< Psalm 132 >

1 Ein Wallfahrtslied. Gedenke, o HERR, dem David alle seine Mühen,
Wimbo wa kwenda juu. Ee Bwana, mkumbuke Daudi na taabu zote alizozistahimili.
2 daß er dem HERRN schwur und dem Mächtigen Jakobs gelobte:
Aliapa kiapo kwa Bwana na akaweka nadhiri kwa Yule Mwenye Nguvu wa Yakobo:
3 Ich will nicht in das Zelt meines Hauses gehen, noch auf das Lager meines Bettes steigen,
“Sitaingia nyumbani mwangu au kwenda kitandani mwangu:
4 ich will meinen Augen keinen Schlaf und meinen Augenlidern keinen Schlummer gönnen,
sitaruhusu usingizi katika macho yangu, wala kope zangu kusinzia,
5 bis ich eine Stätte gefunden habe für den HERRN, eine Wohnung für den Mächtigen Jakobs!
mpaka nitakapompatia Bwana mahali, makao kwa ajili ya Yule Mwenye Nguvu wa Yakobo.”
6 Siehe, wir hörten, sie sei zu Ephrata; wir haben sie gefunden im Gefilde von Jear!
Tulisikia habari hii huko Efrathi, tulikutana nayo katika mashamba ya Yaara:
7 Wir wollen kommen zu seiner Wohnung, wir wollen anbeten beim Schemel seiner Füße!
“Twendeni kwenye makao yake, na tuabudu kwenye kiti cha kuwekea miguu yake;
8 HERR, mache dich auf zu deiner Ruhestatt, du und die Lade deiner Macht!
inuka, Ee Bwana, uje mahali pako pa kupumzikia, wewe na Sanduku la nguvu zako.
9 Deine Priester sollen sich in Gerechtigkeit kleiden, und deine Frommen sollen jubeln.
Makuhani wako na wavikwe haki, watakatifu wako na waimbe kwa furaha.”
10 Um Davids, deines Knechtes willen weise nicht ab das Angesicht deines Gesalbten!
Kwa ajili ya Daudi mtumishi wako, usimkatae mpakwa mafuta wako.
11 Der HERR hat David in Wahrheit geschworen, davon wird er nicht abgehen: «Von der Frucht deines Leibes will ich setzen auf deinen Thron!
Bwana alimwapia Daudi kiapo, kiapo cha uhakika ambacho hatakitangua: “Nitamweka mmoja wa wazao wako mwenyewe katika kiti chako cha enzi,
12 Werden deine Söhne meinen Bund bewahren und meine Zeugnisse, die ich sie lehren will, so sollen auch ihre Söhne für immer sitzen auf deinem Thron!»
kama wanao watashika Agano langu na sheria ninazowafundisha, ndipo wana wao watarithi kiti chako cha enzi milele na milele.”
13 Denn der HERR hat Zion erwählt und sie zu seiner Wohnung begehrt:
Kwa maana Bwana ameichagua Sayuni, amepaonea shauku pawe maskani yake:
14 «Dies ist für immer meine Ruhestatt, hier will ich wohnen; denn so habe ich es begehrt.
“Hapa ni mahali pangu pa kupumzika milele na milele; hapa ndipo nitakapoketi nikitawala, kwa sababu nimepaonea shauku:
15 Ihre Nahrung will ich reichlich segnen, ihre Armen sättigen mit Brot.
Nitambariki kwa kumpa mahitaji tele: nitashibisha maskini wake kwa chakula.
16 Ihre Priester will ich mit Heil bekleiden, und ihre Frommen sollen jubeln.
Nitawavika makuhani wake wokovu, nao watakatifu wake watadumu wakiimba kwa furaha.
17 Dort will ich dem David ein Horn hervorsprossen lassen, eine Leuchte zurichten meinem Gesalbten.
“Hapa nitamchipushia Daudi pembe, na kuweka taa kwa ajili ya masiya wangu.
18 Seine Feinde will ich mit Schande bekleiden; aber auf ihm soll seine Krone glänzen!»
Adui zake nitawavika aibu, bali taji kichwani pake itangʼaa sana.”

< Psalm 132 >