< 1 Mose 5 >

1 Dies ist das Buch von Adams Geschlecht: Am Tage, da Gott den Menschen schuf, machte er ihn Gott ähnlich;
Hii ni orodha iliyoandikwa ya vizazi vya Adamu. Wakati Mungu alipomuumba Adamu, alimfanya kwa sura ya Mungu.
2 männlich und weiblich schuf er sie und segnete sie und nannte ihren Namen Adam, am Tage, da er sie schuf.
Aliwaumba mwanaume na mwanamke, akawabariki. Walipokwisha kuumbwa, akawaita “mwanadamu.”
3 Und Adam war 130 Jahre alt, als er einen Sohn zeugte, ihm selbst gleich, nach seinem Bilde, und nannte ihn Seth.
Adamu alipokuwa ameishi miaka 130, alikuwa na mwana aliyekuwa na sura yake, mwenye kufanana naye. Akamwita Sethi.
4 Und nachdem er den Seth gezeugt, lebte Adam noch 800 Jahre und zeugte Söhne und Töchter;
Baada ya Sethi kuzaliwa, Adamu aliishi miaka 800, akawa na watoto wengine wa kiume na wa kike.
5 also daß Adams ganzes Alter 930 Jahre betrug, als er starb.
Adamu aliishi jumla ya miaka 930, ndipo akafa.
6 Seth war 105 Jahre alt, als er den Enosch zeugte;
Sethi alipokuwa ameishi miaka 105, akamzaa Enoshi.
7 und Seth, nachdem er den Enosch gezeugt, lebte 807 Jahre und zeugte Söhne und Töchter;
Baada ya kumzaa Enoshi, Sethi aliishi miaka 807, akawa na watoto wengine wa kiume na wa kike.
8 also daß Seths ganzes Alter 912 Jahre betrug, als er starb.
Sethi aliishi jumla ya miaka 912, ndipo akafa.
9 Enosch war 90 Jahre alt, als er den Kenan zeugte;
Enoshi alipokuwa ameishi miaka tisini, akamzaa Kenani.
10 und Enosch, nachdem er den Kenan gezeugt, lebte 815 Jahre und zeugte Söhne und Töchter;
Baada ya kumzaa Kenani, Enoshi aliishi miaka 815, naye alikuwa na watoto wengine wa kiume na wa kike.
11 also daß Enoschs ganzes Alter 905 Jahre betrug, als er starb.
Enoshi aliishi jumla ya miaka 905, ndipo akafa.
12 Kenan war 70 Jahre alt, als er den Mahalaleel zeugte;
Kenani alipokuwa ameishi miaka sabini, akamzaa Mahalaleli.
13 und Kenan, nachdem er den Mahalaleel gezeugt, lebte 840 Jahre und zeugte Söhne und Töchter;
Baada ya kumzaa Mahalaleli, Kenani aliishi miaka 840, akawa na watoto wengine wa kiume na wa kike.
14 also daß Kenans ganzes Alter 910 Jahre betrug, da er starb.
Kenani aliishi jumla ya miaka 910, ndipo akafa.
15 Mahalaleel war 65 Jahre alt, als er den Jared zeugte;
Mahalaleli alipokuwa ameishi miaka sitini na mitano, akamzaa Yaredi.
16 und Mahalaleel, nachdem er den Jared gezeugt, lebte 830 Jahre und hat Söhne und Töchter gezeugt;
Baada ya kumzaa Yaredi, Mahalaleli aliishi miaka 830, akawa na watoto wengine wa kiume na wa kike.
17 also daß Mahalaleels ganzes Alter 895 Jahre betrug, als er starb.
Mahalaleli aliishi jumla ya miaka 895, ndipo akafa.
18 Jared war 162 Jahre alt, als er den Henoch zeugte;
Yaredi alipokuwa ameishi miaka 162, akamzaa Enoki.
19 und Jared, nachdem er den Henoch gezeugt, lebte 800 Jahre und zeugte Söhne und Töchter;
Baada ya kumzaa Enoki, Yaredi aliishi miaka 800, naye akawa na watoto wengine wa kiume na wa kike.
20 also daß Jareds ganzes Alter 962 Jahre betrug, da er starb.
Yaredi aliishi jumla ya miaka 962, ndipo akafa.
21 Henoch war 65 Jahre alt, als er den Methusalah zeugte;
Enoki alipokuwa ameishi miaka sitini na mitano, akamzaa Methusela.
22 und Henoch, nachdem er den Methusalah gezeugt, wandelte er mit Gott 300 Jahre lang und zeugte Söhne und Töchter;
Baada ya kumzaa Methusela, Enoki alitembea na Mungu miaka 300, na akawa na watoto wengine wa kiume na wa kike.
23 also daß Henochs ganzes Alter 365 Jahre betrug.
Enoki aliishi jumla ya miaka 365.
24 Und Henoch wandelte mit Gott und war nicht mehr, weil Gott ihn zu sich genommen hatte.
Enoki akatembea na Mungu, kisha akatoweka, kwa sababu Mungu alimchukua.
25 Methusalah war 187 Jahre alt, als er den Lamech zeugte;
Methusela alipokuwa ameishi miaka 187, akamzaa Lameki.
26 und Methusalah, nachdem er den Lamech gezeugt, lebte 782 Jahre und zeugte Söhne und Töchter;
Baada ya kumzaa Lameki, Methusela aliishi miaka 782, akawa na watoto wengine wa kiume na wa kike.
27 also daß Methusalahs ganzes Alter 969 Jahre betrug, da er starb.
Methusela aliishi jumla ya miaka 969, ndipo akafa.
28 Lamech war 182 Jahre alt, als er einen Sohn zeugte;
Lameki alipokuwa ameishi miaka 182, alimzaa mwana.
29 den nannte er Noah, indem er sprach: Der wird uns trösten ob unserer Hände Arbeit und Mühe, die herrührt von dem Erdboden, den der HERR verflucht hat!
Akamwita jina lake Noa, akasema, “Yeye ndiye atakayetufariji katika kazi na maumivu makali ya mikono yetu yaliyosababishwa na ardhi iliyolaaniwa na Bwana.”
30 Und Lamech, nachdem er den Noah gezeugt, lebte 590 Jahre lang und zeugte Söhne und Töchter;
Baada ya Noa kuzaliwa, Lameki aliishi miaka 595, akawa na watoto wengine wa kiume na wa kike.
31 also daß Lamechs ganzes Alter 772 Jahre betrug, da er starb.
Lameki aliishi jumla ya miaka 777, ndipo akafa.
32 Und Noah war 500 Jahre alt, da er den Sem, Ham und Japhet zeugte.
Baada ya Noa kuishi miaka 500, aliwazaa Shemu, Hamu na Yafethi.

< 1 Mose 5 >