< Job 41 >

1 Ziehst du das Krokodil mit der Angel heraus, legst du ihm einen Zaum ins Maul?
Je waweza kumvua mamba kwa ndoano ya samaki? Au kumfunga taya zake kwa kamba?
2 Kannst du einen Ring an seine Nase legen und einen Haken durch seine Kinnbacken stoßen?
Je waweza kuweka kamba katika pua zake, au kumtoboa taya yake kwa ndoano?
3 Wird es dich lange bitten oder dir Zärtlichkeiten sagen?
Je atafanya maombi mengi kwako? Je atazungumza na wewe kwa maneno laini?
4 Wird es einen Bund mit dir schließen, daß du es zum ewigen Knechte machest?
Je atafanya agano na wewe, ili kwamba umchukue kwa ajili ya mtumishi milele?
5 Kannst du mit ihm spielen wie mit einem Vögelein, oder es anbinden für deine Mädchen?
Je utacheza pamoja naye kama ambavyo ungecheza na ndege? Je utamfunga kwa ajili ya mtumishi wako wa kike?
6 Verkaufen es die Genossen untereinander, oder teilen es die Händler unter sich?
Je makundi ya wavuvi waweza kumfanyia biashara? Je watamgawanya ili kufanya biashara miongoni mwa wafanya biashara?
7 Kannst du seine Haut mit Pfeilen spicken und mit Fischerhaken seinen Kopf?
Je waweza kuijaza ngozi yake kwa vyusa au kichwa chake kwa mikuki ya kuvulia?
8 Lege deine Hand daran. Du wirst des Kampfes nicht vergessen, wirst es nicht zum zweitenmal tun!
Weka mkono wako juu yake mara moja, nawe utaikumbuka vita na hautaendelea kufanya hivyo tena.
9 Siehe, die Hoffnung auf dasselbe wird getäuscht; fällt man nicht schon bei seinem Anblick dahin?
Tazama, matumaini ya kila mtu ambaye hufanya hivyo ni uongo; je si kila mmoja atatupwa chini katika nchi mbele yake?
10 Niemand ist so kühn, daß er es reizen möchte; wer kann aber vor Mir bestehen?
Hakuna aliye mkali ambaye aweza kuthubutu kumtikisa mamba; Ni nani basi awezaye kusimama mbele yake?
11 Wer ist mir zuvorgekommen, daß ich es ihm vergelte? Unter dem ganzen Himmel ist alles mein!
Ni nani kwanza aliyenipa kitu chochote ili kwamba niweze kumlipa? Chochote kilicho chini ya anga ni changu.
12 Ich will von seinen Gliedern nicht schweigen, sondern reden von seiner großen und schönen Gestalt.
Sitanyamaza kimya kuhusu miguu ya mamba, wala kuhusu jambo linalohusu nguvu zake, wala kuhusu umbo lake zuri.
13 Wer entblößt es von seinem Schuppenpanzer und greift ihm in sein doppeltes Gebiß?
Nani awezaye kuiondoa ngozi yake? Nani anaweza kumchoma kwa silaha mara mbili?
14 Wer öffnet die Türen seines Rachens? Seine Zähne verbreiten Schrecken.
Nani awezaye kuifungua milango ya uso wake, imezungukwa na meno yake ambayo yanaogofya?
15 Prächtig sind seine starken Schilder, fest zusammengeschlossen und versiegelt;
Mgongo wake umefanywa kwa magamba yenye mistari, yamefungwa kwa pamoja kama chapa.
16 einer fügt sich an den andern, daß kein Luftzug dazwischen kommt;
Moja li karibu na jingine na ya kuwa hakuna hewa inaweza kupita katikati yake.
17 sie hängen fest zusammen, sind geschlossen und trennen sich nicht.
Yameunganishwa moja kwa jingine; yamegandamana kwa pamoja, ili kwamba hayawezi kutenganishwa.
18 Sein Niesen strahlt wie Licht, und seine Augen sind wie die Wimpern der Morgenröte.
Mwanga hung'ara kutoka katika kupumua kwake; macho yake ni kama kope za mapambazuko ya asubuhi.
19 Aus seinem Rachen schießen Fackeln, Feuerfunken entsprühen ihm.
Ndani ya mdomo wake hutoka miali ya mwanga, chembe za moto huruka nje.
20 Dampf geht auf von seinen Nüstern, und der Sumpf wird wie ein siedender Topf.
Katika pua zake hutoka moshi kama chungu kinachotokota juu ya moto ambao umechochewa ili uwe na joto sana.
21 Sein Atem facht Kohlen an, eine Flamme schießt aus seinem Munde.
Pumzi yake huwasha mkaa na kuwa mwali; moto hutoka katika mdomo wake.
22 Stärke wohnt auf seinem Nacken und Schrecken zieht vor ihm her.
Katika shingo yake kuna nguvu, na kitisho hucheza mbele yake.
23 Die Wampen seines Fleisches sitzen fest wie angegossen und bewegen sich nicht.
Nofu za mwili wake zimeunganishwa pamoja; ziko imara katika yeye; wala haziwezi kuondolewa.
24 Sein Herz ist hart wie Stein und so fest wie der untere Mühlstein.
Moyo wake ni mgumu kama jiwe - hakika, ni mgumu kama jiwe la chini la kusagia.
25 Die Helden erbeben, wenn es auffährt; vor Zittern geht ihr Bogen fehl.
Na anaposimama mwenyewe, hata miungu huogopa; hurudi nyuma kwasababu ya hofu.
26 Greift man es mit dem Schwerte an, so haftet dieses nicht, kein Speer, kein Wurfspieß und kein Pfeil.
Na ikiwa atapigwa kwa upanga, hauwezi kumfanya kitu chochote, wala mkuki, wala mshale, wala aina yoyote ya silaha iliyochongoka.
27 Es achtet Eisen für einen Strohhalm, und Erz für faules Holz.
Yeye hufikiri juu ya chuma kana kwamba ni majani makavu na hufikiri juu ya fedha kana kwamba ni ubao uliooza.
28 Kein Pfeil vermag es in die Flucht zu schlagen, und Schleudersteine fallen wie Spreu von ihm ab.
Mshale hauwezi akamfanya akimbie; kwake yeye mawe ya kombeo huwa kama makapi.
29 Es achtet die Keule für einen Halm und verlacht das Sausen der Spieße.
Marungu huyaangalia kama majani makavu; yeye hucheka juu ya mkuki unaovuma.
30 Unter ihm sind spitze Scherben, es zieht wie ein Dreschschlitten über den Schlamm dahin.
Sehemu zake za chini zi kama vipande vilivyochongoka vya vyungu; huacha alama zilizosambaa katika udongo kana kwamba alikuwa ni chombo cha kusagia.
31 Es macht die Tiefe sieden wie einen Kessel, macht das Meer zu einem Salbentopf.
Yeye hukifanya kilindi kichemke kama chungu cha maji ya moto; huifanya bahari kama chungu cha lihamu.
32 Hinter ihm her leuchtet der Pfad, es macht die Flut den Silberhaaren gleich.
Yeye huifanya njia ing'are nyuma yake; mtu mmoja angedhani kilindi kuwa cheupe.
33 Auf Erden ist nicht seinesgleichen; es ist gemacht, um ohne Furcht zu sein.
Hakuna cha kumlinganisha juu ya dunia, ambaye yeye alikuwa ameumbwa kuishi pasipo hofu.
34 Es schaut alle Hohen [furchtlos] an, es ist ein König über alle Stolzen.
Hukiona kila kitu chenye kiburi; yeye ni mfalme juu ya wana wote wa kiburi.”

< Job 41 >