< 2 Samuel 22 >
1 Und David redete zu dem HERRN die Worte dieses Liedes, am Tage, als der HERR ihn aus der Hand aller seiner Feinde und aus der Hand Sauls errettet hatte.
Daudi alimwimbia Bwana maneno ya wimbo huu wakati Bwana alipomwokoa mikononi mwa adui zake wote, na pia mkononi mwa Sauli.
2 Er sprach: Der HERR ist meine Felsenkluft, meine Burg und meine Zuflucht;
Akasema: “Bwana ni mwamba wangu, ngome yangu na mwokozi wangu,
3 mein Gott ist mein Fels, darin ich mich berge, mein Schild und das Horn meines Heils, meine Festung und meine Zuflucht, mein Erretter, der mich von Gewalttat befreit.
Mungu wangu ni mwamba wangu, ambaye kwake ninakimbilia, ngao yangu na pembe ya wokovu wangu. Yeye ni ngome yangu, kimbilio langu na mwokozi wangu, huniokoa kutoka kwa watu wenye jeuri.
4 Den HERRN, den Hochgelobten, rief ich an und wurde von meinen Feinden errettet.
Ninamwita Bwana, anayestahili kusifiwa, nami ninaokolewa kutoka kwa adui zangu.
5 Todeswehen umfingen mich, Bäche Belials schreckten mich;
“Mawimbi ya mauti yalinizunguka, mafuriko ya maangamizi yalinilemea.
6 Stricke der Unterwelt umschlangen mich, Todesschlingen kamen mir entgegen. (Sheol )
Kamba za kuzimu zilinizunguka, mitego ya mauti ilinikabili. (Sheol )
7 In meiner Angst rief ich den HERRN an und schrie zu meinem Gott; er hörte in seinem Tempel meine Stimme, mein Schreien kam vor ihn zu seinen Ohren.
Katika shida yangu nalimwita Bwana, nilimlilia Mungu wangu. Kutoka Hekaluni mwake alisikia sauti yangu, kilio changu kikafika masikioni mwake.
8 Die Erde bebte und erzitterte, die Grundfesten des Himmels wurden erschüttert und bebten, weil er zornig war.
“Dunia ilitetemeka na kutikisika, misingi ya mbingu ikatikisika, vilitetemeka kwa sababu alikuwa amekasirika.
9 Rauch stieg auf von seiner Nase und verzehrendes Feuer aus seinem Mund, Feuerglut brannte daraus hervor.
Moshi ukapanda kutoka puani mwake, moto uteketezao ukatoka kinywani mwake, makaa ya moto yawakayo yakatoka ndani mwake.
10 Er neigte den Himmel und fuhr herab, und Dunkel war unter seinen Füßen;
Akazipasua mbingu akashuka chini, mawingu meusi yalikuwa chini ya miguu yake.
11 er fuhr auf dem Cherub und flog daher, er schwebte auf den Fittichen des Windes.
Alipanda juu ya kerubi akaruka, akapaa juu kwa mbawa za upepo.
12 Er machte Finsternis um sich her zu seinem Gezelt, dunkle Wasser, dichte Wolken.
Alifanya giza hema lake la kujifunika: mawingu meusi ya mvua ya angani.
13 Vom Glanz vor ihm brannte Feuerglut;
Kutokana na mwanga wa uwepo wake mawingu yalisogea, ikanyesha mvua ya mawe na umeme wa radi.
14 und der HERR donnerte vom Himmel, der Höchste ließ seine Stimme erschallen;
Bwana alinguruma kutoka mbinguni, sauti ya Aliye Juu Sana ilisikika.
15 er schoß seine Pfeile und zerstreute sie, [schleuderte] Blitze und schreckte sie.
Aliipiga mishale na kutawanya adui, umeme wa radi na kuwafukuza.
16 Da sah man die Betten des Meeres, und die Gründe des Erdbodens wurden aufgedeckt von des HERRN Schelten, von dem Schnauben seines grimmigen Zorns!
Mabonde ya bahari yalifunuliwa, na misingi ya dunia ikawa wazi kwa kukaripia kwake Bwana, kwa uvumi wa pumzi kutoka puani mwake.
17 Er langte herab aus der Höhe und ergriff mich, er zog mich aus großen Wassern;
“Alinyoosha mkono kutoka juu na kunishika; alinitoa kutoka kilindi cha maji makuu.
18 er rettete mich von meinem mächtigen Feind und von meinen Hassern; denn sie waren mir zu stark;
Aliniokoa kutoka adui wangu mwenye nguvu nyingi, kutoka adui zangu waliokuwa na nguvu nyingi kuliko mimi.
19 sie hatten mich überfallen zur Zeit meines Unglücks; aber der HERR ward mir zur Stütze
Walinikabili siku ya msiba wangu, lakini Bwana alikuwa msaada wangu.
20 und führte mich heraus in die Weite, er befreite mich; denn er hatte Wohlgefallen an mir.
Alinileta nje mahali penye nafasi tele, akaniokoa kwa kuwa alipendezwa nami.
21 Der HERR vergalt mir nach meiner Gerechtigkeit, nach der Reinheit meiner Hände lohnte er mir;
“Bwana alinitendea sawasawa na uadilifu wangu; sawasawa na usafi wa mikono yangu amenilipa.
22 denn ich habe die Wege des HERRN bewahrt und bin nicht abgefallen von meinem Gott,
Kwa maana nimezishika njia za Bwana; sijatenda ubaya nikamwacha Mungu wangu.
23 sondern ich hatte alle seine Rechte vor mir und stieß seine Satzungen nicht von mir,
Sheria zake zote zi mbele yangu, wala sijayaacha maagizo yake.
24 und ich hielt es ganz mit ihm und hütete mich vor meiner Sünde.
Nimekuwa sina hatia mbele zake, nami nimejilinda nisitende dhambi.
25 Darum vergalt mir der HERR nach meiner Gerechtigkeit, nach der Reinheit meiner Hände vor seinen Augen.
Bwana amenilipa sawasawa na uadilifu wangu, sawasawa na usafi wangu machoni pake.
26 Gegen den Frommen erzeigst du dich fromm, gegen den Redlichen redlich,
“Kwa yeye aliye mwaminifu unajionyesha kuwa mwaminifu, kwa asiye na hatia unajionyesha kutokuwa na hatia,
27 gegen den Reinen erzeigst du dich rein, aber den Hinterlistigen überlistest du.
kwa aliye mtakatifu unajionyesha kuwa mtakatifu, lakini kwa aliyepotoka unajionyesha kuwa mkaidi.
28 Denn du rettest alles elende Volk, aber du erniedrigst die Augen aller Stolzen.
Wewe huwaokoa wanyenyekevu, lakini macho yako ni juu ya wenye kiburi ili uwashushe.
29 Denn du, HERR, bist meine Leuchte; der HERR macht meine Finsternis licht;
Wewe ni taa yangu, Ee Bwana. Bwana hulifanya giza langu kuwa mwanga.
30 denn mit dir kann ich Kriegsvolk zerschmeißen und mit meinem Gott über die Mauern springen.
Kwa msaada wako naweza kushinda jeshi, nikiwa pamoja na Mungu wangu nitaweza kuruka ukuta.
31 Dieser Gott! Sein Weg ist vollkommen, die Rede des HERRN ist geläutert; er ist ein Schild allen, die ihm vertrauen.
“Kuhusu Mungu, njia yake ni kamilifu; neno la Bwana halina dosari. Yeye ni ngao kwa wote wanaokimbilia kwake.
32 Denn wer ist Gott, außer dem HERRN, und wer ist ein Fels, außer unserm Gott?
Kwa maana ni nani aliye Mungu zaidi ya Bwana? Ni nani aliye Mwamba isipokuwa Mungu wetu?
33 Gott umgürtet mich mit Kraft und macht meinen Weg unsträflich,
Mungu ndiye anivikaye nguvu na kufanya njia yangu kuwa kamilifu.
34 er macht meine Füße den Hirschen gleich und stellt mich auf meine Höhen;
Huifanya miguu yangu kama miguu ya kulungu, huniwezesha kusimama mahali palipo juu.
35 er lehrt meine Hände streiten und meine Arme den ehernen Bogen spannen;
Huifundisha mikono yangu kupigana vita; mikono yangu inaweza kupinda upinde wa shaba.
36 du gabst mir den Schild deines Heils, und deine Herablassung machte mich groß;
Hunipa ngao yako ya ushindi, unajishusha chini ili kuniinua.
37 du machtest mir Raum zum Gehen, daß meine Knöchel nicht wankten.
Huyapanua mapito yangu, ili miguu yangu isiteleze.
38 Ich jagte meinen Feinden nach und vertilgte sie und kehrte nicht um, bis sie aufgerieben waren;
“Niliwafuatia adui zangu na nikawaseta, sikurudi nyuma mpaka walipoangamizwa.
39 ich rieb sie auf und zerschmetterte sie, daß sie nicht mehr aufstehen konnten; sie fielen unter meine Füße.
Niliwaseta kabisa, nao hawakuweza kuinuka tena; walianguka chini ya miguu yangu.
40 Du hast mich gegürtet mit Kraft zum Streit, du hast unter mich gebeugt, die sich wider mich setzten.
Ulinivika nguvu kwa ajili ya kupigana vita; uliwafanya adui zangu wasujudu miguuni pangu.
41 Du wandtest mir den Rücken meiner Feinde zu, und meine Hasser habe ich vertilgt.
Uliwafanya adui zangu wageuke na kukimbia, nami nikawaangamiza adui zangu.
42 Sie schrieen, aber da war kein Retter; zu dem HERRN, aber er antwortete ihnen nicht.
Walipiga yowe, lakini hapakuwepo na yeyote wa kuwaokoa; walimlilia Bwana, lakini hakuwajibu.
43 Und ich zerrieb sie wie Erdenstaub, zertrat sie wie Straßenkot und warf sie hinaus.
Niliwaponda kama mavumbi ya nchi; niliwaponda na kuwakanyaga kama tope barabarani.
44 Du rettetest mich aus den Zänkereien des Volkes und bewahrtest mich auf zum Haupt der Heiden; ein Volk, das ich nicht kannte, dient mir;
“Umeniokoa kutokana na mashambulizi ya watu wangu; umenihifadhi mimi kama kiongozi wa mataifa. Watu ambao sikuwajua wananitumikia,
45 die Kinder der Fremden schmeicheln mir, sie folgen mir aufs Wort;
nao wageni huja wakininyenyekea, mara wanisikiapo, hunitii.
46 die Kinder der Fremden verzagen und kommen zitternd hervor aus ihren Schlössern.
Wote wanalegea, wanatoka katika ngome zao wakitetemeka.
47 Es lebt der HERR, und gepriesen sei mein Fels, und erhoben werde der Gott meines Heils!
“Bwana yu hai! Sifa ni kwa Mwamba wangu! Atukuzwe Mungu, Mwamba, Mwokozi wangu!
48 Der Gott, der mir Rache verlieh und mir die Völker unterwarf;
Yeye ndiye Mungu anilipiziaye kisasi, ayawekaye mataifa chini yangu,
49 der mich meinen Feinden entrinnen ließ und mich trotz meiner Widersacher erhöhte, mich errettete von dem gewalttätigen Mann!
aniwekaye huru toka kwa adui zangu. Uliniinua juu ya adui zangu; uliniokoa toka kwa watu wajeuri.
50 Darum will ich dich, o HERR, loben unter den Heiden und deinem Namen singen,
Kwa hiyo nitakusifu, Ee Bwana, katikati ya mataifa; nitaliimbia sifa jina lako.
51 der seinem Könige große Siege verliehen hat und seinem Gesalbten Gnade erweist, David und seinem Samen bis in Ewigkeit!
Humpa mfalme wake ushindi mkuu; huonyesha fadhili zake kwa mpakwa mafuta wake, kwa Daudi na wazao wake milele.”