< Psalm 76 >
1 Dem Musikmeister, mit Saitenspiel; ein Psalm von Asaph, ein Lied. Allbekannt ist Gott in Juda,
Kwa mwimbishaji. Kwa ala za nyuzi za muziki. Zaburi ya Asafu. Wimbo. Katika Yuda, Mungu anajulikana, jina lake ni kuu katika Israeli.
2 in Salem erstand seine Hütte und seine Wohnstatt in Zion.
Hema lake liko Salemu, makao yake katika Sayuni.
3 Allda hat er zerbrochen des Bogens Blitze, Schild und Schwert und jegliche Kriegswehr. (SELA)
Huko alivunja mishale imetametayo, ngao na panga, silaha za vita.
4 Ruhmvoll bist du, herrlich von den ewigen Bergen her.
Wewe unangʼaa kwa mwanga, mwenye fahari zaidi ya milima yenye utajiri wa wanyama pori.
5 Ausgeplündert wurden die tapferen Streiter, sanken hin in ihren Todesschlaf, und all den Helden versagte der Arm:
Mashujaa hulala wametekwa nyara, hulala usingizi wao wa mwisho; hakuna hata mmoja wa watu wa vita anayeweza kuinua mikono yake.
6 vor deinem Drohruf, du Gott Jakobs, sanken in Betäubung so Wagen wie Rosse.
Kwa kukemea kwako, Ee Mungu wa Yakobo, farasi na gari la vita vilikaa kimya.
7 Ja du bist furchtbar, und wer kann bestehn vor dir, sobald dein Zorn entbrannt ist?
Wewe peke yako ndiye wa kuogopwa. Ni nani awezaye kusimama mbele yako unapokasirika?
8 Vom Himmel her kündigtest du das Gericht an: da erschrak die Erde und wurde still,
Kutoka mbinguni ulitamka hukumu, nayo nchi ikaogopa, ikawa kimya:
9 als Gott sich erhob zum Gerichtsvollzug, um allen Bedrückten auf Erden zu helfen. (SELA)
wakati wewe, Ee Mungu, ulipoinuka kuhukumu, kuwaokoa wote walioonewa katika nchi.
10 Denn der Menschen Grimm wird dir zum Lobpreis, wenn zuletzt du dich gürtest mit Zornesflammen.
Hakika ghadhabu yako dhidi ya wanadamu inakuletea sifa, na masalia ya ghadhabu yako unajifunga mshipi.
11 Bringt Gelübde dar und erfüllt sie dem HERRN, eurem Gott: alle, die ihn rings umgeben, müssen Geschenke dem Schrecklichen bringen,
Wekeni nadhiri kwa Bwana Mungu wenu na kuzitimiza; nchi zote za jirani na walete zawadi kwa Yule astahiliye kuogopwa.
12 ihm, der den Hochmut der Fürsten dämpft und furchtbar ist den Königen der Erde.
Huvunja roho za watawala; anaogopwa na wafalme wa dunia.