< Psalm 113 >

1 Halleluja! Lobet, ihr Knechte des HERRN, lobet den Namen des HERRN!
Msifuni Bwana. Enyi watumishi wa Bwana msifuni, lisifuni jina la Bwana.
2 Gepriesen sei der Name des HERRN von nun an bis in Ewigkeit!
Jina la Bwana na lisifiwe, sasa na hata milele.
3 Vom Aufgang der Sonne bis zu ihrem Niedergang sei gelobt der Name des HERRN!
Kuanzia mawio ya jua hadi machweo yake, jina la Bwana linapaswa kusifiwa.
4 Erhaben über alle Völker ist der HERR, den Himmel überragt seine Herrlichkeit!
Bwana ametukuka juu ya mataifa yote, utukufu wake juu ya mbingu.
5 Wer ist dem HERRN gleich, unserm Gott, der da thront in der Höhe,
Ni nani aliye kama Bwana Mungu wetu, Yeye ambaye ameketi juu kwenye kiti cha enzi,
6 der niederschaut in die Tiefe, im Himmel und auf Erden?
ambaye huinama atazame chini aone mbingu na nchi?
7 Er hebt aus dem Staub den Geringen empor und erhöht aus dem Schmutz den Armen,
Huwainua maskini kutoka mavumbini, na kuwanyanyua wahitaji kutoka kwenye jalala,
8 um ihn sitzen zu lassen neben Edlen, neben den Edlen seines Volks.
huwaketisha pamoja na wakuu, pamoja na wakuu wa watu wake.
9 Er verleiht der kinderlosen Gattin Hausrecht, macht sie zur fröhlichen Mutter von Kindern. Halleluja!
Humjalia mwanamke tasa kutulia nyumbani mwake, akiwa mama watoto mwenye furaha. Msifuni Bwana.

< Psalm 113 >