< Psalm 148 >
1 Hallelujah! Lobet den HERRN vom Himmel her, lobet ihn in der Höhe!
Msifuni Yahwe. Msifuni Yahwe, ninyi mlio katika mbingu; msifuni yeye, ninyi mlio juu.
2 Lobet ihn, alle seine Engel; lobet ihn, alle seine Heerscharen!
Msifuni yeye, enyi malaika wake wote; msifuni yeye, majeshi ya malaika wake wote.
3 Lobet ihn, Sonne und Mond; lobet ihn, alle leuchtenden Sterne!
Msifuni yeye, enyi jua na mwezi; msifuni yeye, nyota zote zing'aazo.
4 Lobet ihn, ihr Himmelshöhen und ihr Wasser oben am Himmel!
Msifuni yeye, enyi mbingu zilizo juu zaidi na maji yaliyo juu ya anga.
5 Sie sollen loben den Namen des HERRN; denn sie entstanden auf sein Geheiß,
Na vilisifu jina la Yahwe, maana aliamuru, navyo vikaumbwa.
6 und er verlieh ihnen ewigen Bestand; er gab ein Gesetz, das nicht überschritten wird.
Pia ameviimrisha milele na milele; naye alitoa amri ambayo haitabadilika.
7 Lobet den HERRN von der Erde her, ihr Walfische und alle Meeresfluten!
Msifuni yeye kutoka nchi, ninyi viumbe wa baharini na viumbe vyote katika kina cha bahari,
8 Feuer und Hagel, Schnee und Dunst, Sturmwind, der sein Wort ausführt;
moto na mvua ya mawe, theluji na mawingu, upepo wa dhoruba ukitimiza neno lake.
9 Berge und alle Hügel, Obstbäume und alle Zedern;
Msifuni yeye, enyi milima na vilima, miti ya matunda na mierezi yote,
10 wilde Tiere und alles Vieh, alles, was kriecht und fliegt;
wanyama pori na wanyama wafugwao, viumbe vitambaavyo na ndege.
11 die Könige der Erde und alle Nationen, die Fürsten und alle Richter auf Erden;
Msifuni Yahwe, wafalme wa nchi na mataifa yote, wakuu na watawala wote wa nchi,
12 Jünglinge und auch Jungfrauen, Greise mitsamt den Knaben;
wote vijana wa kiume na vijana wa kike, wazee na watoto.
13 sie sollen loben den Namen des HERRN! Denn sein Name allein ist erhaben, sein Glanz überstrahlt Erde und Himmel.
Na walisifu jina la Yahwe, kwa kuwa jina lake pekee limetukuka na utukufu wake umeongezwa juu ya nchi na mbingu.
14 Und er hat das Horn seines Volkes erhöht, allen seinen Frommen zum Ruhm, den Kindern Israel, dem Volk, das ihm nahe ist. Hallelujah!
Naye ameyainua mapembe ya watu wake kwa ajili ya sifa kutoka kwa waaminifu wake wote, Waisraeli, watu wa karibu naye. Msifuni Yahwe.