< Psalm 23 >

1 Ein Psalm Davids. Der HERR ist mein Hirte; mir wird nichts mangeln.
Yahwe ni mchungaji wangu; sita pungukiwa na kitu.
2 Er weidet mich auf grünen Auen und führt mich zu stillen Wassern.
Yeye hunilaza katika majani mabichi; huniongoza kando ya maji matulivu.
3 Er erquickt meine Seele, er führt mich auf rechter Straße um seines Namens willen.
Yeye huurejesha uhai wangu; huniongoza katika njia iliyo sahihi kwa ajili ya jina lake.
4 Und ob ich schon wanderte im finstern Todestal, fürchte ich kein Unglück; denn du bist bei mir, dein Stecken und dein Stab, die trösten mich!
Hata ijapokuwa nikipita katika bonde la uvuli na giza nene, sitaogopa kudhurika kwa kuwa wewe uko pamoja nami; fimbo yako na gongo lako vya nifariji.
5 Du bereitest vor mir einen Tisch angesichts meiner Feinde; du hast mein Haupt mit Öl gesalbt, mein Becher fließt über.
Wewe waandaa meza mbele yangu katika uwepo wa maadui zangu; umenipaka mafuta kichwa changu na kikombe changu kinafurika.
6 Nur Güte und Gnade werden mir folgen mein Leben lang, und ich werde bleiben im Hause des HERRN immerdar.
Hakika wema na uaminifu wa agano vitaniandama siku zote za maisha yangu; nami nitaishi katika nyumba ya Yahwe milele!

< Psalm 23 >