< Job 38 >

1 Da antwortete der HERR dem Hiob aus dem Gewittersturm und sprach:
Kisha Bwana akamjibu Ayubu kutoka upepo wa kisulisuli. Akasema:
2 Wer verfinstert da Gottes Rat mit seinen unverständigen Reden?
“Nani huyu atiaye mashauri yangu giza kwa maneno yasiyo na maarifa?
3 Gürte doch deine Lenden wie ein Mann! Ich will dich fragen, lehre mich!
Jikaze kama mwanaume; nitakuuliza swali, nawe unijibu.
4 Wo warst du, als ich den Grund der Erde legte? Sage an, wenn du es weißt!
“Ulikuwa wapi nilipoweka misingi ya dunia? Niambie, kama unafahamu.
5 Wer hat ihre Maße bestimmt? Weißt du das? Oder wer hat die Meßschnur über sie ausgespannt?
Ni nani aliyeweka alama vipimo vyake? Hakika wewe unajua! Ni nani aliyenyoosha kamba ya kupimia juu yake?
6 Worauf wurden ihre Grundpfeiler gestellt, oder wer hat ihren Eckstein gelegt,
Je, misingi yake iliwekwa juu ya nini, au ni nani aliyeweka jiwe la pembeni,
7 als die Morgensterne miteinander jauchzten und alle Söhne Gottes jubelten?
wakati nyota za asubuhi zilipoimba pamoja, na malaika wote walipokuwa wakipiga kelele kwa furaha?
8 Wer hat das Meer mit Dämmen umgeben, als es hervorbrach wie aus Mutterleib,
“Ni nani aliyeifungia bahari milango ilipopasuka kutoka tumbo,
9 da ich es in Wolken kleidete und es in dicke Nebel, wie in Windeln band;
nilipoyafanya mawingu kuwa vazi lake, na kuyafungia katika giza nene,
10 da ich ihm seine Grenze zog und ihm Damm und Riegel gab und zu ihm sprach:
nilipoamuru mipaka yake, na kuiweka milango yake na makomeo mahali pake,
11 «Bis hierher sollst du kommen und nicht weiter, hier soll sich legen deiner Wellen Stolz!»?
niliposema, ‘Unaweza kufika mpaka hapa wala si zaidi; hapa ndipo mawimbi yako yenye kiburi yatakapokomea’?
12 Hast du zu deiner Zeit den Sonnenaufgang angeordnet und dem Morgenrot seinen Platz angewiesen,
“Umepata kuiamrisha asubuhi ipambazuke, au kuyaonyesha mapambazuko mahali pake,
13 daß es die Enden der Erde ergreife, damit die Frevler von ihr abgeschüttelt werden?
yapate kushika miisho ya dunia, na kuwakungʼuta waovu waliomo?
14 Sie wandelt sich wie Ton unter dem Siegel und alles steht da wie ein [Pracht-]Gewand;
Dunia hubadilika kama udongo wa mfinyanzi chini ya lakiri; sura yake hukaa kama ile ya vazi.
15 den Gottlosen wird ihr Licht entzogen und der Frevler Arm zerbricht.
Waovu huzuiliwa nuru yao, nao mkono wao ulioinuliwa huvunjwa.
16 Bist du auch bis zu den Meeresquellen gekommen, oder hast du die Meerestiefe ausgeforscht?
“Je, umepata kufika kwenye chemchemi za bahari? Au kutembea mahali pa ndani pa vilindi?
17 Sind dir die Tore des Todes geöffnet worden, oder hast du die Tore des Todesschattens gesehen?
Umewahi kuonyeshwa malango ya mauti? Umewahi kuiona milango ya uvuli wa mauti?
18 Hast du die Breiten der Erde überschaut? Weißt du das alles, so sage es mir!
Je, wewe unafahamu ukubwa wa dunia? Niambie kama unajua haya yote.
19 Welches ist der Weg zu den Wohnungen des Lichts, und wo hat die Finsternis ihren Ort,
“Njia ya kufika kwenye makao ya nuru ni ipi? Nako maskani mwa giza ni wapi?
20 daß du bis zu ihrer Grenze gelangen und den Pfad zu ihrem Hause finden könntest?
Je, unaweza kuvirudisha kwenye makao yake? Unajua njia za kufika maskani mwake?
21 Du weißt es, denn zu der Zeit warst du geboren, und die Zahl deiner Tage ist groß!
Hakika unajua, kwa kuwa ulikuwa umeshazaliwa! Kwani umeishi miaka mingi!
22 Bist du auch bis zu den Vorratskammern des Schnees gekommen, und hast du die Speicher des Hagels gesehen,
“Je, umeshawahi kuingia katika ghala za theluji, au kuona ghala za mvua ya mawe,
23 die ich aufbehalten habe für die Zeit der Not, für den Tag des Krieges und des Streits?
ambazo nimeziweka akiba kwa ajili ya wakati wa taabu, na kwa ajili ya wakati wa vita na mapigano?
24 Auf welche Weise verteilt sich das Licht, und wie verbreitet sich der Ostwind über die Erde?
Ni ipi njia iendayo mahali umeme wa radi unapotawanyiwa, au mahali upepo wa mashariki unaposambaziwa juu ya dunia?
25 Wer hat dem Regenstrom sein Bett gegraben und dem Donnerstrahl einen Weg gebahnt,
Ni nani aliyepasua mifereji kwa ajili ya maji mengi ya mvua yaendayo kasi na njia ya umeme wa radi,
26 damit es regne auf unbewohntes Land, auf die Wüste, wo kein Mensch ist,
ili kusababisha mvua kunyeshea mahali pasipokaliwa na mtu, jangwa lisilo na yeyote ndani yake,
27 um zu sättigen die Einöde und Wildnis, damit das junge Grün gedeihen kann?
ili kuitosheleza nchi ya ukiwa na jangwa, na majani yaanze kumea ndani yake?
28 Hat der Regen auch einen Vater, und wer hat die Tropfen des Taues erzeugt?
Je, mvua ina baba? Ni nani baba azaaye matone ya umande?
29 Aus wessen Leibe ist das Eis hervorgegangen, und wer hat des Himmels Reif geboren?
Barafu inatoka tumbo la nani? Ni nani azaaye ukungu kutoka mbinguni,
30 Wie zu Stein erstarren die Gewässer, und der Wasserspiegel schließt sich fest zusammen.
wakati maji yawapo magumu kama jiwe, wakati uso wa vilindi vya maji unapoganda?
31 Hast du die Bande des Siebengestirns geknüpft, oder kannst du die Fesseln des Orion lösen?
“Je, waweza kuufunga mnyororo wa Kilimia? Waweza kulegeza kamba za Orioni?
32 Kannst du die Zeichen des Tierkreises zu ihrer Zeit herausführen, und leitest du den Großen Bären samt seinen Jungen?
Waweza kuyaongoza makundi ya nyota kwa majira yake, au kuongoza Dubu na watoto wake?
33 Kennst du die Gesetze des Himmels, oder bestimmst du seine Herrschaft über die Erde?
Je, unajua sheria zinazotawala mbingu? Waweza kuweka utawala wa Mungu duniani?
34 Kannst du deine Stimme zu den Wolken erheben [und befehlen], daß dich Regengüsse bedecken?
“Waweza kuiinua sauti yako mpaka mawinguni, na kujifunika mwenyewe na gharika ya maji?
35 Kannst du Blitze entsenden, daß sie hinfahren und zu dir sagen: Siehe, hier sind wir?
Je, wewe hutuma umeme wa radi kwenye njia zake? Je, hutoa taarifa kwako kukuambia, ‘Sisi tuko hapa’?
36 Wer hat Weisheit in die Nieren gelegt, oder wer hat dem Herzen Verstand verliehen?
Ni nani aliyeujalia moyo hekima au kuzipa akili ufahamu?
37 Wer zählt die Wolken mit Weisheit, und wer schüttet die Schläuche des Himmels aus,
Nani mwenye hekima ya kuyahesabu mawingu? Ni nani awezaye kuinamisha magudulia ya mbinguni
38 daß der Staub zu Klumpen wird und die Schollen aneinander kleben?
wakati mavumbi yawapo magumu, na mabonge ya udongo kushikamana pamoja?
39 Jagst du der Löwin ihre Beute und stillst die Begierde der jungen Löwen,
“Je, utamwindia simba jike mawindo, na kuwashibisha simba wenye njaa
40 wenn sie in ihren Höhlen kauern, im Dickicht auf der Lauer liegen?
wakati wao wamejikunyata mapangoni mwao, au wakivizia kichakani?
41 Wer bereitet den Raben ihre Speise, wenn ihre Jungen zu Gott schreien und aus Mangel an Nahrung herumflattern?
Ni nani ampaye kunguru chakula wakati makinda yake yanamlilia Mungu, yakizungukazunguka kwa ajili ya kukosa chakula?

< Job 38 >