< Psalm 63 >
1 Ein Psalm Davids, als er in der Wüste Juda war. O Gott, du bist mein Gott: dich suche ich,
Mungu, wewe ni Mungu wangu! Ninakutafuta wewe kwa bidii, moyo wangu unakiu yako, mwili wangu unakutamani sana wewe, katika ukame na nchi iliyochoka mahali ambapo hakuna maji.
2 So hab’ ich nach dir im Heiligtum ausgeschaut, um deine Macht und Herrlichkeit zu erblicken;
Hivyo nimekutafuta wewe katika watu watakatifu kuona nguvu zako na utukufu wako.
3 denn deine Gnade ist besser als das Leben: meine Lippen sollen dich rühmen.
Kwa sababu uaminifu wa agano lako ni bora kuliko uhai, midomo yangu itakusifu wewe.
4 So will ich dich preisen mein Leben lang, in deinem Namen meine Hände erheben.
Hivyo nitakutukuza wewe niwapo hai; kwa jina lako nitainua mikono yangu juu.
5 Wie an Mark und Fett ersättigt sich meine Seele, und mit jubelnden Lippen lobpreist mein Mund,
Itakuwa kana kwamba nilikula mlo wa mafuta na wenye kunona, kwa midomo ya furaha kinywa changu kitakusifu wewe,
6 so oft ich deiner gedenke auf meinem Lager, in den Stunden der Nacht über dich sinne;
nikufikiripo kitandani mwangu na kukutafakari wewe wakati wa saa za usiku.
7 denn du bist mir ein Helfer gewesen, und im Schatten deiner Flügel darf ich jubeln.
Kwa maana umekuwa msaada wangu, na katika uvuli wa mbawa zako ninafurahia.
8 Meine Seele klammert sich an dich, aufrecht hält mich deine rechte Hand.
Ninashikamana nawe; mkono wako wa kuume unanisaidia.
9 Doch sie, die nach dem Leben mir trachten, mich zu verderben, sie werden in der Erde unterste Tiefen fahren.
Lakini wale watafutao kuuharibu uhai wangu wataenda chini kwenye sehemu ya chini kabisa ya nchi;
10 Man wird sie der Schärfe des Schwerts überliefern; die Beute der Schakale werden sie sein.
watakabidhiwa kwa wale ambao mikono yao hutumia upanga, nao watakuwa chakula cha mbweha.
11 Der König dagegen wird Gottes sich freuen: Ruhm wird ernten ein jeder, der bei ihm schwört; den Lügnern dagegen wird der Mund gestopft werden.
Bali mfalme atashangilia katika Mungu; yeyote anaye apa kupitia yeye atajivunia yeye, lakini vinywa ya wale wasemao uongo watanyamazishwa.