< Psalm 110 >

1 Von David, ein Psalm. So lautet der Ausspruch des HERRN an meinen Herrn:
Yahwe humwambia bwana wangu, “Kaa mkono wangu wa kuume mpaka nitakapowaweka adui zako chini ya miguu yako.”
2 Dein machtvolles Zepter wird der HERR von Zion hinausstrecken: herrsche inmitten deiner Feinde!
Yahwe atainyosha fimbo ya nguvu yako toka Sayuni; utawale kati ya adui zako.
3 Dein Volk wird voller Willigkeit sein am Tage deines Heereszuges; in heiligem Schmuck, wie aus des Frührots Schoß der Tau, wird dir kommen deine junge Mannschaft.
Siku ile ya uweza wako watu wako watakufuata wakiwa katika mavazi matakatifu ya hiari yao wenyewe; tokea tumbo la alfajiri ujana wako utakuwa kwako kama umande.
4 Geschworen hat der HERR und wird sich’s nicht leid sein lassen: »Du sollst ein Priester in Ewigkeit sein nach der Weise Melchisedeks.«
Yahwe ameapa, na hatabadilika: “Wewe ni kuhani milele, baada ya namna ya Melkizedeki.”
5 Der Allherr, der dir zur Rechten steht, wird Könige zerschmettern am Tage seines Zorns;
Bwana yuko mkono wako wa kuume. Siku ile ya hasira yake atawaua wafalme.
6 Gericht wird er unter den Völkern halten, füllt alles mit Leichen an, zerschmettert ein Haupt auf weitem Gefilde.
Yeye atahukumu matifa; ataujaza uwanja wa vita kwa maiti; atawauwa viongozi kaitka nchi nyingi.
7 Aus dem Bach am Wege wird er trinken; darum wird er das Haupt hoch halten.
Atakunywa maji ya kijito njiani, kisha baada ya ushindi atainua kichwa chake juu.

< Psalm 110 >