< Psalm 2 >
1 Was soll das Toben der Völker und das eitle Sinnen der Völkerschaften?
Kwa nini mataifa wanashauriana kufanya mabaya, na kabila za watu kula njama bure?
2 Die Könige der Erde rotten sich zusammen, und die Fürsten halten Rat miteinander gegen den HERRN und den von ihm Gesalbten:
Wafalme wa dunia wanajipanga na watawala wanajikusanya pamoja dhidi ya Bwana na dhidi ya Mpakwa Mafuta wake.
3 »Laßt uns zerreißen ihre Bande und von uns werfen ihre Fesseln!«
Wanasema, “Tuvunje minyororo yao na kuvitupilia mbali vifungo vyao.”
4 Der im Himmel thront, der lacht, der Allherr spottet ihrer.
Yeye atawalaye mbinguni hucheka, Bwana huwadharau.
5 Dann aber wird er zu ihnen reden in seinem Zorn und sie schrecken in seinem Ingrimm:
Kisha huwakemea katika hasira yake na kuwaogopesha katika ghadhabu yake, akisema,
6 »Habe ich doch meinen König eingesetzt auf dem Zion, meinem heiligen Berge!« –
“Nimemtawaza Mfalme wangu juu ya Sayuni, mlima wangu mtakatifu.”
7 Laßt mich kundtun den Ratschluß des HERRN! Er hat zu mir gesagt: »Mein Sohn bist du; ich selbst habe heute dich gezeugt.
Nitatangaza amri ya Bwana: Yeye aliniambia, “Wewe ni Mwanangu, leo mimi nimekuzaa.
8 Fordre von mir, so gebe ich dir die Völker zum Erbe und dir zum Besitz die Enden der Erde.
Niombe, nami nitayafanya mataifa kuwa urithi wako, miisho ya dunia kuwa milki yako.
9 Du sollst sie mit eiserner Keule zerschmettern, wie Töpfergeschirr sie zerschlagen!« –
Utawatawala kwa fimbo ya chuma na kuwavunjavunja kama chombo cha mfinyanzi.”
10 So nehmt denn Klugheit an, ihr Könige, laßt euch warnen, ihr Richter der Erde!
Kwa hiyo, ninyi wafalme, kuweni na hekima; mwonyeke, enyi watawala wa dunia.
11 Dienet dem HERRN mit Furcht und jubelt ihm zu mit Zittern!
Mtumikieni Bwana kwa hofu na mshangilie kwa kutetemeka.
12 Küsset den Sohn, auf daß er nicht zürne und ihr zugrunde geht auf eurem Wege! denn leicht entbrennt sein Zorn. Wohl allen, die bei ihm sich bergen!
Mbusu Mwana, asije akakasirika nawe ukaangamizwa katika njia yako, kwa maana hasira yake inaweza kuwaka ghafula. Heri wote wanaomkimbilia.