< Psalm 48 >
1 Ein Lied, ein Psalm von den Korahiten. Groß ist der HERR und hoch zu preisen
Yahwe ndiye aliye mkuu na mwenyekusifiwa sana, katika mji wa Mungu wetu kwenye mlima wake mtakatifu.
2 Herrlich ragt empor, die Wonne der ganzen Erde, der Zionsberg, der wahre Götterberg, die Stadt eines großen Königs.
Ni mzuri katika mwinuko wake, furaha ya nchi yote, ni mlima Sayuni, kwenye upande wa kaskazini, mji wa Mfalme mkuu.
3 Gott hat in ihren Palästen sich kundgetan als eine feste Burg.
Mungu amejifunua mwenyewe katika jumba lake la kifahari kama kimbilio la usalama.
4 Denn siehe, die Könige hatten sich versammelt, waren vereint herangezogen;
Maana, tazama, wafalme walikusanyika wenyewe; wote pamoja walipita.
5 doch als sie’s sahen, waren sie betroffen, erschraken, flohen bestürzt davon;
Nao waliuona, wakashangaa; walifadhaika, na wakaharakisha kuondoka.
6 Zittern erfaßte sie dort, Angst wie ein Weib in Wehen.
Pale pale tetemeko liliwashikilia, maumivu makali kama mwanamke anaye zaa.
7 Durch einen Oststurm zertrümmertest du die stolzen Tharsisschiffe.
Kwa upepo wa mashariki wewe huivunja meli ya Tarshishi.
8 Wie wir’s gehört, so haben wir’s nun gesehen in der Stadt des HERRN der Heerscharen, unsres Gottes Stadt: Gott läßt sie auf ewig feststehn. (SELA)
Kama tulivyo sikia, vivyo hivyo tumeona katika mji wa Yahwe wa majeshi, katika mji wa Mungu wetu; Mungu atautunza milele. (Selah)
9 Wir gedenken, o Gott, deiner Gnade inmitten deines Tempels.
Tumeutafakari uaminifu wa agano lako, Mungu, katikati ya hekalu lako.
10 Wie dein Name, o Gott, so reicht auch dein Ruhm bis an die Enden der Erde; mit Gerechtigkeit ist deine Rechte gefüllt.
Kama lilivyo jina lako, Mungu, hivyo ndivyo zilivyo sifa zako mpaka miisho ya dunia; mkono wako wa kuume umejaa haki.
11 Des freue sich der Zionsberg, jubeln mögen die Töchter Judas um deiner Gerichte willen!
Milma Sayuni na ufurahi, nao wana wa Yuda washangilie kwa sababu ya amri ya haki yako.
12 Umkreist den Zion, umwandelt ihn rings und zählt seine Türme;
Tembeeni katika Mlima Sayuni, muuzungukie mji,
13 betrachtet genau seine Bollwerke, mustert seine Paläste, damit ihr dem künftgen Geschlecht erzählet,
mzitazame kwa makini nguzo zake, na mtazame majumba yake ya kifahari ili kwamba muweze kuwasimulia kizazi kijacho.
14 daß dies ist Gott, unser Gott: immer und ewig wird er uns führen [bis zum Tode].
Kwa kuwa huyu Mungu ni Mungu wetu milele na milele; naye atakuwa kiongozi wetu mpaka kufa.