< 4 Mose 33 >
1 Folgendes sind die einzelnen Züge der Israeliten, in denen sie aus Ägypten nach ihren Heerscharen unter der Führung Moses und Aarons ausgezogen sind.
Hizi ndizo safari za wana wa Israeli hapo walipotoka katika nchi ya Misri pamoja na makundi yao ya kijeshi chini ya uongozi wa Musa na Haruni.
2 Mose hatte nämlich auf Befehl des HERRN die Orte aufgeschrieben, von denen ihre Auszüge erfolgt waren; und folgendes sind ihre Züge von einem Aufbruchsort zum andern:
Musa aliandika maeneo yote tangu walipoondoka mpaka walipofika, kama alivyoamuriwa na BWANA. Hizi ndizo safari zao kama kutoka kwao kulivyokuwa kwa kila walipotoka.
3 Sie brachen von Ramses am fünfzehnten Tage des ersten Monats auf; am Tage nach dem Passah zogen die Israeliten mit hoch erhobener Hand vor den Augen aller Ägypter aus,
Mwezi wa kwanza walisafiri kutoka Ramesi, waliondoka siku ya kumi na tano. Asubuhi siku iliyofuata baada ya Pasaka, Wana wa Israeli waliondoka wazi wazi, mbele ya machoya Wamisri wote.
4 während die Ägypter alle Erstgeborenen begruben, die der HERR unter ihnen hatte sterben lassen; denn der HERR hatte auch an ihren Göttern ein Strafgericht vollzogen.
Hii ilitokea wakati Wamisiri walipokuwa wakizika wazaliwa wao wa kwanza, ambao BWANA alikuwa amewaua miongoni mwao, kwa kuwa pia alikuwa ameiadhibu miungu yao.
5 Die Israeliten brachen also von Ramses auf und lagerten in Sukkoth.
Wana wa Israeli walisafiri kutoka Ramesi na kuweka kambi
6 Von Sukkoth zogen sie dann weiter und lagerten in Etham, das am Rande der Wüste liegt.
Sukothi. Walisafiri toka Sukothi na kuweka kambi Ethamu, mwisho wa nyika.
7 Von Etham zogen sie weiter und wandten sich nach Pi-Hahiroth, das Baal-Zephon gegenüber liegt, und lagerten östlich von Migdol.
Wakasafiri kutoka Ethamu wakarudi mpaka Pi-Hahirothi, ambayo inaikabili Baali Zephoni, ambapo waliweka kambi kuikabili Migidoli
8 Von Pi-Hahiroth brachen sie auf und zogen mitten durch das Meer nach der Wüste hin; sie wanderten dann drei Tagereisen weit in der Wüste Etham und lagerten in Mara.
Kisha wakasafiri toka mkabala wa Pi-Hairothi na kupita katikati ya bahari kuelekea nyikani. Wakasafiri safari ya siku tatu katika nyika ya Ethamu na kuweka kambi Mara.
9 Von Mara zogen sie weiter und kamen nach Elim; dort waren zwölf Wasserquellen und siebzig Palmbäume, und sie lagerten daselbst.
Wakasafiri kutoka Mara kufika Elimu. Pale Elimu kulikuwa na chemichemi kumi na mbili za maji na miti sabini ya mitende. hapo ndipo walipoweka kambi.
10 Von Elim zogen sie weiter und lagerten am Schilfmeer.
Walisafiri kutoka Elimu na kuweka kambi karibu na Bahari ya Shamu.
11 Vom Schilfmeer zogen sie weiter und lagerten in der Wüste Sin.
Walisafiri kutoka Bahari ya Shamu na kuweka kambi katika nyika ya Sini.
12 Aus der Wüste Sin zogen sie weiter und lagerten in Dophka.
Walisafiri kutoka nyika ya Sini na kuweka kambi Dofka.
13 Von Dophka zogen sie weiter und lagerten in Alus.
Wakasafiri kutoka Dofka na kuweka kambi Alushi.
14 Von Alus zogen sie weiter und lagerten in Rephidim; dort hatte das Volk kein Wasser zu trinken.
Wakasafiri kutoka Alushi na kuweka kambi Refidimu, ambapo watu walikosa maji ya kunywa.
15 Von Rephidim zogen sie weiter und lagerten in der Wüste Sinai.
Walisafiri kutoka Refidimu na kuweka kambi kwenye nyika ya Sinai.
16 Aus der Wüste Sinai zogen sie weiter und lagerten bei den Lustgräbern.
Walisafiri kutoka nyika ya Sinai na kuweka kambi Kibrothi Hataava.
17 Von den Lustgräbern zogen sie weiter und lagerten in Hazeroth.
Walisafiri kutoka Kibrothi Hataava na kuweka kambi Hazerothi.
18 Von Hazeroth zogen sie weiter und lagerten in Rithma.
Walisafiri kutoka Hazerothi na kuweka kambi Rithima.
19 Von Rithma zogen sie weiter und lagerten in Rimmon-Perez.
Walisafiri kutoka Rithima na kuweka kambi Rimoni Perezi.
20 Von Rimmon-Perez zogen sie weiter und lagerten in Libna.
Walisafiri kutoka Rimoni Perezi na kuweka kambi Libna.
21 Von Libna zogen sie weiter und lagerten in Rissa.
Walisafiri kutoka Libna na kuweka kambi Risa.
22 Von Rissa zogen sie weiter und lagerten in Kehelatha.
Walisafiri kutoka Risa na kuweka kambi Kehelatha.
23 Von Kehelatha zogen sie weiter und lagerten am Berge Sepher.
Walisafiri kutoka Kehelatha na kuweka kambi kwenye Mlima Sheferi.
24 Vom Berge Sepher zogen sie weiter und lagerten in Harada.
Walisafiri kutoka Mlima Sheferi na kuweka kambi Harada.
25 Von Harada zogen sie weiter und lagerten in Makheloth.
Walisafiri kutoka Harada na kuweka kambi Makelothi.
26 Von Makheloth zogen sie weiter und lagerten in Thahath.
Walisafiri kutoka Makelothi na kuweka kambi Tahathi.
27 Von Thahath zogen sie weiter und lagerten in Therah.
Walisafiri kutoka Ttahalathi na kuweka kambi Tera.
28 Von Therah zogen sie weiter und lagerten in Mithka.
Walisafiri kutokaTera na kuweka kambi Mithika.
29 Von Mithka zogen sie weiter und lagerten in Hasmona.
Walisafiri kutoka Mithika na kuweka kambi Hashimona.
30 Von Hasmona zogen sie weiter und lagerten in Moseroth.
Walisafiri kutoka Hashimona na kuweka kambi Moserothi.
31 Von Moseroth zogen sie weiter und lagerten in Bene-Jaakan.
Walisafiri kutoka Moserothi na kuweka kambi Bene Jaakani.
32 Von Bene-Jaakan zogen sie weiter und lagerten in Hor-Hagidgad.
Walisafiri kutoka Bene Jaakani na kuweka kambi Hori Hagidigadi.
33 Von Hor-Hagidgad zogen sie weiter und lagerten in Jotbatha.
Walisafiri kutoka Hori Hagidigadi na kuweka kambi Jotibatha.
34 Von Jotbatha zogen sie weiter und lagerten in Abrona.
Walisafiri kutoka Jotibatha na kuweka kambi Abrona.
35 Von Abrona zogen sie weiter und lagerten in Ezjon-Geber.
Walisafiri kutoka Abrona na kuweka kambi Ezioni Geberi.
36 Von Ezjon-Geber zogen sie weiter und lagerten in der Wüste Zin, das ist Kades.
Walisafiri toka Ezioini Geberi na kuweka kambi katika nyika ya Sini kule Kadeshi.
37 Von Kades zogen sie weiter und lagerten am Berge Hor, an der Grenze des Landes der Edomiter.
Walisafiri kutoka Kadeshi na kuweka kambi Mlima Hori, Pembezoni mwa nchi ya Edomu.
38 Da stieg der Priester Aaron nach dem Befehl des HERRN auf den Berg Hor hinauf und starb daselbst im vierzigsten Jahr nach dem Auszug der Israeliten aus dem Lande Ägypten am ersten Tage des fünften Monats;
Hapo ndipo Haruni kuhani alipoenda kwenye Mlima Hori kwa amri ya BWANA na kufa kule mwaka wa arobaini bada ya Wisraeli kutoka katika nchi ya Misri, katika siku ya kwanza ya mwezi wa tano.
39 Aaron war aber 123 Jahre alt, als er auf dem Berge Hor starb.
Haruni alikuwa na umri wa mika 123 alipokufa pale juu ya Mlima Hori.
40 [Und der Kanaanäer, der König von Arad, der im südlichen Teile des Landes Kanaan wohnte, hörte vom Heranrücken der Israeliten.]
Wakanaani, mfalme wa Aradi, ambao waliishi kusini mwa nyika katika nchi ya Kanaani, walisikia juu ya ujio wa wana wa Israeli.
41 Vom Berge Hor zogen sie dann weiter und lagerten in Zalmona.
Walisafiri kutika Mlima Hori n a kuweka kambi Zalimona.
42 Von Zalmona zogen sie weiter und lagerten in Phunon.
Walisafiri kutoka Zalimona na kuweka kambi Punoni.
43 Von Phunon zogen sie weiter und lagerten in Oboth.
Walisafiri kutoka Punoni na kuweka kambi Obothi.
44 Von Oboth zogen sie weiter und lagerten in Ijje-Abarim an der Grenze des Moabiterlandes.
Walisafiri kutoka Obothi na kuweka kambi Abarimu, katika mpaka wa Moabu.
45 Von Ijjim zogen sie weiter und lagerten in Dibon-Gad.
Walisafiri kutoka Abarimu na kuweka kambi Diboni Gadi.
46 Von Dibon-Gad zogen sie weiter und lagerten in Almon-Diblathaim.
Walisafiri kutoka Diboni Gadi na kuweka kambi Alimoni Diblathaimu.
47 Von Almon-Diblathaim zogen sie weiter und lagerten am Gebirge Abarim östlich vom Nebo.
Walisafiri kutoka Alimoni Diblathaimu na kuweka kambi kwenye milima ya Abarimu mkabala na Nebo.
48 Vom Gebirge Abarim zogen sie weiter und lagerten sich in den Steppen der Moabiter am Jordan, Jericho gegenüber;
Walisafiri kutoka mlima wa Abarimuna kuweka kambi kwenye nyanda za Moabu karibu na Yorodani huko Yeriko.
49 und zwar lagerten sie am Jordan von Beth-Jesimoth bis Abel-Sittim in den Steppen der Moabiter.
Waliweka kambi karibu na Yorodani, kutoka Bethi Jeshimothi mpaka Abeli Shitimu katika nyanda za Moabu.
50 Der HERR gebot dann dem Mose in den Steppen der Moabiter am Jordan, Jericho gegenüber: »Teile den Israeliten folgende Verordnungen mit:
Hapo BWANA alinenana Musa katika nyanda za Moabu karibu na Yorodani kule Yeriko akasema,
51 Wenn ihr über den Jordan in das Land Kanaan hinübergezogen seid,
“Nena na wana wa Israeli uwaambie. 'Mtakapovuka mto Yorodani kuingia Kanaani,
52 sollt ihr alle Bewohner des Landes vor euch her austreiben und alle ihre Götzenbilder vernichten; auch alle ihre Gußbilder sollt ihr vernichten und alle ihre Höhen zerstören.
ndipo mtakapowafukuza wenyeji wote mbele yenu. Mtaziharibu sanamu zote za kuchongwa. Mtaziharibu sanamu zao za kusubu na kuharibu mahali pao pote palipoinuka.
53 Ihr sollt dann das Land in Besitz nehmen und darin wohnen; denn euch habe ich das Land als Eigentum verliehen.
Mtachukua hiyo ardhi iwe mali yenu na muishi ndani yake, kwa sababu nimewapeni hiyo nchi iwe mali yenu.
54 Und zwar sollt ihr euch das Land durch das Los als Erbbesitz zuteilen entsprechend euren Stämmen: den größeren Stämmen sollt ihr einen größeren Erbbesitz geben und den kleineren einen weniger großen Erbbesitz zuteilen; doch wohin immer einem jeden das Los fällt, da soll es ihm als Eigentum zuteil werden: nach euren väterlichen Stämmen sollt ihr euch das Land als Erbbesitz zuteilen.
Mtairithi hiyo nchi kwa kupiga kura, kwa kufuata kila ukoo. Kwa zile koo kubwa kubwa mtawapa sehemu kubwa ya ardhi, na kwa zile koo ndogo ndogo mtawapa sehemu ndogo ya ardhi. Kura itakapoanguka kwenye kila ukoo, hiyo ardhi itakuwa mali yake. Mtairithi ardhi kufuata ukoo wa kabilla la jamaa zenu.
55 Wenn ihr aber die Bewohner des Landes nicht vor euch her austreibt, so werden die, welche ihr von ihnen übriglaßt, zu Dornen in euren Augen und zu Stacheln in euren Seiten werden und euch in dem Lande, in dem ihr wohnen werdet, bedrängen.
Lakini kama hamtawafukuza wenyeji wa nchi hiyo watoke mbele yenu, ndipo wale watu mtakaowaruhusu wakae nanyi watakapokuwa kama sindano machoni mwenu na miiba katika mbavu zenu. Watayafanya maisha yenu yawe magumu katika nchi mnayoishi.
56 Die Folge wird dann sein, daß ich euch das Geschick widerfahren lasse, das ich ihnen zugedacht hatte.«
Ndipo itakapotokea kuwa kile ambacho Mimi ninakusudia kufanya kwa wale watu, Nitawafanyia pia ninyi'”