< Psalm 78 >

1 Eine Unterweisung Asaphs. Höre, mein Volk, mein Gesetz; neigt eure Ohren zu der Rede meines Mundes!
Utenzi wa Asafu. Enyi watu wangu, sikieni mafundisho yangu, sikilizeni maneno ya kinywa changu.
2 Ich will meinen Mund auftun zu Sprüchen und alte Geschichten aussprechen,
Nitafungua kinywa changu kwa mafumbo, nitazungumza mambo yaliyofichika, mambo ya kale:
3 die wir gehört haben und wissen und unsre Väter uns erzählt haben,
yale ambayo tuliyasikia na kuyajua, yale ambayo baba zetu walituambia.
4 daß wir's nicht verhalten sollten ihren Kindern, die hernach kommen, und verkündigten den Ruhm des HERRN und seine Macht und seine Wunder, die er getan hat.
Hatutayaficha kwa watoto wao; tutakiambia kizazi kijacho matendo yastahiliyo sifa ya Bwana, uweza wake, na maajabu aliyoyafanya.
5 Er richtete ein Zeugnis auf in Jakob und gab ein Gesetz in Israel, das er unsern Vätern gebot zu lehren ihre Kinder,
Aliagiza amri kwa Yakobo na akaweka sheria katika Israeli, ambazo aliwaamuru baba zetu wawafundishe watoto wao,
6 auf daß es die Nachkommen lernten und die Kinder, die noch sollten geboren werden; wenn sie aufkämen, daß sie es auch ihren Kinder verkündigten,
ili kizazi kijacho kizijue, pamoja na watoto ambao watazaliwa, nao pia wapate kuwaeleza watoto wao.
7 daß sie setzten auf Gott ihre Hoffnung und nicht vergäßen der Taten Gottes und seine Gebote hielten
Ndipo wangeweka tumaini lao kwa Mungu, nao wasingesahau matendo yake, bali wangalizishika amri zake.
8 und nicht würden wie ihre Väter, eine abtrünnige und ungehorsame Art, welchen ihr Herz nicht fest war und ihr Geist nicht treulich hielt an Gott,
Ili wasifanane na baba zao, waliokuwa kizazi cha ukaidi na uasi, ambao roho zao hazikuwa na uaminifu kwake, ambao roho zao hazikumwamini.
9 wie die Kinder Ephraim, die geharnischt den Bogen führten, abfielen zur Zeit des Streits.
Watu wa Efraimu, ingawa walijifunga pinde, walikimbia siku ya vita.
10 Sie hielten den Bund Gottes nicht und wollten nicht in seinem Gesetz wandeln
Hawakulishika agano la Mungu na walikataa kuishi kwa sheria yake.
11 und vergaßen seiner Taten und seiner Wunder, die er ihnen erzeigt hatte.
Walisahau aliyokuwa ameyatenda, maajabu aliyokuwa amewaonyesha.
12 Vor ihren Vätern tat er Wunder in Ägyptenland, im Felde Zoan.
Alitenda miujiza machoni mwa baba zao, huko Soani, katika nchi ya Misri.
13 Er zerteilte das Meer und ließ sie hindurchgehen und stellte das Wasser wie eine Mauer.
Aliigawanya bahari akawapitisha, alifanya maji yasimame imara kama ukuta.
14 Er leitete sie des Tages mit einer Wolke und des Nachts mit einem hellen Feuer.
Aliwaongoza kwa wingu mchana na kwa nuru kutoka kwenye moto usiku kucha.
15 Er riß die Felsen in der Wüste und tränkte sie mit Wasser die Fülle
Alipasua miamba jangwani na akawapa maji tele kama bahari,
16 und ließ Bäche aus den Felsen fließen, daß sie hinabflossen wie Wasserströme.
alitoa vijito kutoka kwenye jabali lililochongoka, akayafanya maji yatiririke kama mito.
17 Dennoch sündigten sie weiter gegen ihn und erzürnten den Höchsten in der Wüste
Lakini waliendelea kutenda dhambi dhidi yake, wakiasi jangwani dhidi ya Aliye Juu Sana.
18 und versuchten Gott in ihrem Herzen, daß sie Speise forderten für ihre Seelen,
Kwa makusudi walimjaribu Mungu, wakidai vyakula walivyovitamani.
19 und redeten gegen Gott und sprachen: “Ja, Gott sollte wohl können einen Tisch bereiten in der Wüste?
Walinena dhidi ya Mungu, wakisema, “Je, Mungu aweza kuandaa meza jangwani?
20 Siehe, er hat wohl den Felsen geschlagen, daß Wasser flossen und Bäche sich ergossen; aber wie kann er Brot geben und seinem Volke Fleisch verschaffen?”
Alipopiga mwamba, maji yalitoka kwa nguvu, vijito vikatiririka maji mengi. Lakini je, aweza kutupa chakula pia? Je, anaweza kuwapa watu wake nyama?”
21 Da nun das der HERR hörte, entbrannte er, und Feuer ging an in Jakob, und Zorn kam über Israel,
Bwana alipowasikia, alikasirika sana, moto wake ukawa dhidi ya Yakobo, na ghadhabu yake ikawaka dhidi ya Israeli,
22 daß sie nicht glaubten an Gott und hofften nicht auf seine Hilfe.
kwa kuwa hawakumwamini Mungu, wala kuutumainia ukombozi wake.
23 Und er gebot den Wolken droben und tat auf die Türen des Himmels
Hata hivyo alitoa amri kwa anga zilizo juu na kufungua milango ya mbingu,
24 und ließ das Man auf sie regnen, zu essen, und gab ihnen Himmelsbrot.
akawanyeshea mana ili watu wale; aliwapa nafaka ya mbinguni.
25 Sie aßen Engelbrot; er sandte ihnen Speise die Fülle.
Watu walikula mkate wa malaika, akawatumia chakula chote ambacho wangeliweza kula.
26 Er ließ wehen den Ostwind unter dem Himmel und erregte durch seine Stärke den Südwind
Aliachia upepo wa mashariki kutoka kwenye mbingu na kuuongoza upepo wa kusini kwa uwezo wake.
27 und ließ Fleisch auf sie regnen wie Staub und Vögel wie Sand am Meer
Aliwanyeshea nyama kama mavumbi, ndege warukao kama mchanga wa pwani.
28 und ließ sie fallen unter ihr Lager allenthalben, da sie wohnten.
Aliwafanya washuke ndani ya kambi yao, kuzunguka mahema yao yote.
29 Da aßen sie und wurden allzu satt; er ließ sie ihre Lust büßen.
Walikula na kusaza, kwa maana alikuwa amewapa kile walichotamani.
30 Da sie nun ihre Lust gebüßt hatten und noch davon aßen,
Kabla hawajamaliza kula walichokitamani, hata kilipokuwa kingali bado vinywani mwao,
31 da kam der Zorn Gottes über sie und erwürgte die Vornehmsten unter ihnen und schlug darnieder die Besten in Israel.
hasira ya Mungu ikawaka juu yao, akawaua wale waliokuwa na nguvu zaidi miongoni mwao, akiwaangusha vijana wa Israeli.
32 Aber über das alles sündigten sie noch mehr und glaubten nicht an seine Wunder.
Licha ya haya yote, waliendelea kutenda dhambi, licha ya maajabu yake, hawakuamini.
33 Darum ließ er sie dahinsterben, daß sie nichts erlangten und mußten ihr Leben lang geplagt sein.
Kwa hiyo akamaliza siku zao katika ubatili na miaka yao katika vitisho.
34 Wenn er sie erwürgte, suchten sie ihn und kehrten sich zu Gott
Kila mara Mungu alipowaua baadhi yao, waliosalia walimtafuta, walimgeukia tena kwa shauku.
35 und gedachten, daß Gott ihr Hort ist und Gott der Höchste ihr Erlöser ist,
Walikumbuka kwamba Mungu alikuwa Mwamba wao, kwamba Mungu Aliye Juu Sana alikuwa Mkombozi wao.
36 und heuchelten mit ihrem Munde und logen ihm mit ihrer Zunge;
Lakini walimdanganya kwa vinywa vyao, wakisema uongo kwa ndimi zao,
37 aber ihr Herz war nicht fest an ihm, und hielten nicht treulich an seinem Bund.
mioyo yao haikuwa thabiti kwake, wala hawakuwa waaminifu katika agano lake.
38 Er aber war barmherzig und vergab die Missetat und vertilgte sie nicht und wandte oft seinen Zorn ab und ließ nicht seinen ganzen Zorn gehen.
Hata hivyo alikuwa na huruma, alisamehe maovu yao na hakuwaangamiza. Mara kwa mara alizuia hasira yake, wala hakuchochea ghadhabu yake yote.
39 Denn er gedachte, daß sie Fleisch sind, ein Wind, der dahinfährt und nicht wiederkommt.
Alikumbuka kwamba wao walikuwa nyama tu, upepo upitao ambao haurudi.
40 Wie oft erzürnten sie ihn in der Wüste und entrüsteten ihn in der Einöde!
Mara ngapi walimwasi jangwani na kumhuzunisha nyikani!
41 Sie versuchten Gott immer wieder und meisterten den Heiligen in Israel.
Walimjaribu Mungu mara kwa mara, wakamkasirisha yeye Aliye Mtakatifu wa Israeli.
42 Sie gedachten nicht an seine Hand des Tages, da er sie erlöste von den Feinden;
Hawakukumbuka uwezo wake, siku aliyowakomboa kutoka kwa mtesi,
43 wie er denn seine Zeichen in Ägypten getan hatte und seine Wunder im Lande Zoan;
siku aliyoonyesha ishara zake za ajabu huko Misri, maajabu yake huko Soani.
44 da er ihr Wasser in Blut wandelte, daß sie ihre Bäche nicht trinken konnten;
Aligeuza mito yao kuwa damu, hawakuweza kunywa maji kutoka vijito vyao.
45 da er Ungeziefer unter sie schickte, daß sie fraß, und Frösche, die sie verderbten,
Aliwapelekea makundi ya mainzi yakawala, na vyura wakawaharibu.
46 und gab ihre Gewächse den Raupen und ihre Saat den Heuschrecken;
Aliruhusu tunutu kuharibu mimea yao, mazao yao kwa nzige.
47 da er ihre Weinstöcke mit Hagel schlug und ihre Maulbeerbäume mit Schloßen;
Aliharibu mizabibu yao kwa mvua ya mawe na mikuyu yao kwa mvua iliyochangamana na theluji.
48 da er ihr Vieh schlug mit Hagel und ihre Herden mit Wetterstrahlen;
Aliwaachia mifugo yao mvua ya mawe, akayapiga makundi ya wanyama wao kwa radi.
49 da er böse Engel unter sie sandte in seinem grimmigen Zorn und ließ sie toben und wüten und Leid tun;
Aliwafungulia hasira yake kali, ghadhabu yake, hasira na uadui, na kundi la malaika wa kuharibu.
50 da er seinen Zorn ließ fortgehen und ihre Seele vor dem Tode nicht verschonte und übergab ihr Leben der Pestilenz;
Aliitengenezea njia hasira yake, hakuwaepusha na kifo, bali aliwaachia tauni.
51 da er alle Erstgeburt in Ägypten schlug, die Erstlinge ihrer Kraft in den Hütten Hams,
Aliwapiga wazaliwa wote wa kwanza wa Misri, matunda ya kwanza ya ujana katika mahema ya Hamu.
52 und ließ sein Volk ausziehen wie die Schafe und führte sie wie eine Herde in der Wüste.
Lakini aliwatoa watu wake kama kundi, akawaongoza kama kondoo kupitia jangwani.
53 Und leitete sie sicher, daß sie sich nicht fürchteten; aber ihre Feinde bedeckte das Meer.
Aliwaongoza salama, wala hawakuogopa, bali bahari iliwameza adui zao.
54 Und er brachte sie zu seiner heiligen Grenze, zu diesem Berge, den seine Rechte erworben hat,
Hivyo akawaleta hadi kwenye mpaka wa nchi yake takatifu, hadi nchi ya vilima ambayo mkono wake wa kuume ulikuwa umeitwaa.
55 und vertrieb vor ihnen her die Völker und ließ ihnen das Erbe austeilen und ließ in jener Hütten die Stämme Israels wohnen.
Aliyafukuza mataifa mbele yao, na kuwagawia nchi zao kama urithi, aliwakalisha makabila ya Israeli katika makao yao.
56 Aber sie versuchten und erzürnten Gott den Höchsten und hielten ihre Zeugnisse nicht
Lakini wao walimjaribu Mungu, na kuasi dhidi ya Yeye Aliye Juu Sana, wala hawakuzishika sheria zake.
57 und fielen zurück und verachteten alles wie ihre Väter und hielten nicht, gleichwie ein loser Bogen,
Kama baba zao, hawakuwa thabiti wala waaminifu, wakawa wasioweza kutegemewa kama upinde wenye kasoro.
58 und erzürnten ihn mit ihren Höhen und reizten ihn mit ihren Götzen.
Wakamkasirisha Mungu kwa mahali pao pa juu pa kuabudia miungu, wakachochea wivu wake kwa sanamu zao.
59 Und da das Gott hörte, entbrannte er und verwarf Israel ganz,
Wakati Mungu alipowasikia, alikasirika sana, akamkataa Israeli kabisa.
60 daß er seine Wohnung zu Silo ließ fahren, die Hütte, da er unter Menschen wohnte,
Akaiacha hema ya Shilo, hema aliyokuwa ameiweka katikati ya wanadamu.
61 und gab seine Macht ins Gefängnis und seine Herrlichkeit in die Hand des Feindes
Akalipeleka Sanduku la nguvu zake utumwani, utukufu wake mikononi mwa adui.
62 und übergab sein Volk ins Schwert und entbrannte über sein Erbe.
Aliachia watu wake wauawe kwa upanga, akaukasirikia sana urithi wake.
63 Ihre junge Mannschaft fraß das Feuer, und ihre Jungfrauen mußten ungefreit bleiben.
Moto uliwaangamiza vijana wao, na wanawali wao hawakuimbiwa nyimbo za arusi,
64 Ihre Priester fielen durchs Schwert, und waren keine Witwen, die da weinen sollten.
makuhani wao waliuawa kwa upanga, wala wajane wao hawakuweza kulia.
65 Und der Herr erwachte wie ein Schlafender, wie ein Starker jauchzt, der vom Wein kommt,
Ndipo Bwana alipoamka kama vile kuamka usingizini, kama vile mtu aamkavyo kutoka kwenye bumbuazi la mvinyo.
66 und schlug seine Feinde zurück und hängte ihnen ewige Schande an.
Aliwapiga na kuwashinda adui zake, akawatia katika aibu ya milele.
67 Und er verwarf die Hütte Josephs und erwählte nicht den Stamm Ephraim,
Ndipo alipozikataa hema za Yosefu, hakulichagua kabila la Efraimu,
68 sondern erwählte den Stamm Juda, den Berg Zion, welchen er liebte.
lakini alilichagua kabila la Yuda, Mlima Sayuni, ambao aliupenda.
69 Und baute sein Heiligtum hoch, wie die Erde, die ewiglich fest stehen soll.
Alijenga patakatifu pake kama vilele, kama dunia ambayo aliimarisha milele.
70 Und erwählte seinen Knecht David und nahm ihn von den Schafställen;
Akamchagua Daudi mtumishi wake na kumtoa kwenye mazizi ya kondoo.
71 von den säugenden Schafen holte er ihn, daß er sein Volk Jakob weiden sollte und sein Erbe Israel.
Kutoka kuchunga kondoo alimleta kuwa mchungaji wa watu wake Yakobo, wa Israeli urithi wake.
72 Und er weidete sie auch mit aller Treue und regierte mit allem Fleiß.
Naye Daudi aliwachunga kwa uadilifu wa moyo, kwa mikono ya ustadi aliwaongoza.

< Psalm 78 >