< 1 Mose 5 >

1 Dies ist das Buch von Adams Geschlecht: Am Tage, da Gott den Menschen schuf, machte er ihn Gott ähnlich;
Hii ni orodha ya vizazi vya Adamu. Katika siku ambayo Mungu alimuumba mtu, aliwaumba katika mfano wake mwenyewe.
2 männlich und weiblich schuf er sie und segnete sie und nannte ihren Namen Adam, am Tage, da er sie schuf.
Mwanaume na mwanamke aliwaumba. Akawabariki na akawaita Adam wakati walipoumbwa.
3 Und Adam war 130 Jahre alt, als er einen Sohn zeugte, ihm selbst gleich, nach seinem Bilde, und nannte ihn Seth.
Wakati Adamu alipokuwa ameishi miaka 130, akamzaa mwana katika sura yake mwenyewe, kwa mfano wake, na akamuita jina lake Sethi.
4 Und nachdem er den Seth gezeugt, lebte Adam noch 800 Jahre und zeugte Söhne und Töchter;
Baada ya Adamu kumzaa Sethi, aliishi miaka mia nane. Akawazaa wana wengi waume na wake.
5 also daß Adams ganzes Alter 930 Jahre betrug, als er starb.
Adamu akaishi miaka 930 kisha akafariki.
6 Seth war 105 Jahre alt, als er den Enosch zeugte;
Wakati Sethi alipokuwa ameishi miaka 105, akamzaa Enoshi.
7 und Seth, nachdem er den Enosch gezeugt, lebte 807 Jahre und zeugte Söhne und Töchter;
Baada ya kumzaa Enoshi, akaishi miaka 807 na akawazaa wana wengi waume na wake.
8 also daß Seths ganzes Alter 912 Jahre betrug, als er starb.
Sethi akaishi miaka 912 kisha akafariki.
9 Enosch war 90 Jahre alt, als er den Kenan zeugte;
Wakati Enoshi alipokuwa ameishi miaka tisini, akamzaa Kenani.
10 und Enosch, nachdem er den Kenan gezeugt, lebte 815 Jahre und zeugte Söhne und Töchter;
Baada ya kumzaa Kenani, Enoshi aliishi miaka 815. Akazaa wana wengi wa ume na wake.
11 also daß Enoschs ganzes Alter 905 Jahre betrug, als er starb.
Enoshi aliishi miaka 905 na kisha akafariki.
12 Kenan war 70 Jahre alt, als er den Mahalaleel zeugte;
Wakati Kanani alipokuwa ameishi miaka sabini, akamzaa Mahalaleli.
13 und Kenan, nachdem er den Mahalaleel gezeugt, lebte 840 Jahre und zeugte Söhne und Töchter;
Baada ya kumzaa Mahalaleli, Kenani aliishi miaka 840. Akawazaa wana wengi wa ume na wake.
14 also daß Kenans ganzes Alter 910 Jahre betrug, da er starb.
Kenani aliishi miaka 910, na kisha akafariki.
15 Mahalaleel war 65 Jahre alt, als er den Jared zeugte;
Mahalaleli alipokuwa ameishi miaka sitini na tano, alimzaa Yaredi.
16 und Mahalaleel, nachdem er den Jared gezeugt, lebte 830 Jahre und hat Söhne und Töchter gezeugt;
Baada ya kumzaa Yaredi, Mahalaleli aliishi miaka 830. Akazaa wana wengi wa ume na wake.
17 also daß Mahalaleels ganzes Alter 895 Jahre betrug, als er starb.
Mahalaleli aliishi miaka 895 na kisha akafariki.
18 Jared war 162 Jahre alt, als er den Henoch zeugte;
Yaredi alipokuwa ameishi miaka 162, alimzaa Henoko.
19 und Jared, nachdem er den Henoch gezeugt, lebte 800 Jahre und zeugte Söhne und Töchter;
Baada ya kumzaa Henoko, Yaredi aliishi miaka mianane. Akazaa wana wengi waume na wake.
20 also daß Jareds ganzes Alter 962 Jahre betrug, da er starb.
Yaredi aliishi miaka 962 na kisha akafariki.
21 Henoch war 65 Jahre alt, als er den Methusalah zeugte;
Henoko alipokuwa ameishi miaka sitini na tano, akamzaa Methusela.
22 und Henoch, nachdem er den Methusalah gezeugt, wandelte er mit Gott 300 Jahre lang und zeugte Söhne und Töchter;
Henoko akaenenda na Mungu miaka miatatu baada ya kumzaa Methusela. Aliwazaa wana wengi wa ume na wake.
23 also daß Henochs ganzes Alter 365 Jahre betrug.
Henoko aliishi miaka 365.
24 Und Henoch wandelte mit Gott und war nicht mehr, weil Gott ihn zu sich genommen hatte.
Henoko alienenda na Mungu, na kisha alitoweka, kwa kuwa Mungu alimtwaa.
25 Methusalah war 187 Jahre alt, als er den Lamech zeugte;
Wakati Methusela alipokuwa ameishi miaka 187, alimzaa Lameki.
26 und Methusalah, nachdem er den Lamech gezeugt, lebte 782 Jahre und zeugte Söhne und Töchter;
Baada ya kumzaa Lameki, Methusela aliishi miaka 782. Akawazaa wana wengi wa ume na wake.
27 also daß Methusalahs ganzes Alter 969 Jahre betrug, da er starb.
Methusela aliishi miaka 969. Kisha akafariki.
28 Lamech war 182 Jahre alt, als er einen Sohn zeugte;
Wakati Lameki alipokuwa ameishi miaka 182, alimzaa mwana.
29 den nannte er Noah, indem er sprach: Der wird uns trösten ob unserer Hände Arbeit und Mühe, die herrührt von dem Erdboden, den der HERR verflucht hat!
Akamuita jina lake Nuhu, akisema, “Huyu ndiye atatupatia pumziko kutoka katika kazi yetu na kutoka katika kazi ya taabu ya mikono yetu, ambayo lazima tuifanye kwa sababu ya ardhi ambayo Yahwe ameilaani.”
30 Und Lamech, nachdem er den Noah gezeugt, lebte 590 Jahre lang und zeugte Söhne und Töchter;
Lameki aliishi miaka 595 baada ya kumzaa baba wa Nuhu. Akazaa wanawengi wa ume na wake.
31 also daß Lamechs ganzes Alter 772 Jahre betrug, da er starb.
Lameki aliishi miaka 777. Kisha akafariki.
32 Und Noah war 500 Jahre alt, da er den Sem, Ham und Japhet zeugte.
Baada ya Nuhu kuishi miaka miatano, akamzaa Shemu, Hamu, na Yafethi.

< 1 Mose 5 >