< Job 21 >

1 Darauf antwortete Hiob und sprach:
Kisha Ayubu akajibu na kusema,
2 Hört, hört, was ich zu sagen habe; das soll der Trost sein, den ihr mir gewährt!
“Sikilizeni hotuba yangu kwa makini, hii na iwe faraja yenu.
3 Erlaubet mir, daß ich rede; und wenn ich gesprochen habe, mögt ihr spotten!
Nimeteswa, lakini pia nitasema; nikisha kusema, endeleeni kudhihaki.
4 Richte ich meine Klage an einen Menschen? Und warum sollte ich nicht ungeduldig sein?
Lakini kwangu mimi, malalamikio yangu ni kwa mtu? Kwa nini nisiwe mwenye subira?
5 Wendet euch zu mir und erstaunet und leget die Hand auf den Mund!
Nitazameni na mshangae, nanyi wekeni mkono wenu midomoni mwenu.
6 Ja, wenn ich daran denke, so erschrecke ich, und Zittern erfaßt meinen Leib.
Ninapoyafikiria mateso yangu, ninaumizwa, mwili wangu unaogopa.
7 Warum leben denn die Gottlosen, werden alt, groß und stark?
Kwa nini waovu wanaendelea kuishi, wanazeeka, na kuwa na uwezo katika madaraka?
8 Ihr Same ist beständig vor ihnen, und ihre Sprößlinge wachsen vor ihren Augen um sie her.
Wazao wao wanathibitishwa mbele zao, na uzao wao unaimarika machoni pao.
9 Ihre Häuser sind in Frieden, ohne Furcht; die Rute Gottes schlägt sie nicht.
Nyumba zao ziko salama mbali na hofu; wala fimbo ya Mungu haiko juu yao.
10 Ihr Ochse bespringt, und nicht umsonst; ihre Kühe kalben und sind nicht unfruchtbar.
Dume lao la ng'ombe linazalisha; halishindwi kufanya hivyo; ng'ombe wao anazaa na hafishi ndama wake akiwa mchanga.
11 Ihre Buben lassen sie ausziehen wie eine Schafherde, und ihre Kinder hüpfen herum.
Wanawapeleka wadogo wao kama kundi la kondoo, na watoto wao hucheza.
12 Sie singen laut zur Pauke und Harfe und sind fröhlich beim Klang der Schalmei.
Wanaimba kwa tari na vinubi na hufurahi kwa muziki na zomari.
13 Sie verbringen in Wohlfahrt ihre Tage und fahren in einem Augenblick ins Totenreich hinab. (Sheol h7585)
Wanatumia siku zao katika mafanikio, na wanashuka kuzimu kwa utulivu. (Sheol h7585)
14 Und doch sprechen sie zu Gott: «Hebe dich weg von uns; der Erkenntnis deiner Wege fragen wir nichts nach!
Wanamwambia Mungu, 'Ondoka kwetu kwani hatutaki ufahamu wowote juu ya njia zako.
15 Was sollten wir dem Allmächtigen dienen, und was nützt es uns, ihn anzurufen?»
Mwenye enzi ni nani, hata tumwabudu? Tutafaidika na nini tukimwabudu? Tutapata faida gani ikiwa tutamwomba?
16 Und doch steht ihr Glück nicht in ihrer Hand; darum sei der Rat der Gottlosen fern von mir!
Tazama, je mafanikio yao hayamo katika mikono yao wenyewe? Sina cha kufanya na ushauri wa waovu.
17 Wie oft erlischt die Leuchte der Gottlosen und ereilt sie ihr Schicksal? Teilt Er ihnen Schmerzen zu in seinem Zorn?
Mara ngapi taa za waovu huzimwa, au kwamba majanga huja juu yao? Mara ngapi inatokea kwamba Mungu husambaza huzuni kwao kwa hasira?
18 Werden sie wie Stroh vor dem Wind und wie Spreu, die der Sturm entführt?
Ni mara ngapi inatokea kwamba wanakuwa kama mabua mbele ya upepo au kama makapi yanayopeperushwa na dhoruba?
19 Spart Gott sein Unglück für seine Kinder auf? Ihm selbst sollte er vergelten, so daß er es weiß!
Mnasema, 'Mungu huweka hatia ya mtu kwa watoto wake kuilipa.' Na alipe yeye mwenyewe, ili kwamba aweze kujua hatia yake mwenyewe.
20 Seine eigenen Augen sollen sein Verderben sehen, und den Zorn des Allmächtigen soll er selbst trinken!
Acha macho yake yaone uangamivu wake mwenyewe, na acha anywe gadhabu ya Mwenyezi.
21 Denn was für Freude wird er an seiner Nachkommenschaft haben, wenn die Zahl seiner Monde abgeschnitten ist?
Kwani anaangaliaje familia yake mbele yake idadi ya miezi yake inapokwisha.
22 Kann man Gott Erkenntnis lehren, da er doch die Himmlischen richtet?
Je kuna mtu anaweza kumfundisha Mungu maarifa kwa kuwa yeye huwaukumu hata walio juu?
23 Der eine stirbt im Vollbesitz seines Glücks, vollkommen ruhig und sorglos;
Mtu mmoja ufa katika nguvu zake kamili, akiwa na utulivu kabisa na kwa amani.
24 seine Tröge fließen über von Milch, und das Mark seiner Gebeine wird getränkt.
Mwili wake hauna uhitaji, na kiini cha mifupa yake ina unyevu na afya njema.
25 Der andere aber stirbt mit betrübter Seele und hat nie Gutes geschmeckt:
Mtu mwingine ufa kwa uchungu wa nafsi, bila kujifurahisha kwa jambo lolote jema.
26 Gemeinsam liegen sie im Staube, und Gewürm bedeckt sie beide.
Wanazikwa kaburini wote kwa pamoja, funza wanawafunika wote.
27 Seht, ich kenne eure Gedanken und die Anschläge, mit denen ihr mir Unrecht tut.
Tazama, nayajua mawazo yenu, na jinsi mnavyotaka kunikosesha.
28 Denn ihr denkt: Wo ist das Haus des Tyrannen hingekommen? Und wo ist das Zelt, darin die Gottlosen wohnten?
Kwa kuwa mwasema, 'Iko wapi sasa nyumba ya mwana wa mfalme? Liko wapi kao alipokaa mwovu?'
29 Habt ihr euch nicht bei denen erkundigt, die des Weges zogen? Und könnt ihr ihre Zeichen nicht anerkennen,
Je hamjawauliza wasafiri? Hamfahamu wanavyoweza kusema,
30 daß der Böse am Tage des Unglücks verschont bleibt und dem Tage des Zorns entgeht?
kwamba mwovu anaepushwa na siku ya shida, na kwamba anawekwa mbali na siku ya gadhabu?
31 Wer kann ihm ins Gesicht seinen Wandel vorhalten, und sein Tun, wer vergilt es ihm?
Ni nani atakaye ituhumu siku ya mwovu mbele yake? Ni nani atakayemwadhibu kwa alichokifanya?
32 Doch er wird zu Grabe getragen, und über seinem Grabhügel hält man Wache.
Hata hivyo atapelekwa kaburini; watu wataliona kaburi lake.
33 Süß sind ihm des Grabes Schollen; hinter ihm her zieht jedermann, und vor ihm her eine unzählbare Schar.
Udongo wa bondeni utakuwa mtamu kwake; watu wote watamfuata, hata kuwe na watu wengi mbele yake.
34 Was tröstet ihr mich denn so vergeblich? Eure Antworten sind nichts als Treulosigkeit!
Ni jinsi gani basi mtanifariji bila kufikiri, kwa kuwa majibu yenu hayana lolote ila uongo?”

< Job 21 >