< Psalm 107 >
1 «Danket dem Herrn, denn er ist gütig, denn seine Gnade währt ewig!»
Mshukuruni Bwana, kwa kuwa yeye ni mwema, upendo wake wadumu milele.
2 So sollen sagen die Erlösten des HERRN, die er aus der Hand des Feindes erlöst
Waliokombolewa wa Bwana na waseme hivi, wale aliowaokoa kutoka mkono wa adui,
3 und die er aus den Ländern zusammengebracht hat, vom Aufgang und vom Niedergang, von Mitternacht und vom Meer,
wale aliowakusanya kutoka nchi mbalimbali, kutoka mashariki na magharibi, kutoka kaskazini na kusini.
4 die irregingen in der Wüste, auf ungebahntem Weg und keine Stadt fanden, wo sie wohnen konnten,
Baadhi yao walitangatanga jangwani, hawakuona njia ya kuwafikisha mji ambao wangeweza kuishi.
5 hungrig und durstig, daß ihre Seele in ihnen verschmachtete.
Walikuwa na njaa na kiu, nafsi zao zikadhoofika.
6 Da schrieen sie zum HERRN in ihrer Not, und er rettete sie aus ihren Ängsten
Ndipo walipomlilia Bwana katika shida yao, naye akawaokoa kutoka taabu yao.
7 und führte sie auf den rechten Weg, daß sie zu einer bewohnten Stadt gelangten,
Akawaongoza kwa njia iliyo sawa hadi mji ambao wangeweza kuishi.
8 die sollen dem HERRN danken für seine Gnade und für seine Wunder an den Menschenkindern,
Basi na wamshukuru Bwana kwa upendo wake usiokoma, na kwa matendo yake ya ajabu kwa wanadamu,
9 daß er die durstige Seele getränkt und die hungernde Seele mit Gutem gesättigt hat!
kwa maana yeye humtosheleza mwenye kiu, na kumshibisha mwenye njaa kwa vitu vyema.
10 Die in Finsternis und Todesschatten saßen, gebunden in Elend und Eisen,
Wengine walikaa gizani na katika huzuni kuu, wafungwa wakiteseka katika minyororo,
11 weil sie den Geboten Gottes widerstrebt und den Rat des Höchsten verachtet hatten,
kwa sababu walikuwa wameasi dhidi ya maneno ya Mungu na kudharau shauri la Aliye Juu Sana.
12 so daß er ihr Herz durch Strafe beugte, daß sie dalagen und ihnen niemand half.
Aliwatumikisha kwa kazi ngumu; walijikwaa na hapakuwepo yeyote wa kuwasaidia.
13 Da schrieen sie zum HERRN in ihrer Not, und er rettete sie aus ihren Ängsten,
Ndipo walipomlilia Bwana katika shida yao, naye akawaokoa kutoka taabu yao.
14 und führte sie aus Finsternis und Todesschatten heraus und zerriß ihre Bande,
Akawatoa katika giza na huzuni kuu na akavunja minyororo yao.
15 die sollen dem HERRN danken für seine Gnade und für seine Wunder an den Menschenkindern,
Basi na wamshukuru Bwana kwa upendo wake usiokoma, na kwa matendo yake ya ajabu kwa wanadamu,
16 daß er eherne Türen zerbricht und eiserne Riegel zerschlägt!
kwa kuwa yeye huvunja malango ya shaba na kukata mapingo ya chuma.
17 Die Toren, die wegen ihrer Übertretung und um ihrer Missetaten willen geplagt wurden,
Wengine wakawa wapumbavu kutokana na uasi wao, wakapata mateso kwa sababu ya uovu wao.
18 daß ihrer Seele vor aller Nahrung ekelte und sie nahe waren den Pforten des Todes.
Wakachukia kabisa vyakula vyote, wakakaribia malango ya mauti.
19 Da schrieen sie zum HERRN in ihrer Not, und er rettete sie aus ihren Ängsten.
Ndipo walipomlilia Bwana katika shida yao, naye akawaokoa kutoka taabu yao.
20 Er sandte sein Wort und machte sie gesund und ließ sie ihren Gräbern entrinnen,
Akalituma neno lake na kuwaponya, akawaokoa kutoka maangamizo yao.
21 die sollen dem HERRN danken für seine Gnade und für seine Wunder an den Menschenkindern,
Basi na wamshukuru Bwana kwa upendo wake usiokoma, na kwa matendo yake ya ajabu kwa wanadamu.
22 sollen ihm Dankopfer bringen und seine Taten jubelnd erzählen!
Na watoe dhabihu za kushukuru, na wasimulie matendo yake kwa nyimbo za furaha.
23 Die in Schiffen sich aufs Meer begaben und Handel trieben auf großen Wassern,
Wengine walisafiri baharini kwa meli, walikuwa wafanyabiashara kwenye maji makuu.
24 die des HERRN Werke sahen und seine Wunder auf hoher See,
Waliziona kazi za Bwana, matendo yake ya ajabu kilindini.
25 wenn er sprach und einen Sturmwind erregte, der die Wellen in die Höhe warf,
Kwa maana alisema na kuamsha tufani iliyoinua mawimbi juu.
26 daß sie emporfuhren gen Himmel und hinabfuhren zur Tiefe und ihre Seele vor Angst verging;
Yakainuka juu mbinguni, yakashuka chini hadi vilindini, katika hatari hii ujasiri wao uliyeyuka.
27 daß sie wirbelten und schwankten wie Trunkene, und alle ihre Weisheit dahin war.
Walipepesuka na kuyumbayumba kama walevi, ujanja wao ukafikia ukomo.
28 Da schrieen sie zum HERRN in ihrer Not, und er führte sie heraus aus ihren Ängsten;
Ndipo walipomlilia Bwana katika shida yao, naye akawatoa kwenye taabu yao.
29 er stillte den Sturm, daß er schwieg und die Wellen sich beruhigten;
Akatuliza dhoruba kwa mnongʼono, mawimbi ya bahari yakatulia.
30 und jene wurden froh, daß sie sich legten; und er führte sie an das erwünschte Gestade,
Walifurahi ilipokuwa shwari, naye akawaongoza hadi bandari waliyoitamani.
31 die sollen dem HERRN danken für seine Gnade und für seine Wunder an den Menschenkindern
Basi na wamshukuru Bwana kwa upendo wake usiokoma, na kwa matendo yake ya ajabu kwa wanadamu.
32 und sollen ihn erheben in der Versammlung des Volkes und im Kreise der Ältesten ihn rühmen!
Na wamtukuze yeye katika kusanyiko la watu, na wamsifu katika baraza la wazee.
33 Er machte Ströme zur Wüste und ließ Wasserquellen vertrocknen;
Yeye aligeuza mito kuwa jangwa, chemchemi za maji zitiririkazo kuwa ardhi yenye kiu,
34 fruchtbares Land wurde zur Salzwüste wegen der Bosheit derer, die es bewohnten.
nchi izaayo ikawa ya chumvi isiyofaa, kwa sababu ya uovu wa wale walioishi humo.
35 Er machte aber auch die Wüste zum Wasserteich und dürres Land zu Wasserquellen.
Aligeuza jangwa likawa madimbwi ya maji, nayo ardhi kame kuwa chemchemi za maji zitiririkazo;
36 Und er ließ Hungrige daselbst wohnen, und sie gründeten eine bewohnte Stadt;
aliwaleta wenye njaa wakaishi humo, nao wakajenga mji wangeweza kuishi.
37 und sie säten Äcker an und pflanzten Weinberge und hatten von den Früchten einen schönen Ertrag;
Walilima mashamba na kupanda mizabibu, nayo ikazaa matunda mengi,
38 und er segnete sie, daß sie sich stark mehrten, und auch ihres Viehs machte er nicht wenig,
Mungu aliwabariki, hesabu yao ikaongezeka sana, wala hakuruhusu mifugo yao kupungua.
39 nachdem sie vermindert worden waren und gedemütigt durch den Druck des Unglücks und Kummers,
Kisha hesabu yao ilipungua, na walinyenyekeshwa kwa kuonewa, maafa na huzuni.
40 als er Verachtung auf die Fürsten goß und sie irregehen ließ in unwegsamer Wildnis;
Yeye ambaye huwamwagia dharau wakuu, aliwafanya watangetange nyikani isiyo na njia.
41 aber er erhob den Armen aus dem Elend und machte die Geschlechter wie Schafherden.
Lakini yeye aliwainua wahitaji katika taabu zao, na kuongeza jamaa zao kama makundi ya kondoo.
42 Die Redlichen sollen es sehen und sich freuen, und alle Bosheit soll ihr Maul verschließen!
Wanyofu wataona na kufurahi, lakini waovu wote watafunga vinywa vyao.
43 Wer weise ist, der beobachte solches und merke sich die Gnadenerweisungen des HERRN!
Yeyote aliye na hekima, ayasikie mambo haya, na atafakari upendo mkuu wa Bwana.