< Psalm 104 >
1 Lobe den HERRN, meine Seele! HERR, mein Gott, du bist sehr groß; mit Pracht und Majestät bist du angetan,
Ee nafsi yangu, umhimidi Bwana. Ee Bwana Mungu wangu, wewe ni mkuu sana, umejivika utukufu na enzi.
2 du, der in Licht sich hüllt wie in ein Gewand, der den Himmel ausspannt wie ein Zelt,
Amejifunika katika nuru kama vile kwa vazi, amezitandaza mbingu kama hema
3 der sich seinen Söller zimmert aus Wasser, Wolken zu seinem Wagen macht und auf den Fittichen des Windes einherfährt,
na kuziweka nguzo za orofa yake juu ya maji. Huyafanya mawingu kuwa gari lake, na hupanda kwenye mbawa za upepo.
4 der Winde zu seinen Boten macht, Feuerflammen zu seinen Dienern.
Huzifanya pepo kuwa wajumbe wake, miali ya moto watumishi wake.
5 Er hat die Erde auf ihre Grundfesten gestützt, daß sie nimmermehr wanken wird.
Ameiweka dunia kwenye misingi yake, haiwezi kamwe kuondoshwa.
6 Mit der Flut decktest du sie wie mit einem Kleid; die Wasser standen über den Bergen;
Uliifunika kwa kilindi kama kwa vazi, maji yalisimama juu ya milima.
7 aber vor deinem Schelten flohen sie, von deiner Donnerstimme wurden sie verscheucht.
Lakini kwa kukemea kwako maji yalikimbia, kwa sauti ya radi yako yakatoroka,
8 Berge stiegen empor, Täler senkten sich zu dem Ort, welchen du ihnen gesetzt hast.
yakapanda milima, yakateremka mabondeni, hadi mahali pale ulipoyakusudia.
9 Du hast den Wassern eine Grenze gesetzt, die sie nicht überschreiten sollen; sie dürfen die Erde nicht wiederum bedecken.
Uliyawekea mpaka ambao hayawezi kuuvuka, kamwe hayataifunika dunia tena.
10 Du lässest Quellen entspringen in den Tälern; sie fließen zwischen den Bergen hin;
Huzifanya chemchemi zimwage maji mabondeni, hutiririka kati ya milima.
11 sie tränken alle Tiere des Feldes; die Wildesel löschen ihren Durst.
Huwapa maji wanyama wote wa kondeni, punda-mwitu huzima kiu yao.
12 Über ihnen wohnen die Vögel des Himmels; die lassen aus dem Dickicht ihre Stimme erschallen.
Ndege wa angani hufanya viota kando ya maji, huimba katikati ya matawi.
13 Du tränkst die Berge von deinem Söller herab; von der Frucht deiner Werke wird die Erde satt.
Huinyeshea milima kutoka orofa zake, dunia inatoshelezwa kwa matunda ya kazi yake.
14 Du lässest Gras wachsen für das Vieh und Pflanzen, die der Mensch bearbeiten soll, um Nahrung aus der Erde zu ziehen;
Huyafanya majani ya mifugo yaote, na mimea kwa watu kulima, wajipatie chakula kutoka ardhini:
15 und damit der Wein des Menschen Herz erfreue und seine Gestalt schön werde vom Öl und das Brot das Herz des Menschen stärke.
divai ya kuufurahisha moyo wa mwanadamu, mafuta kwa ajili ya kungʼarisha uso wake, na mkate wa kutia mwili nguvu.
16 Die Bäume des HERRN trinken sich satt, die Zedern Libanons, die er gepflanzt hat,
Miti ya Bwana inanyeshewa vizuri, mierezi ya Lebanoni aliyoipanda.
17 woselbst die Vögel nisten und der Storch, der die Zypressen bewohnt.
Humo ndege hufanya viota vyao, korongo ana nyumba yake kwenye msunobari.
18 Die hohen Berge sind für die Steinböcke, die Felsenklüfte sind der Klippdachsen Zuflucht.
Milima mirefu ni makao ya mbuzi-mwitu, majabali ni kimbilio la pelele.
19 Er hat den Mond für bestimmte Zeiten gemacht; die Sonne weiß ihren Untergang.
Mwezi hugawanya majira, na jua hutambua wakati wake wa kutua.
20 Schaffst du Finsternis, und wird es Nacht, so regen sich alle Tiere des Waldes.
Unaleta giza, kunakuwa usiku, wanyama wote wa mwituni huzurura.
21 Die jungen Löwen brüllen nach Raub und verlangen ihre Nahrung von Gott.
Simba hunguruma kwa mawindo yao, na kutafuta chakula chao kutoka kwa Mungu.
22 Geht die Sonne auf, so ziehen sie sich zurück und legen sich in ihre Höhlen;
Jua huchomoza, nao huondoka, hurudi na kulala katika mapango yao.
23 der Mensch aber geht aus an sein Tagewerk, an seine Arbeit bis zum Abend.
Kisha mwanadamu huenda kazini mwake, katika kazi yake mpaka jioni.
24 HERR, wie sind deiner Werke so viel! Du hast sie alle weislich geordnet, und die Erde ist voll deiner Geschöpfe.
Ee Bwana, jinsi matendo yako yalivyo mengi! Kwa hekima ulizifanya zote, dunia imejaa viumbe vyako.
25 Da ist das Meer, so groß und weit ausgedehnt; darin wimmelt es ohne Zahl, kleine Tiere samt großen;
Pale kuna bahari, kubwa na yenye nafasi tele, imejaa viumbe visivyo na idadi, vitu vyenye uhai vikubwa na vidogo.
26 da fahren die Schiffe; der Leviatan, den du gemacht hast, um darin zu spielen.
Huko meli huenda na kurudi, pia Lewiathani, uliyemuumba acheze ndani yake.
27 Sie alle warten auf dich, daß du ihnen ihre Speise gebest zu seiner Zeit;
Hawa wote wanakutazamia wewe, uwape chakula chao kwa wakati wake.
28 wenn du ihnen gibst, so sammeln sie; wenn du deine Hand auftust, so werden sie mit Gut gesättigt;
Wakati unapowapa, wanakikusanya, unapofumbua mkono wako, wao wanashibishwa mema.
29 verbirgst du dein Antlitz, so erschrecken sie; nimmst du ihren Odem weg, so vergehen sie und werden wieder zu Staub;
Unapoficha uso wako, wanapata hofu, unapoondoa pumzi yao, wanakufa na kurudi mavumbini.
30 sendest du deinen Odem aus, so werden sie erschaffen, und du erneuerst die Gestalt der Erde.
Unapopeleka Roho wako, wanaumbwa, nawe huufanya upya uso wa dunia.
31 Die Herrlichkeit des HERRN währe ewig! Möge der HERR Freude erleben an seinen Werken!
Utukufu wa Bwana na udumu milele, Bwana na azifurahie kazi zake:
32 Blickt er die Erde an, so zittert sie; rührt er die Berge an, so rauchen sie.
yeye aitazamaye dunia, nayo ikatetemeka, aigusaye milima, nayo ikatoa moshi.
33 Ich will dem HERRN singen mein Leben lang, meinen Gott lobpreisen, solange ich noch bin.
Nitamwimbia Bwana maisha yangu yote; nitaimba sifa kwa Mungu wangu muda wote ninaoishi.
34 Möge mein Gedicht ihm wohlgefallen! Ich freue mich am HERRN.
Kutafakari kwangu na kumpendeze yeye, ninapofurahi katika Bwana.
35 Möchten die Sünder von der Erde vertilgt werden und die Gottlosen nicht mehr sein! Lobe den HERRN, meine Seele! Hallelujah!
Lakini wenye dhambi na watoweke katika dunia na waovu wasiwepo tena. Ee nafsi yangu, msifu Bwana. Msifuni Bwana.