< Psalm 34 >

1 Von David, als er sich vor Abimelech irrsinnig stellte und dieser ihn von sich trieb, so daß er von dannen ging. Ich will den HERRN allzeit preisen,
Nitamsifu Yahwe wakati wote, siku zote sifa zake zitakuwa mdomoni mwangu.
2 Des HERRN soll meine Seele sich rühmen, die Demütigen sollen es hören und sich freuen.
Nitamsifu Yahwe! walio onewa wasikie na kufurahi.
3 Verherrlicht mit mir den HERRN und laßt uns gemeinsam seinen Namen erheben!
Msifuni Yahwe pamoja nami, kwa pamoja tuliinue jina lake.
4 Sooft den HERRN ich suchte, hat er mich erhört und aus allen meinen Ängsten mich befreit.
Nilimuomba Yahwe msaada naye akanijibu, akanipa ushindi juu ya hofu yangu yote.
5 Wer auf ihn blickt, wird heiteren Sinnes, und sein Antlitz braucht nicht beschämt zu erröten.
Wale wanao mtazama yeye wana furaha, na nyuso zao hazina aibu.
6 Hier ist ein (solcher) Dulder, der rief: da hörte der HERR und half ihm aus all seinen Nöten.
Huyu mtu aliye onewa alilia na Yahwe akamsikia na kumuokoa kwenye matatizo yake yote.
7 Der Engel des HERRN lagert sich rings um die Gottesfürchtigen und rettet sie.
Malaika wa Yahwe huweka kambi wakiwazunguka wale wanao muogopa yeye na kuwaokoa.
8 Schmecket und sehet, wie freundlich der HERR ist: wohl dem Manne, der auf ihn vertraut!
Onjeni muone Yahwe ni mzuri. Amebarikiwa mtu yule ambaye Yahwe ni kimbilio lake.
9 Fürchtet den HERRN, ihr seine Heiligen! denn die ihn fürchten, leiden keinen Mangel.
Muogopeni Yahwe, ninyi watu watakatifu wake. Hakuna kupungukikwa kwa wale wanao mhofu yeye.
10 Junge Löwen müssen darben und leiden Hunger; doch wer den HERRN sucht, entbehrt nichts Gutes.
Simba wadogo wakati mwingine hukosa chakula na kuteseka kwa njaa, bali wale wamtafutao Yahwe hawatapungukiwa chochote kilicho kizuri.
11 Kommt her, ihr Kinder, hört mir zu: die Furcht des HERRN will ich euch lehren!
Njoni, wana, mnisikilize mimi. nitawafundisha ninyi hofu ya Yahwe.
12 Wer ist der Mann, der langes Leben begehrt, der viele Tage sich wünscht, um Glück zu genießen?
Mtu nani aliyepo ambaye anatamani maisha na anapenda kuwa na siku nyingi, ili kwamba aweze kuona vizuri?
13 Hüte deine Zunge vor Bösem und deine Lippen vor Worten des Trugs!
Hivyo uepushe ulimi wako na uovu na uilinde midomo yako kuongea uongo.
14 Halte dich fern vom Bösen und tu das Gute, suche den Frieden und jage ihm nach!
Uache uovu na utende mema. Uitafute amani na kuiendea amani.
15 Die Augen des HERRN sind auf die Gerechten gerichtet und seine Ohren auf ihr Hilfsgeschrei.
Macho ya Yahwe yako kwenye haki na masikio yake huelekea kulia kwao.
16 Das Antlitz des HERRN steht gegen die Frevler, um ihr Gedächtnis auszutilgen von der Erde.
Uso wa Yahwe uko kinyume na wale watendao uovu, kuikatilia mbali kumbukumbu yao duniani.
17 Wenn sie schreien, so hört es der HERR und rettet sie aus all ihren Nöten.
Wenye haki hulia na Yahwe husikia na kuwaokoa kwenye matatizo yao yote.
18 Der HERR ist nahe den zerbrochenen Herzen, hilft denen, die zerschlagenen Geistes sind.
Yahwe yu karibu nao waliovunjika moyo, naye huwaokoa waliogandamizwa rohoni.
19 Zahlreich sind die Leiden des Gerechten, doch aus allen rettet ihn der HERR.
Mateso ya wenye haki ni mengi, bali Yahwe huwaokoa nayo yote.
20 Er behütet alle seine Gebeine, daß nicht eins von ihnen zerbrochen wird.
Yeye huitunza mifupa yake yote, hakuna hata mmoja wao utavunjika.
21 Den Gottlosen wird das Unglück töten, und wer den Gerechten haßt, muß es büßen.
Uovu utawauwa waovu. Wale wachukiao haki watahukumiwa.
22 Der HERR erlöst die Seele seiner Knechte, und alle, die zu ihm sich flüchten, brauchen nicht zu büßen.
Yahwe huokoa maisha ya watumishi wake. Hakuna atakaye hukumiwa hata mmoja atafutaye usalama katika yeye.

< Psalm 34 >