Sie haben sich verwundert, als sie solches sahen; sie erschraken und flohen davon.
walimwona nao wakashangaa, wakakimbia kwa hofu.
6 Zittern ergriff sie daselbst, Angst wie eine Gebärende.
Kutetemeka kuliwashika huko, maumivu kama ya mwanamke mwenye utungu wa kuzaa.
7 Durch den Ostwind zerbrichst du Tarsisschiffe.
Uliwaangamiza kama meli za Tarshishi zilizovunjwa na upepo wa mashariki.
8 Wie wir's gehört, so haben wir's gesehen in der Stadt des HERRN der Heerscharen, in der Stadt unsres Gottes. Gott wird sie erhalten bis in Ewigkeit. (Pause)
Kama tulivyokuwa tumesikia, ndivyo tulivyoona katika mji wa Bwana Mwenye Nguvu Zote, katika mji wa Mungu wetu: Mungu ataufanya uwe salama milele.
9 Wir gedenken, o Gott, deiner Gnade inmitten deines Tempels.
Ee Mungu, hekaluni mwako tunatafakari upendo wako usiokoma.
10 O Gott, wie dein Name, also reicht auch dein Ruhm bis an die Enden der Erde; deine Rechte ist voller Gerechtigkeit.
Ee Mungu, kama jina lako lilivyo, sifa zako zinafika hadi miisho ya dunia, mkono wako wa kuume umejazwa na haki.
11 Der Berg Zion freut sich, die Töchter Judas frohlocken um deiner Gerichte willen.
Mlima Sayuni unashangilia, vijiji vya Yuda vinafurahi kwa sababu ya hukumu zako.
12 Geht rings um Zion, umwandelt sie, zählt ihre Türme!
Tembeeni katika Sayuni, uzungukeni mji, hesabuni minara yake;
13 Beachtet ihre Bollwerke, durchgehet ihre Paläste, auf daß ihr es den Nachkommen erzählet,
yatafakarini vyema maboma yake, angalieni ngome zake, ili mpate kusimulia habari zake kwa kizazi kijacho.
14 daß dieser Gott unser Gott ist immer und ewig; er führt uns über den Tod hinweg!
Kwa kuwa huyu Mungu ni Mungu wetu milele na milele; atakuwa kiongozi wetu hata mwisho.

< Psalm 48 >