< Psalm 34 >

1 Von David. Als er seine Gebärde verstellte vor Abimelech und dieser ihn von sich trieb und er hinwegging. Ich will den HERRN allezeit preisen, sein Lob soll immerdar in meinem Munde sein.
Zaburi ya Daudi, alipojifanya mwendawazimu mbele ya Abimeleki, ambaye alimfukuza, naye akaondoka. Nitamtukuza Bwana nyakati zote, sifa zake zitakuwa midomoni mwangu siku zote.
2 Meine Seele rühme sich des HERRN; die Elenden sollen es hören und sich freuen.
Nafsi yangu itajisifu katika Bwana, walioonewa watasikia na wafurahi.
3 Preiset mit mir den HERRN, und lasset uns miteinander seinen Namen erhöhen!
Mtukuzeni Bwana pamoja nami, naam, na tulitukuze jina lake pamoja.
4 Da ich den HERRN suchte, antwortete er mir und errettete mich aus aller meiner Furcht.
Nilimtafuta Bwana naye akanijibu, akaniokoa kwenye hofu zangu zote.
5 Die auf ihn blicken, werden strahlen, und ihr Angesicht wird nicht erröten.
Wale wamtazamao hutiwa nuru, nyuso zao hazifunikwi na aibu kamwe.
6 Da dieser Elende rief, hörte der HERR und half ihm aus allen seinen Nöten.
Maskini huyu alimwita Bwana, naye akamsikia, akamwokoa katika taabu zake zote.
7 Der Engel des HERRN lagert sich um die her, so ihn fürchten, und errettet sie.
Malaika wa Bwana hufanya kituo akiwazunguka wale wamchao, naye huwaokoa.
8 Schmecket und sehet, wie freundlich der HERR ist; wohl dem, der auf ihn traut!
Onjeni mwone kwamba Bwana ni mwema, heri mtu yule anayemkimbilia.
9 Fürchtet den HERRN, ihr seine Heiligen; denn die ihn fürchten, haben keinen Mangel.
Mcheni Bwana enyi watakatifu wake, kwa maana wale wamchao hawapungukiwi na chochote.
10 Junge Löwen leiden Not und Hunger; aber die den HERRN suchen, müssen nichts Gutes entbehren.
Wana simba wenye nguvu hutindikiwa na kuona njaa, bali wale wamtafutao Bwana hawatakosa kitu chochote kilicho chema.
11 Kommt her, ihr Kinder, hört mir zu; ich will euch die Furcht des HERRN lehren!
Njooni, watoto wangu, mnisikilize, nitawafundisha kumcha Bwana.
12 Wer hat Lust zum Leben und möchte gern gute Tage sehen?
Yeyote kati yenu anayependa uzima na kutamani kuziona siku nyingi njema,
13 Behüte deine Zunge vor Bösem und deine Lippen, daß sie nicht trügen;
basi auzuie ulimi wake na mabaya, na midomo yake kutokana na kusema uongo.
14 weiche vom Bösen und tue Gutes, suche Frieden und jage ihm nach!
Aache uovu, atende mema, aitafute amani na kuifuatilia.
15 Die Augen des HERRN achten auf die Gerechten und seine Ohren auf ihr Schreien;
Macho ya Bwana huwaelekea wenye haki, na masikio yake yako makini kusikiliza kilio chao.
16 das Antlitz des HERRN steht wider die, so Böses tun, daß er ihr Gedächtnis von der Erde vertilge.
Uso wa Bwana uko kinyume na watendao maovu, ili kufuta kumbukumbu lao duniani.
17 Als jene schrieen, hörte der HERR und rettete sie aus aller ihrer Not.
Wenye haki hulia, naye Bwana huwasikia, huwaokoa katika taabu zao zote.
18 Der HERR ist nahe denen, die zerbrochenen Herzens sind, und hilft denen, deren Geist zerschlagen ist.
Bwana yu karibu na waliovunjika moyo, na huwaokoa waliopondeka roho.
19 Der Gerechte muß viel leiden; aber der HERR rettet ihn aus dem allem.
Mwenye haki ana mateso mengi, lakini Bwana humwokoa nayo yote,
20 Er bewahrt ihm alle seine Gebeine, daß nicht eines derselben zerbrochen wird.
huhifadhi mifupa yake yote, hata mmoja hautavunjika.
21 Den Gottlosen wird die Bosheit töten, und die den Gerechten hassen, müssen es büßen.
Ubaya utamuua mtu mwovu, nao adui za mwenye haki watahukumiwa.
22 Der HERR erlöst die Seele seiner Knechte, und alle, die auf ihn vertrauen, werden es nicht zu büßen haben.
Bwana huwakomboa watumishi wake, yeyote anayemkimbilia yeye hatahukumiwa kamwe.

< Psalm 34 >