< Psalm 2 >
1 Warum toben die Heiden und reden die Völker vergeblich?
Kwa nini mataifa wanashauriana kufanya mabaya, na kabila za watu kula njama bure?
2 Die Könige der Erde stehen zusammen, und die Fürsten verabreden sich wider den HERRN und wider seinen Gesalbten:
Wafalme wa dunia wanajipanga na watawala wanajikusanya pamoja dhidi ya Bwana na dhidi ya Mpakwa Mafuta wake.
3 «Wir wollen ihre Bande zerreißen und ihre Fesseln von uns werfen!»
Wanasema, “Tuvunje minyororo yao na kuvitupilia mbali vifungo vyao.”
4 Der im Himmel thront, lacht, der HERR spottet ihrer.
Yeye atawalaye mbinguni hucheka, Bwana huwadharau.
5 Dann wird er zu ihnen reden in seinem Zorn und sie schrecken mit seinem Grimm:
Kisha huwakemea katika hasira yake na kuwaogopesha katika ghadhabu yake, akisema,
6 «Ich habe meinen König eingesetzt auf Zion, meinem heiligen Berge!»
“Nimemtawaza Mfalme wangu juu ya Sayuni, mlima wangu mtakatifu.”
7 Ich will erzählen vom Ratschluß des HERRN; er hat zu mir gesagt: «Du bist mein Sohn, heute habe ich dich gezeugt
Nitatangaza amri ya Bwana: Yeye aliniambia, “Wewe ni Mwanangu, leo mimi nimekuzaa.
8 Heische von mir, so will ich dir die Nationen zum Erbe geben und die Enden der Erde zu deinem Eigentum.
Niombe, nami nitayafanya mataifa kuwa urithi wako, miisho ya dunia kuwa milki yako.
9 Du sollst sie mit eisernem Zepter zerschmettern, wie Töpfergeschirr sie zerschmeißen!»
Utawatawala kwa fimbo ya chuma na kuwavunjavunja kama chombo cha mfinyanzi.”
10 So nehmet nun Verstand an, ihr Könige, und lasset euch warnen, ihr Richter der Erde!
Kwa hiyo, ninyi wafalme, kuweni na hekima; mwonyeke, enyi watawala wa dunia.
11 Dienet dem HERRN mit Furcht und frohlocket mit Zittern.
Mtumikieni Bwana kwa hofu na mshangilie kwa kutetemeka.
12 Küsset den Sohn, daß er nicht zürne und ihr nicht umkommet auf dem Wege; denn wie leicht kann sein Zorn entbrennen! Wohl allen, die sich bergen bei ihm!
Mbusu Mwana, asije akakasirika nawe ukaangamizwa katika njia yako, kwa maana hasira yake inaweza kuwaka ghafula. Heri wote wanaomkimbilia.