< Job 29 >

1 Und Hiob fuhr in dem Vortrag seiner Sprüche fort und sprach:
Ayubu akaendelea na hoja yake, akasema:
2 Wer gibt mir die vorigen Monate zurück und die Tage, in welchen Gott mich behütete?
“Tazama jinsi ninavyoitamani miezi iliyopita, zile siku ambazo Mungu alikuwa akinilinda,
3 als seine Leuchte über meinem Haupte schien und ich in seinem Lichte durch das Dunkel ging;
wakati taa yake iliniangazia kichwani changu, na kwa mwanga wake Mungu nikapita katikati ya giza!
4 wie ich in den Tagen meines Herbstes vertrauten Umgang mit Gott bei meinem Zelte pflog;
Natamani siku zile nilizokuwa katika ustawi wangu, wakati urafiki wa Mungu wa ndani ulipoibariki nyumba yangu,
5 als der Allmächtige noch mit mir war und meine Knaben um mich her;
wakati Mwenyezi alikuwa pamoja nami, nao watoto wangu walikuwa wamenizunguka,
6 da ich meine Tritte in Milch badete und der Fels neben mir Öl in Strömen goß;
wakati njia yangu ilikuwa imenyweshewa siagi, nao mwamba ukanimiminia vijito vya mafuta ya zeituni.
7 als ich noch zum Tore ging, zur Stadt hinauf, und meinen Sitz auf dem Markt aufstellte.
“Wakati nilipokwenda kwenye lango la mji na kuketi katika kiwanja,
8 Wenn mich die Knaben sahen, so verbargen sie sich, die Greise standen auf und blieben stehen.
vijana waliniona wakakaa kando, nao wazee walioketi wakasimama;
9 Die Fürsten hörten auf zu reden und legten die Hand auf den Mund.
wakuu wakaacha kuzungumza na kuziba vinywa vyao kwa mikono yao;
10 Die Stimme der Vornehmen stockte, und ihre Zunge klebte am Gaumen.
wenye vyeo wakanyamazishwa, nazo ndimi zao zikagandamana na makaakaa ya vinywa vyao.
11 Wessen Ohr mich hörte, der pries mich glücklich, und wessen Auge mich sah, der stimmte mir zu.
Yeyote aliyenisikia alinena mema juu yangu, nao walioniona walinisifu,
12 Denn ich rettete den Elenden, der da schrie, und das Waislein, das keinen Helfer hatte.
kwa sababu nilimwokoa maskini aliyeomba msaada, naye yatima aliyekuwa hana wa kumsaidia.
13 Der Segen des Verlorenen kam über mich, und ich machte das Herz der Witwe jauchzen.
Mtu aliyekuwa karibu kufa alinibariki, nami niliufanya moyo wa mjane kuimba.
14 Gerechtigkeit zog ich an, und sie bekleidete mich, mein Talar und Turban war das Recht.
Niliivaa haki kama vazi langu; uadilifu ulikuwa joho langu na kilemba changu.
15 Ich war des Blinden Auge und des Lahmen Fuß.
Nilikuwa macho ya kipofu na miguu kwa kiwete.
16 Ich war des Armen Vater; und die Streitsache, die ich nicht kannte, untersuchte ich.
Nilikuwa baba kwa mhitaji; nilimtetea mgeni.
17 Ich zerbrach die Stockzähne des Ungerechten und riß ihm den Raub aus den Zähnen.
Niliyavunja meno makali ya waovu, na kuwapokonya wahanga kwenye meno yao.
18 Und so dachte ich, ich würde mit meinem Neste sterben und wie der Phönix viele Tage erleben.
“Nikafikiri, ‘Nitafia katika nyumba yangu mwenyewe, nazo siku zangu zitakuwa nyingi kama chembechembe za mchanga.
19 Meine Wurzel war an Wassern ausgebreitet, und der Tau übernachtete auf meinem Zweig.
Mizizi yangu itafika mpaka kwenye maji, nao umande utakaa juu ya matawi yangu usiku kucha.
20 Meine Herrlichkeit erneuerte sich bei mir, und mein Bogen verjüngte sich in meiner Hand.
Utukufu wangu utabakia kuwa mpya ndani yangu, upinde wangu daima utaendelea kuwa mpya mkononi mwangu.’
21 Auf mich hörte und wartete man und lauschte stillschweigend auf meinen Rat.
“Watu walinisikiliza kwa tumaini, wakingojea ushauri wangu kwa utulivu.
22 Auf meine Rede folgte kein Widerspruch, und meine Worte träufelten auf sie.
Baada ya mimi kuzungumza, hawakusema zaidi; maneno yangu yaliingia masikioni mwao kwa makini.
23 Sie harrten auf mich, wie das Erdreich auf einen Regen, und sperrten ihren Mund auf, wie nach einem Spätregen.
Waliningojea kama manyunyu ya mvua na kuyapokea maneno yangu kama ardhi inyonyavyo mvua ya vuli.
24 Lächelte ich sie an, so konnten sie es kaum glauben, und das Licht meines Angesichts konnten sie nicht verdunkeln.
Walipokata tamaa niliwaonyesha uso wa furaha; nuru ya uso wangu ilikuwa ya thamani kwao.
25 Ich prüfte ihren Weg und saß oben an und wohnte wie ein König unter dem Volke, wie einer, der die Traurigen tröstet.
Niliwachagulia njia na kukaa kama mkuu wao; niliishi kama mfalme katikati ya majeshi yake; nikawa kama yeye anayewafariji waombolezaji.

< Job 29 >