< Psalm 50 >
1 Ein Psalm von Asaph. Der Gott der Götter, der HERR, redet und ruft der Erde zu
Zaburi ya Asafu. Mwenye Nguvu, Mungu, Bwana, asema na kuiita dunia, tangu mawio ya jua hadi mahali pake liendapo kutua.
2 aus Zion, der Krone der Schönheit, strahlt Gott in lichtem Glanz hervor:
Kutoka Sayuni, penye uzuri mkamilifu, Mungu anaangaza.
3 unser Gott kommt und kann nicht schweigen, verzehrendes Feuer geht vor ihm her, und rings um ihn her stürmt es gewaltig.
Mungu wetu anakuja na hatakaa kimya, moto uteketezao unamtangulia, akiwa amezungukwa na tufani kali.
4 Er ruft dem Himmel droben zu und der Erde, um sein Volk zu richten:
Anaziita mbingu zilizo juu, na nchi, ili aweze kuwahukumu watu wake:
5 »Versammelt mir meine Gesetzestreuen, die den Bund mit mir geschlossen beim Opfer!«
“Nikusanyieni watu wangu waliowekwa wakfu, waliofanya agano nami kwa dhabihu.”
6 Da taten die Himmel seine Gerechtigkeit kund; denn Gott selbst ist’s, der da Gericht hält. (SELA)
Nazo mbingu zinatangaza haki yake, kwa maana Mungu mwenyewe ni hakimu.
7 »Höre, mein Volk, und laß mich reden, Israel, daß ich dich ernstlich warne: Gott, dein Gott bin ich!
“Sikieni, enyi watu wangu, nami nitasema, ee Israeli, nami nitashuhudia dhidi yenu: Mimi ndimi Mungu, Mungu wenu.
8 Nicht deiner Opfer wegen rüge ich dich, sind doch deine Brandopfer stets mir vor Augen.
Sikukemei kwa sababu ya dhabihu zako, au sadaka zako za kuteketezwa, ambazo daima ziko mbele zangu.
9 Doch ich mag nicht Stiere nehmen aus deinem Hause, nicht Böcke aus deinen Hürden;
Sina haja ya fahali wa banda lako, au mbuzi wa zizi lako.
10 denn mein ist alles Wild des Waldes, das Getier auf meinen Bergen zu Tausenden.
Kwa maana kila mnyama wa msituni ni wangu, na pia makundi ya mifugo juu ya vilima elfu.
11 Ich kenne jeden Vogel auf den Bergen, und was auf dem Felde sich regt, steht mir zur Verfügung.
Ninamjua kila ndege mlimani, nao viumbe wa kondeni ni wangu.
12 Hätte ich Hunger: ich brauchte es dir nicht zu sagen, denn mein ist der Erdkreis und all seine Fülle.
Kama ningekuwa na njaa, nisingewaambia ninyi, kwa maana ulimwengu ni wangu, pamoja na vyote vilivyomo ndani yake.
13 Esse ich etwa das Fleisch von Stieren, und soll ich das Blut von Böcken trinken?
Je, mimi hula nyama ya mafahali au kunywa damu ya mbuzi?
14 Bringe Dank dem HERRN als Opfer dar und bezahle so dem Höchsten deine Gelübde,
Toa sadaka za shukrani kwa Mungu, timiza nadhiri zako kwake Yeye Aliye Juu Sana,
15 und rufe mich an am Tage der Not, so will ich dich retten, und du sollst mich preisen!«
na uniite siku ya taabu; nami nitakuokoa, nawe utanitukuza.”
16 Zum Gottlosen aber spricht der Allherr: »Was hast du meine Satzungen aufzuzählen und meinen Bund im Munde zu führen,
Lakini kwake mtu mwovu, Mungu asema: “Una haki gani kunena sheria zangu au kuchukua agano langu midomoni mwako?
17 da du selbst doch die Zucht mißachtest und meinen Worten den Rücken kehrst?
Unachukia mafundisho yangu na kuyatupa maneno yangu nyuma yako.
18 Siehst du einen Dieb, so befreundest du dich mit ihm, und mit Ehebrechern hast du Gemeinschaft;
Unapomwona mwizi, unaungana naye, unapiga kura yako pamoja na wazinzi.
19 deinem Munde läßt du freien Lauf zur Bosheit, und deine Zunge zettelt Betrug an;
Unakitumia kinywa chako kwa mabaya na kuuongoza ulimi wako kwa hila.
20 du sitzest da und redest (Böses) gegen deinen Bruder und bringst den Sohn deiner Mutter in Verruf!
Wanena daima dhidi ya ndugu yako na kumsingizia mwana wa mama yako.
21 Das (alles) hast du getan, und ich habe geschwiegen; da hast du gedacht, ich sei so wie du. Das mache ich dir zum Vorwurf und gebe dir’s zu bedenken.
Mambo haya unayafanya, nami nimekaa kimya, ukafikiri Mimi nami ni kama wewe. Lakini nitakukemea na kuweka mashtaka mbele yako.
22 O beherzigt das wohl, ihr Gottvergeßnen: sonst raffe ich euch hinweg ohne Rettung!
“Yatafakarini haya, ninyi mnaomsahau Mungu, ama sivyo nitawararua vipande vipande, wala hapatakuwepo na yeyote wa kuwaokoa:
23 Wer Dank als Opfer darbringt, erweist mir Ehre, und wer unsträflich wandelt, den lasse ich schauen Gottes Heil.«
Atoaye dhabihu za shukrani ananiheshimu mimi, naye aiandaa njia yake ili nimwonyeshe wokovu wa Mungu.”