< Psalm 106 >
1 Halleluja! Preiset den HERRN, denn er ist freundlich, ja ewiglich währt seine Gnade!
Msifuni Bwana. Mshukuruni Bwana, kwa kuwa ni mwema; upendo wake wadumu milele.
2 Wer kann des HERRN Machttaten gebührend preisen und kundtun all seinen Ruhm?
Ni nani awezaye kusimulia matendo makuu ya Bwana au kutangaza kikamilifu sifa zake?
3 Wohl denen, die am Recht festhalten, und dem, der Gerechtigkeit übt zu jeder Zeit!
Heri wale wanaodumisha haki, ambao daima wanafanya yaliyo mema.
4 Gedenke meiner, o HERR, mit der Liebe zu deinem Volk, nimm dich meiner an mit deiner Hilfe,
Ee Bwana, unikumbuke unapowatendea mema watu wako, uwe msaada wangu unapowaokoa,
5 daß ich schau’ meine Lust am Glück deiner Erwählten, an der Freude deines Volkes Anteil habe und glücklich mich preise mit deinem Eigentumsvolke!
ili niweze kufurahia mafanikio ya wateule wako, niweze kushiriki katika furaha ya taifa lako, na kuungana na urithi wako katika kukusifu.
6 Wir haben gesündigt gleich unsern Vätern, wir haben gefehlt und gottlos gehandelt.
Tumetenda dhambi, kama vile baba zetu walivyotenda, tumekosa na tumetenda uovu.
7 Unsre Väter in Ägypten achteten nicht auf deine Wunder, gedachten nicht der Fülle deiner Gnadenerweise, waren widerspenstig gegen den Höchsten schon am Schilfmeer;
Wakati baba zetu walipokuwa Misri, hawakuzingatia maajabu yako, wala hawakukumbuka wingi wa fadhili zako, bali waliasi kando ya bahari, Bahari ya Shamu.
8 dennoch half er ihnen um seines Namens willen, um seine Heldenkraft zu erweisen.
Hata hivyo aliwaokoa kwa ajili ya jina lake, ili apate kudhihirisha uweza wake mkuu.
9 Er schalt das Schilfmeer: da ward es trocken, und er ließ sie ziehn durch die Fluten wie über die Trift.
Alikemea Bahari ya Shamu, nayo ikakauka, akawaongoza katika vilindi vyake kama vile jangwani.
10 So rettete er sie aus der Hand des Verfolgers und erlöste sie aus der Gewalt des Feindes:
Aliwaokoa mikononi mwa adui; kutoka mikononi mwa adui aliwakomboa.
11 die Fluten bedeckten ihre Bedränger, nicht einer von ihnen blieb übrig.
Maji yaliwafunika adui zao, hakunusurika hata mmoja.
12 Da glaubten sie an seine Worte, besangen seinen Ruhm.
Ndipo walipoamini ahadi zake, nao wakaimba sifa zake.
13 Doch schnell vergaßen sie seine Taten und warteten seinen Ratschluß nicht ab;
Lakini mara walisahau aliyowatendea, wala hawakungojea shauri lake.
14 sie fröhnten ihrem Gelüst in der Wüste und versuchten Gott in der Einöde:
Jangwani walitawaliwa na tamaa zao, walimjaribu Mungu nyikani.
15 da gewährte er ihnen ihr Verlangen, sandte aber die Seuche gegen ihr Leben.
Kwa hiyo aliwapa kile walichoomba, lakini akatuma juu yao ugonjwa wa kudhoofisha.
16 Dann wurden sie eifersüchtig auf Mose im Lager, auf Aaron, den Geweihten des HERRN:
Kambini walimwonea wivu Mose, na pia Aroni aliyekuwa amewekwa wakfu kwa Bwana.
17 da tat die Erde sich auf und verschlang Dathan und begrub die ganze Rotte Abirams,
Ardhi ilifunguka ikawameza Dathani, ikawazika Abiramu na kundi lake.
18 Feuer verbrannte ihre Rotte, Flammen verzehrten die Frevler.
Moto uliwaka katikati ya wafuasi wao, mwali wa moto uliwateketeza waovu.
19 Sie machten sich ein Kalb am Horeb und warfen vor einem Gußbild sich nieder
Huko Horebu walitengeneza ndama, na kuabudu sanamu ya kusubu kwa chuma.
20 und vertauschten so die Herrlichkeit ihres Gottes mit dem Bildnis eines Stieres, der Gras frißt.
Waliubadilisha Utukufu wao kwa sanamu ya fahali, ambaye hula majani.
21 Sie hatten Gott, ihren Retter, vergessen, der große Dinge getan in Ägypten,
Walimsahau Mungu aliyewaokoa, aliyekuwa ametenda mambo makuu huko Misri,
22 Wunderzeichen im Lande Hams, furchtbare Taten am Schilfmeer.
miujiza katika nchi ya Hamu na mambo ya kutisha huko Bahari ya Shamu.
23 Da gedachte er sie zu vertilgen, wenn nicht Mose, sein Auserwählter, mit Fürbitte vor ihn hingetreten wäre, um seinen Grimm vom Vernichten abzuwenden.
Kwa hiyo alisema kwamba angewaangamiza: kama Mose mteule wake, asingesimama kati yao na Mungu kuizuia ghadhabu yake kuwaangamiza.
24 Sodann verschmähten sie das herrliche Land und schenkten seiner Verheißung keinen Glauben,
Kisha waliidharau ile nchi nzuri, hawakuiamini ahadi yake.
25 sondern murrten in ihren Zelten, gehorchten nicht der Weisung des HERRN.
Walinungʼunika ndani ya mahema yao, wala hawakumtii Bwana.
26 Da erhob er seine Hand gegen sie zum Schwur, sie in der Wüste niederzuschlagen,
Kwa hiyo akaapa kwa mkono ulioinuliwa kwamba atawafanya waanguke jangwani,
27 ihre Nachkommen unter die Heiden niederzuwerfen und sie rings zu zerstreuen in die Länder.
kuwatawanya wazao wao waanguke miongoni mwa mataifa, na kuwatawanya katika nchi zote.
28 Dann hängten sie sich an den Baal-Peor und aßen Opferfleisch der toten (Götzen)
Walijifunga nira na Baali wa Peori, wakala dhabihu zilizotolewa kwa miungu isiyo na uhai.
29 und erbitterten ihn durch ihr ganzes Tun. Als nun ein Sterben unter ihnen ausbrach,
Waliichochea hasira ya Bwana, wakamkasirisha kwa matendo yao maovu, nayo tauni ikazuka katikati yao.
30 trat Pinehas auf und hielt Gericht: da wurde dem Sterben Einhalt getan.
Lakini Finehasi alisimama na kuingilia kati, nayo tauni ikazuiliwa.
31 Das wurde ihm angerechnet zur Gerechtigkeit von Geschlecht zu Geschlecht in Ewigkeit. –
Hili likahesabiwa kwake haki, kwa vizazi visivyo na mwisho vijavyo.
32 Dann erregten sie Gottes Zorn am Haderwasser, und Mose erging es übel um ihretwillen;
Kwenye maji ya Meriba, walimkasirisha Bwana, janga likampata Mose kwa sababu yao;
33 denn weil sie dem Geiste Gottes widerstrebten, hatte er unbedacht mit seinen Lippen geredet.
kwa maana walimwasi Roho wa Mungu, na maneno yasiyofaa yakatoka midomoni kwa Mose.
34 Sie vertilgten auch die Völker nicht, von denen der HERR es ihnen geboten,
Hawakuyaangamiza yale mataifa kama Bwana alivyowaagiza,
35 sondern traten mit den Heiden in Verkehr und gewöhnten sich an deren (böses) Tun
bali walijichanganya na mataifa na wakazikubali desturi zao.
36 und dienten ihren Götzen: die wurden ihnen zum Fallstrick.
Waliabudu sanamu zao, zikawa mtego kwao.
37 Ja, sie opferten ihre Söhne und ihre Töchter den bösen Geistern
Wakawatoa wana wao na binti zao dhabihu kwa mashetani.
38 und vergossen unschuldig Blut [das Blut ihrer Söhne und Töchter, die sie den Götzen Kanaans opferten]: so wurde das Land durch Blutvergießen entweiht.
Walimwaga damu isiyo na hatia, damu za wana wao na binti zao, ambao waliwatoa dhabihu kwa sanamu za Kanaani, nayo nchi ikanajisika kwa damu zao.
39 Sie wurden unrein durch ihr Verhalten und verübten Abfall durch ihr Tun. –
Wakajinajisi wenyewe kwa yale waliyotenda; kwa matendo yao wenyewe wakajifanyia ukahaba.
40 Da entbrannte der Zorn des HERRN gegen sein Volk, und Abscheu fühlte er gegen sein Erbe;
Kwa hiyo Bwana akawakasirikia watu wake na akauchukia sana urithi wake.
41 er ließ sie in die Hand der Heiden fallen, so daß ihre Hasser über sie herrschten;
Akawakabidhi kwa mataifa na adui zao wakawatawala.
42 ihre Feinde bedrängten sie hart, so daß sie sich beugen mußten unter deren Hand.
Adui zao wakawaonea na kuwatia chini ya mamlaka yao.
43 Oftmals zwar befreite er sie, doch sie blieben widerspenstig gegen seinen Ratschluß und sanken immer tiefer durch ihre Schuld.
Mara nyingi aliwaokoa lakini walikuwa wamezama kwenye uasi, nao wakajiharibu katika dhambi zao.
44 Er aber nahm sich ihrer Drangsal an, sooft er ihr Wehgeschrei hörte,
Lakini akaangalia mateso yao wakati aliposikia kilio chao;
45 und gedachte seines Bundes ihnen zugut, fühlte Mitleid nach seiner großen Güte
kwa ajili yao akakumbuka agano lake, na kutokana na upendo wake mkuu akapooza hasira yake.
46 und ließ sie Erbarmen finden bei allen, die sie gefangen hielten.
Akawafanya wahurumiwe na wote waliowashikilia mateka.
47 O hilf uns, HERR, unser Gott, und bring uns wieder zusammen aus den Heiden, damit wir deinem heiligen Namen danken, uns glücklich preisen, deinen Ruhm zu künden!
Ee Bwana Mungu wetu, tuokoe. Tukusanye tena kutoka kwa mataifa, ili tuweze kulishukuru jina lako takatifu, na kushangilia katika sifa zako.
48 Gepriesen sei der HERR, der Gott Israels, von Ewigkeit zu Ewigkeit! Und alles Volk sage »Amen!« Halleluja!
Atukuzwe Bwana, Mungu wa Israeli, tangu milele na hata milele. Watu wote na waseme, “Amen!” Msifuni Bwana.