< Psalm 72 >

1 Von Salomo. Gott, dein richterlich Walten verleihe dem König
Mpe mfalme amri ya haki yako, Mungu, haki yako kwa wana wa mfalme.
2 daß er dein Volk mit Gerechtigkeit richte und deine Elenden nach dem Recht!
Naye awaamue watu wako kwa haki na maskini wako kwa haki sawa.
3 Laß die Berge dem Volke Frieden tragen und die Hügel sich kleiden in Gerechtigkeit!
Milima iwazalie watu amani; vilima navyo vizae haki.
4 Er schaffe Recht den Elenden im Volk, er helfe den armen Leuten und zertrete den Bedrücker.
Naye awahukumu watu maskini; awaokoe watoto wa wahitaji na kuwavunja vipande vipande wenye kuwatesa.
5 Möge er leben, solange die Sonne scheint und der Mond (uns leuchtet), von Geschlecht zu Geschlecht!
Na wakuheshimu wewe wakati wa jua, na kwa kipindi cha kudumu kwa mwezi katika vizazi vyote.
6 Er möge sein wie Regen für frischgemähte Wiesen, wie Regenschauer, die das Land besprengen!
Naye apate kuja kama mvua juu ya nyasi zilizokatwa, kama manyuyu yanyunyizayo nchi.
7 In seinen Tagen möge der Gerechte blühen und Friede in Fülle bestehn, bis kein Mond mehr scheint.
Mwenye haki na astawi kwa wakati wake, na amani iwepo kwa wingi mpaka mwezi utakapotoweka.
8 Er herrsche von Meer zu Meer und vom Euphratstrom bis hin an die Enden der Erde!
Na awe na mamlaka toka bahari na bahari, na kutoka Mto hadi miisho ya dunia.
9 Vor ihm müssen die Steppenvölker die Knie beugen und seine Feinde den Staub lecken;
Na wote waishio jangwani wainame mbele zake; adui zake na walambe mavumbi.
10 die Könige von Tharsis und den Meeresländern müssen Geschenke ihm bringen, die Herrscher von Saba und Seba Abgaben entrichten;
Wafalme wa Tashishi na visiwa walete kodi; wafalme wa Sheba na Seba watoe zawadi.
11 ja huldigen müssen ihm alle Könige, die Völker alle ihm dienen!
Hakika wafalme wote wamwinamie yeye; mataifa yote yamtumikie yeye.
12 Denn er wird den Armen retten, der um Hilfe schreit, den Leidenden und den, der keinen Helfer hat.
Kwa kuwa yeye humsaidia mhitaji na maskini asiye na msaidizi.
13 Er wird sich erbarmen des Schwachen und Armen und Hilfe gewähren den Seelen der Armen;
Yeye huwahurumia maskini na wahitaji, na huokoa maisha ya wahitaji.
14 aus Bedrückung und Gewalttat wird er ihre Seelen erlösen, und ihr Blut wird kostbar sein in seinen Augen.
Huyaokoa maisha yao dhidi ya mateso na vurugu, na damu yao ni ya thamani machoni pake.
15 So lebe er denn, und man gebe ihm vom Golde aus Saba, man bete immerdar für ihn und segne ihn allezeit!
Naye apate kuishi! Na dhahabu za Sheba apewe yeye. Watu wamuombee yeye siku zote; Mungu ambariki daima.
16 Fülle von Korn möge sein im Lande bis auf die Gipfel der Berge, es rausche seine Frucht wie der Libanon! Und aus den Städten blühe das Volk hervor so zahlreich wie das Gras der Erde!
Kuwepo na nafaka nyingi katika ardhi; juu ya milima kuwe na mawimbi ya mimea. Matunda yake yawe kama Lebanoni; watu wasitawi katika miji kama nyansi za kondeni.
17 Sein Name möge ewig bestehn: solange die Sonne scheint, lebe sein Name fort, so daß man in ihm sich Segen wünscht und alle Völker ihn glücklich preisen!
Jina lake lidumu milele; jina lake ilindelee kama vile jua ling'aavyo; watu wabarikiwe katika yeye; mataifa yote wamwite mbarikiwa.
18 Gepriesen sei Gott der HERR, der Gott Israels, der Wunder vollbringt, er allein!
Yahwe Mungu, Mungu wa Israel, atukuzwe, ambaye pekee hufanya mambo ya ajabu.
19 Und gepriesen sei sein herrlicher Name in Ewigkeit, und die ganze Erde sei seiner Herrlichkeit voll! Amen, ja Amen! –
Jina lake tukufu litukuzawe milele, nayo nchi yote ijazwe na utukufu wake. Amina, Amina.
20 Zu Ende sind die Gebete Davids, des Sohnes Isais.
Maombi ya Daudi mwana wa Yese yamemalizika. Kutatu cha tatu

< Psalm 72 >