< Psalm 107 >
1 »Danket dem HERRN, denn er ist freundlich, ja, ewiglich währt seine Gnade«:
Mshukuruni Bwana, kwa kuwa yeye ni mwema, upendo wake wadumu milele.
2 so sollen die vom HERRN Erlösten sprechen, die er befreit hat aus Drangsal
Waliokombolewa wa Bwana na waseme hivi, wale aliowaokoa kutoka mkono wa adui,
3 und die er gesammelt aus den Ländern vom Aufgang her und vom Niedergang, vom Norden her und vom Meer.
wale aliowakusanya kutoka nchi mbalimbali, kutoka mashariki na magharibi, kutoka kaskazini na kusini.
4 Sie irrten umher in der Wüste, der Öde, und fanden den Weg nicht zu einer Wohnstatt;
Baadhi yao walitangatanga jangwani, hawakuona njia ya kuwafikisha mji ambao wangeweza kuishi.
5 gequält vom Hunger und vom Durst, wollte ihre Seele in ihnen verschmachten.
Walikuwa na njaa na kiu, nafsi zao zikadhoofika.
6 Da schrien sie zum HERRN in ihrer Not, und er rettete sie aus ihren Ängsten
Ndipo walipomlilia Bwana katika shida yao, naye akawaokoa kutoka taabu yao.
7 und leitete sie auf richtigem Wege, daß sie kamen zu einer bewohnten Ortschaft: –
Akawaongoza kwa njia iliyo sawa hadi mji ambao wangeweza kuishi.
8 die mögen danken dem HERRN für seine Güte und für seine Wundertaten an den Menschenkindern,
Basi na wamshukuru Bwana kwa upendo wake usiokoma, na kwa matendo yake ya ajabu kwa wanadamu,
9 daß er die lechzende Seele gesättigt und die hungernde Seele gefüllt hat mit Labung.
kwa maana yeye humtosheleza mwenye kiu, na kumshibisha mwenye njaa kwa vitu vyema.
10 Die da saßen in Finsternis und Todesnacht, gefangen in Elend und Eisenbanden –
Wengine walikaa gizani na katika huzuni kuu, wafungwa wakiteseka katika minyororo,
11 denn sie hatten Gottes Geboten getrotzt und den Ratschluß des Höchsten verachtet,
kwa sababu walikuwa wameasi dhidi ya maneno ya Mungu na kudharau shauri la Aliye Juu Sana.
12 so daß er ihren Sinn durch Leiden beugte, daß sie niedersanken und keinen Helfer hatten –;
Aliwatumikisha kwa kazi ngumu; walijikwaa na hapakuwepo yeyote wa kuwasaidia.
13 da schrien sie zum HERRN in ihrer Not, und er rettete sie aus ihren Ängsten;
Ndipo walipomlilia Bwana katika shida yao, naye akawaokoa kutoka taabu yao.
14 er führte sie heraus aus Finsternis und Todesnacht und zersprengte ihre Fesseln: –
Akawatoa katika giza na huzuni kuu na akavunja minyororo yao.
15 die mögen danken dem HERRN für seine Güte und für seine Wundertaten an den Menschenkindern,
Basi na wamshukuru Bwana kwa upendo wake usiokoma, na kwa matendo yake ya ajabu kwa wanadamu,
16 daß er eherne Türen zerbrochen und eiserne Riegel zerschlagen.
kwa kuwa yeye huvunja malango ya shaba na kukata mapingo ya chuma.
17 Die da krank waren infolge ihres Sündenlebens und wegen ihrer Verfehlungen leiden mußten –
Wengine wakawa wapumbavu kutokana na uasi wao, wakapata mateso kwa sababu ya uovu wao.
18 vor jeglicher Speise hatten sie Widerwillen, so daß sie den Pforten des Todes nahe waren –;
Wakachukia kabisa vyakula vyote, wakakaribia malango ya mauti.
19 da schrien sie zum HERRN in ihrer Not, und er rettete sie aus ihren Ängsten;
Ndipo walipomlilia Bwana katika shida yao, naye akawaokoa kutoka taabu yao.
20 er sandte sein Wort, sie gesund zu machen, und ließ sie aus ihren Gruben entrinnen: –
Akalituma neno lake na kuwaponya, akawaokoa kutoka maangamizo yao.
21 die mögen danken dem HERRN für seine Güte und für seine Wundertaten an den Menschenkindern;
Basi na wamshukuru Bwana kwa upendo wake usiokoma, na kwa matendo yake ya ajabu kwa wanadamu.
22 sie mögen Opfer des Dankes bringen und seine Taten mit Jubel verkünden!
Na watoe dhabihu za kushukuru, na wasimulie matendo yake kwa nyimbo za furaha.
23 Die aufs Meer gefahren waren in Schiffen, auf weiten Fluten Handelsgeschäfte trieben,
Wengine walisafiri baharini kwa meli, walikuwa wafanyabiashara kwenye maji makuu.
24 die haben das Walten des HERRN geschaut und seine Wundertaten auf hoher See.
Waliziona kazi za Bwana, matendo yake ya ajabu kilindini.
25 Denn er gebot und ließ einen Sturm entstehn, der hoch die Wogen des Meeres türmte:
Kwa maana alisema na kuamsha tufani iliyoinua mawimbi juu.
26 sie stiegen empor zum Himmel und fuhren hinab in die Tiefen, so daß ihr Herz vor Angst verzagte;
Yakainuka juu mbinguni, yakashuka chini hadi vilindini, katika hatari hii ujasiri wao uliyeyuka.
27 sie wurden schwindlig und schwankten wie Trunkne, und mit all ihrer Weisheit war’s zu Ende: –
Walipepesuka na kuyumbayumba kama walevi, ujanja wao ukafikia ukomo.
28 da schrien sie zum HERRN in ihrer Not, und er befreite sie aus ihren Ängsten;
Ndipo walipomlilia Bwana katika shida yao, naye akawatoa kwenye taabu yao.
29 er stillte das Ungewitter zum Säuseln, und das Toben der Wogen verstummte;
Akatuliza dhoruba kwa mnongʼono, mawimbi ya bahari yakatulia.
30 da wurden sie froh, daß es still geworden, und er führte sie zum ersehnten Hafen: –
Walifurahi ilipokuwa shwari, naye akawaongoza hadi bandari waliyoitamani.
31 die mögen danken dem HERRN für seine Güte und für seine Wundertaten an den Menschenkindern;
Basi na wamshukuru Bwana kwa upendo wake usiokoma, na kwa matendo yake ya ajabu kwa wanadamu.
32 sie mögen ihn erheben in der Volksgemeinde und im Kreise der Alten ihn preisen!
Na wamtukuze yeye katika kusanyiko la watu, na wamsifu katika baraza la wazee.
33 Er wandelte Ströme zur Wüste und Wasserquellen zu dürrem Land,
Yeye aligeuza mito kuwa jangwa, chemchemi za maji zitiririkazo kuwa ardhi yenye kiu,
34 fruchtbares Erdreich zu salziger Steppe wegen der Bosheit seiner Bewohner.
nchi izaayo ikawa ya chumvi isiyofaa, kwa sababu ya uovu wa wale walioishi humo.
35 Wiederum machte er wüstes Land zum Wasserteich und dürres Gebiet zu Wasserquellen
Aligeuza jangwa likawa madimbwi ya maji, nayo ardhi kame kuwa chemchemi za maji zitiririkazo;
36 und ließ dort Hungrige seßhaft werden, so daß sie eine Stadt zum Wohnsitz bauten
aliwaleta wenye njaa wakaishi humo, nao wakajenga mji wangeweza kuishi.
37 und Felder besäten und Weinberge pflanzten, die reichen Ertrag an Früchten brachten;
Walilima mashamba na kupanda mizabibu, nayo ikazaa matunda mengi,
38 und er segnete sie, daß sie stark sich mehrten, und ließ ihres Viehs nicht wenig sein.
Mungu aliwabariki, hesabu yao ikaongezeka sana, wala hakuruhusu mifugo yao kupungua.
39 Dann aber nahmen sie ab und wurden gebeugt durch den Druck des Unglücks und Kummers;
Kisha hesabu yao ilipungua, na walinyenyekeshwa kwa kuonewa, maafa na huzuni.
40 »über Edle goß er Verachtung aus und ließ sie irren in pfadloser Öde«.
Yeye ambaye huwamwagia dharau wakuu, aliwafanya watangetange nyikani isiyo na njia.
41 Den Armen aber hob er empor aus dem Elend und machte seine Geschlechter wie Kleinviehherden.
Lakini yeye aliwainua wahitaji katika taabu zao, na kuongeza jamaa zao kama makundi ya kondoo.
42 »Die Gerechten sehen’s und freuen sich, alle Bosheit aber muß schließen ihren Mund«.
Wanyofu wataona na kufurahi, lakini waovu wote watafunga vinywa vyao.
43 Wer ist weise? Der beachte dies und lerne die Gnadenerweise des HERRN verstehn!
Yeyote aliye na hekima, ayasikie mambo haya, na atafakari upendo mkuu wa Bwana.