< 1 Chronik 6 >
1 Die Kinder Levis waren: Gerson, Kahath und Merari.
Wana wa Levi walikuwa Gerishoni, Kohathi, na Merari.
2 Die Kinder aber Kahaths waren: Amram, Jizhar, Hebron und Usiel.
Wana wa Kohathi walikuwa Amramu, Izhari, Hebroni, na Uzieli.
3 Die Kinder Amrams waren: Aaron, Mose und Mirjam. Die Kinder Aaron waren Nadab, Abihu, Eleasar und Ithamar.
Wana wa Amramu walikuwa Aruni, Musa, Miriamu. Wana wa Aruni walikuwa Nadabu, Abihu, Eleazari, na Ithamari.
4 Eleasar zeugte Pinehas. Pinehas zeugte Abisua.
Eleazari akawa baba wa Finehasi, na Finehasi akawa baba wa Abishua.
5 Abisua zeugte Bukki. Bukki zeugte Usi.
Abishua akawa baba wa Buki, na Buki akawa baba wa Uzi.
6 Usi zeugte Serahja. Serahja zeugte Merajoth.
Uzi akawa baba wa Zerahia, na Zerahia akawa baba wa Meraioti.
7 Merajoth zeugte Amarja. Amarja zeugte Ahitob.
Meraioti akawa baba wa Amaria, na Amaria akawa baba wa Ahitubi.
8 Ahitob zeugte Zadok. Zadok zeugte Ahimaaz.
Ahitubi akawa baba wa Zadoki, na Zadoki akawa baba wa Ahimazi.
9 Ahimaaz zeugte Asarja. Asarja zeugte Johanan.
Ahimazi akawa baba wa Azaria, na Azaria akawa baba wa Yohanani.
10 Johanan zeugte Asarja, den, der Priester war in dem Hause, das Salomo baute zu Jerusalem.
Yohanani akawa baba wa Azaria, aliye hudumu katika hekalu alilo lijenga Sulemani ndaniya Yerusalemu.
11 Asarja zeugte Amarja. Amarja zeugte Ahitob.
Azaria akawa baba wa Amaria, na Amaria akawa baba wa Ahitubi.
12 Ahitob zeugte Zadok. Zadok zeugte Sallum.
Ahitubi akawa baba wa Zadoki, na Zadoki akawa baba wa Shalumu.
13 Sallum zeugte Hilkia. Hilkia zeugte Asarja.
Shalumu akawa baba wa Hilikia, na Hilikia akawa baba wa Azaria.
14 Asarja zeugte Seraja. Seraja zeugte Jozadak.
Azaria akawa baba Seraia, na Seraia akawa baba wa Yehozadaki.
15 Jozadak aber ward mit weggeführt, da der HERR Juda und Jerusalem durch Nebukadnezar ließ gefangen wegführen.
Yehozadaki akaenda matekani Yahweh alipo wapeleka utumwani Yuda na Yerusalemu kwa mkono wa Nebukadneza.
16 So sind nun die Kinder Levis diese: Gerson, Kahath, Merari.
Wana wa Levi walikuwa Gerishomu, Kohathi, na Merari.
17 So heißen aber die Kinder Gersons: Libni und Simei.
Wana wa Gerishomu walikuwa Libini na Shimei.
18 Aber die Kinder Kahaths heißen: Amram, Jizhar, Hebron und Usiel.
Wana wa Kohathi walikuwa Amramu, Izhari, Hebroni, na Uzieli.
19 Die Kinder Meraris heißen: Maheli und Musi. Das sind die Geschlechter der Leviten nach ihren Vaterhäusern.
Wana wa Merari walikuwa Mahili na Mushi. Hawa walikuwa koo za Walawi kwa familia za baba zao.
20 Gerson Sohn war Libni; des Sohn war Jahath; des Sohn war Simma;
Uzao wa Gerishomu ulianza na mwanae Libini. Mwana wa Libini alikuwa Jahathi. Mwanae alikuwa Zima.
21 des Sohn war Joah; des Sohn war Iddo; des Sohn war Serah; des Sohn war Jeathrai.
Mwanae alikuwa Yoa. Mwanae alikuwa alikuwa Ido. Mwanae alikuwa Zera. Mwanae alikuwa Yeatherai.
22 Kahaths Sohn aber war Aminadab; des Sohn war Korah; des Sohn war Assir;
Uzao wa Kohathi ulianza na mwanae Aminadabu. Mwanae alikuwa Kora. Mwanae alikuwa Asiri.
23 des Sohn war Elkana; des Sohn war Abiasaph; des Sohn war Assir;
Mwanae alikuwa Elikana. Mwanae alikuwa Ebiasa. Mwanae alikuwa Asiri.
24 des Sohn war Thahat; des Sohn war Uriel; des Sohn war Usia; des Sohn war Saul.
Mwanae alikuwa Tahathi. Mwanae alikuwa Urieli. Mwanae alikuwa uzia. Mwanae alikuwa Shauli.
25 Die Kinder Elkanas waren: Amasai und Ahimoth;
Wana wa Elikana walikuwa Amasai, Ahimothi, na Elikana.
26 des Sohn war Elkana; des Sohn war Elkana von Zoph; des Sohn war Nahath;
Mwana wa huyu Elikana wa pili alikuwa Zofai. Mwanae alikuwa Nahathi.
27 des Sohn war Eliab; des Sohn war Jeroham; des Sohn war Elkana.
Mwanae alikuwa Eliabu. Mwanae alikuwa Yehoramu. Mwanae alikuwa Elikana.
28 Und die Kinder Samuels waren: der Erstgeborene Vasni und Abia.
Wana wa Samwali walikuwa mzaliwa wa kwanza, Yoeli, na Abija, wa pili.
29 Meraris Sohn war Maheli; des Sohn war Libni; des Sohn war Simei; des Sohn war Usa;
Mwana wa Merari alikuwa Mahili. Mwanae alikuwa Libini.
30 des Sohn war Simea; des Sohn war Haggia; des Sohn war Asaja.
Mwanae alikuwa Shimei. Mwanae alikuwa Uza. Mwanae alikuwa Shimea. Mwanae alikuwa Hagia. Mwana alikuwa Asaia.
31 Dies sind aber, die David bestellte, zu singen im Hause des HERRN, als die Lade des Bundes zur Ruhe gekommen war;
Haya ndio majina ya wanaume ambao Daudi waliwaeka kusimamia muziki katika nyumba ya Yahweh, baada ya sanduku kuja hapo.
32 und sie dienten vor der Wohnung der Hütte des Stifts mit Singen, bis daß Salomo das Haus des HERRN baute zu Jerusalem, und standen nach ihrer Weise in ihrem Amt.
Walitumika kwa kuimba mbele ya hema, hema la kukutania, mpaka Sulemani alipo jenga nyumba ya Yahweh ndani ya Yerusalemu. Walikamilisha wajibu wao kwa kadiri ya maelekezo waliopewa.
33 Und dies sind sie, die da standen, und ihre Kinder: Von den Kindern Kahaths war Heman, der Sänger, der Sohn Joels, des Sohnes Samuel;
Hawa walitumika pamoja na wana wao. Katika makabila ya Wakohathi alitoka Hemani mwana muziki. Babu zake walikuwa hawa, kurudi nyuma ya wakati: Hemani alikuwa mwana wa Yoeli. Yoeli alikuwa mwana wa Samweli.
34 des Sohnes Elkanas, des Sohnes Jerohams, des Sohnes Eliels, des Sohnes Thoahs,
Samweli alikuwa mwana wa Elikana. Elikana alikuwa mwana wa Yerohamu. Yerohamu alikuwa mwana wa Elieli. Elieli alikuwa mwana wa Toa.
35 des Sohnes Zuphs, des Sohnes Elkanas, des Sohnes Mahaths, des Sohnes Amasais,
Toa alikuwa mwana wa Zufi. Zufi alikuwa mwana wa Elikana. Elikana alikuwa mwana wa Mahathi. Mahathi alikuwa mwana wa Amasai. Amasai alikuwa mwana wa Elikana.
36 des Sohnes Elkanas, des Sohnes Joels, des Sohnes Asarjas, des Sohnes Zephanjas,
Elikana alikuwa mwana wa Yoeli. Yoeli alikuwa mwana wa Azaria. Azaria alikuwa mwana wa Zefania.
37 des Sohnes Thahaths, des Sohnes Assirs, des Sohnes Abiasaphs, des Sohnes Korahs,
Zefania alikuwa mwana wa Tahathi. Tahathi alikuwa mwana wa Asiri. Asiri alikuwa mwana wa Ebiasa. Ebiasa alikuwa mwana wa Kora.
38 des Sohnes Jizhars, des Sohnes Kahaths, des Sohnes Levis, des Sohnes Israels.
Kora alikuwa mwana wa Izhari. Izhari alikuwa mwana wa Kohathi. Kohathi alikuwa mwana wa Levi. Levi alikuwa mwana wa Israeli.
39 Und sein Bruder Asaph stand zu seiner Rechten. Und er, der Asaph, war ein Sohn Berechjas, des Sohnes Simeas,
Msaidizi wa Hemani alikuwa Asafu, aliye simama mkono wake wa kuume. Asafu alikuwa mwana Berekia. Berekia alikuwa mwana wa Shimea.
40 des Sohnes Michaels, des Sohnes Baesejas, des Sohnes Malchias,
Shimea alikuwa mwana Mikaeli. Mikaeli alikuwa mwana wa Baaseia. Baaseia alikuwa mwana wa Malikiya.
41 des Sohnes Athnis, des Sohnes Serahs, des Sohnes Adajas,
Malikiya alikuwa mwana wa Ethini. Ethini alikuwa mwana wa Zera. Zera alikuwa mwana wa Adaia.
42 des Sohnes Ethans, des Sohnes Simmas, des Sohnes Simeis,
Adaia alikuwa mwana wa Ethani. Ethani alikuwa mwana wa Zima. Zima alikuwa mwana wa Shimei.
43 des Sohnes Jahats, des Sohnes Gersons, des Sohnes Levis.
Shimei alikuwa mwana wa Yahathi. Yahathi alikuwa mwana wa Gerishomu. Gerishomu alikuwa mwana wa Levi.
44 Ihre Brüder aber, die Kinder Meraris, standen zur Linken: nämlich Ethan, der Sohn Kusis, des Sohnes Abdis, des Sohnes Malluchs,
Upande wa mkono wa koshoto wa Hemani walikuwa wasaidizi wake wana wa Merari. Alikuwa Ethani mwana wa Kishi. Kishi alikuwa mwana wa Abdi. Abdi alikuwa mwana wa Maluki.
45 des Sohnes Hasabjas, des Sohnes Amazjas, des Sohnes Hilkias,
Maluki alikuwa mwana wa Hashabia. Hashabia alikuwa mwana wa Amazia. Amazia alikuwa mwana wa Hilikia.
46 des Sohnes Amzis, des Sohnes Banis, des Sohnes Semers,
Hilikia alikuwa mwana wa Amzi. Amzi alikuwa mwana wa Bani. Bani alikuwa mwana wa Shemeri.
47 des Sohnes Mahelis, des Sohnes Musis, des Sohnes Meraris, des Sohnes Levis.
Shemeri alikuwa mwana wa Mahili. Mahili alikuwa mwana wa Mushi. Mushi alikuwa mwana wa Merari. Merari alikuwa mwana wa Levi.
48 Ihre Brüder aber, die Leviten, waren gegeben zu allerlei Amt an der Wohnung des Hauses Gottes.
Walawi, alipangiwa kufanya kazi zote za hema, nyumba ya Mungu.
49 Aaron aber und seine Söhne waren im Amt, anzuzünden auf dem Brandopferaltar und auf dem Räucheraltar und zu allem Geschäft im Allerheiligsten und zu versöhnen Israel, wie Mose, der Knecht Gottes, geboten hatte.
Aruni na wana wake walitoa sadaka katika madhabahu kwa ajili ya sadaka za kuteketeza; na sadaka katika madhabahu ya uvumba kwa kazi zote katika pa patakatifu. Hizi sadaka zilifanya maombezi kwa ajili ya Waisraeli, kwa kadiri ya yote ambayo Musa mtumishi wa Mungu aliwaamuru.
50 Dies sind aber die Kinder Aarons: Eleasar, sein Sohn: des Sohn war Pinehas; des Sohn war Abisua;
Uzao wa Aruni una kumbukwa kama ifuatavyo: Mwana wa Aruni alikuwa Eleazari. Mwana Eleazari alikuwa Finehasi. Mwana wa Finehasi alikuwa Abishua.
51 des Sohn war Bukki, des Sohn war Usi; des Sohn war Serahja;
Mwana wa Abishua alikuwa Buki. Mwana wa Buki alikuwa Uzi. Mwana wa Buki alikuwa Zerahia.
52 des Sohn war Merajoth; des Sohn war Amarja; des Sohn war Ahitob;
Mwana wa Zerahia alikuwa Meraiothi. Mwana wa Meraiothi alikuwa Amaria. Mwana wa Amaria alikuwa Ahitubi.
53 des Sohn war Zadok; des Sohn war Ahimaaz.
Mwana wa Ahitubi alikuwa Zadoki. Mwana wa Zadoki alikuwa Ahimazi.
54 Und dies ist ihre Wohnung und Sitz in ihren Grenzen, nämlich der Kinder Aaron, des Geschlechts der Kahathiter; denn das Los fiel ihnen zu,
Hizi ni sehemu ambazo wazao wa Aruni walipangiwa kuishi, wazao wa Aruni ambao walitoka katika koo za Wakohathi (maeneo ya kwanza yalikuwa yao).
55 und sie gaben ihnen Hebron im Lande Juda und desselben Vorstädte umher.
Walipewa Hebroni katika nchi ya Yuda na nchi ya malisho,
56 Aber das Feld der Stadt und ihre Dörfer gaben sie Kaleb, dem Sohn Jephunnes.
lakini maeneo ya mji na vijiji alipewa Kalebu mwana wa Yefune.
57 So gaben sie nun den Kinder Aaron die Freistädte Hebron und Libna samt ihren Vorstädten, Jatthir und Esthemoa mit ihren Vorstädten.
Kwa wazao wa Aruni waliwapa: Hebroni ( mji wa makimblio), na Libina pamoja na nchi ya malisho, Yatiri, Eshitemoa pamoja na nchi ya malisho,
Hileni pamoja na nchi ya malisho, na Debiri pamoja na nchi ya malisho.
59 Asan und Beth-Semes mit ihren Vorstädten;
Waliwapa uzao wa Aruni: Ashani pamoja na nchi ya malisho na Bethi Shemeshi pamoja na nchi ya malisho;
60 und aus dem Stamm Benjamin: Geba, Alemeth und Anathoth mit ihren Vorstädten, daß aller Städte in ihren Geschlechtern waren dreizehn.
na kutoka katika kabila la Benjamini walipewa Geba pamoja na nchi ya malisho, Alemethi pamoja na nchi ya malisho, na Anothothi na nchi ya malisho. Jumla ya miji yao ilikuwa kumi na tatu.
61 Aber den Kindern Kahaths nach ihren Geschlechtern wurden durch Los aus dem Stamm Ephraim, aus dem Stamm Dan und aus dem halben Stamm Manasse zehn Städte.
Uzao mwengine wa Kohathi waliwapa kwa sehemu miji kumi kutoka kwa kabila la Manase.
62 Den Kindern Gerson nach ihren Geschlechtern wurden aus dem Stamm Isaschar und aus dem Stamm Asser und aus dem Stamm Naphthali und aus dem Stamm Manasse in Basan dreizehn Städte.
Kwa uzao wa Gerishomu kwa koo zao tofauti walipewa miji kumi na tatu kutoka kwa makabila ya Isakari, Asheri, Naftali, na nusu ya kabila la Manase huko Bashani.
63 Den Kindern Merari nach ihren Geschlechtern wurden durch das Los aus dem Stamm Ruben und aus dem Stamm Gad und aus dem Stamm Sebulon zwölf Städte.
Kwa uzao wa Merari walipewa miji kumi, kulingana na koo zao, kutoka kwa makabila ya Rubeni, Gadi, na Zebuluni.
64 Und die Kinder Israel gaben den Leviten die Städte mit ihren Vorstädten,
Hivyo watu wa Israeli walitoa hii miji pamoja na nchi za malisho kwa Walawi.
65 nämlich durchs Los aus dem Stamm der Kinder Juda und aus dem Stamm der Kinder Simeon und aus dem Stamm der Kinder Benjamin die Städte, die sie mit Namen bestimmten.
Walitoa kwa sehemu miji iliyo tajwa awali kutoka katika kabila la Yuda, Simeoni, na Benjamini.
66 Aber den Geschlechtern der Kinder Kahath wurden Städte ihres Gebietes aus dem Stamm Ephraim.
Kwa baadhi ya koo za Wakohathi walitoa miji kutoka kwa kabila la Efraimu.
67 So gaben sie nun ihnen, dem Geschlecht der andern Kinder Kahath, die Freistädte: Sichem auf dem Gebirge Ephraim, Geser,
Waliwapa: Shekemu ( mji wa makimbilio) pamoja na nchi ya malisho katika milima ya Efraimu, Gezeri na nchi ya malisho,
Jokimeamu pamoja na nchi ya malisho, Bethi Horoni pamoja na nchi ya malisho,
69 Ajalon und Gath-Rimmon mit ihren Vorstädten.
Aiyaloni pamoja na nchi ya malisho, na Gathi Rimoni pamoja na nchi ya malisho.
70 Dazu aus dem halben Stamm Manasse: Aner und Bileam mit ihren Vorstädten.
Nusu ya kabila la Manase waliwapa Wakohathi: Aneri pamoja na nchi ya malisho na Bileamu pamoja na nchi ya malisho. Hizi zikawa mali za koo za Wakohathi.
71 Aber den Kindern Gerson gaben sie aus dem Geschlecht des halben Stammes Manasse: Golan in Basan und Astharoth mit ihren Vorstädten.
Kwa uzao wa Gerishomu kutoka koo za nusu ya kabila la Manase, waliwapa: Golani huko Baashani na nchi ya malisho na Ashitarothi pamoja na nchi ya malisho.
72 Aus dem Stamm Isaschar: Kedes, Dabrath,
Kabila la Isakari liliwapa uzao wa Gerishomu: Kedeshi pamoja na nchi ya malisho, Dabera pamoja na nchi ya malisho,
73 Ramoth und Anem mit ihren Vorstädten.
Ramothi pamoja na nchi ya malisho, na Anemu pamoja na nchi ya malisho.
74 Aus dem Stamm Asser: Masal, Abdon,
Isakari alipokea kutoka kwa kabila la Asheri: Mashali pamoja na nchi ya malisho, Abdoni pamoja na nchi ya malisho,
75 Hukok und Rehob mit ihren Vorstädten.
Hukoki pamoja na nchi ya malisho, na Rehobu pamoja na nchi ya malisho.
76 Aus dem Stamm Naphthali: Kedes in Galiläa, Hammon und Kirjathaim mit ihren Vorstädten.
Walipokea kutoka kabila la Naftali: Kedeshi iliyo Galileya pamoja na nchi ya malisho, Hamoni pamoja na nchi ya malisho, na Kiriathaimu pamoja na nchi ya malisho.
77 Den andern Kindern Merari gaben sie aus dem Stamm Sebulon: Rimmono und Thabor mit ihren Vorstädten;
Kwa Walawi wengine, uzao wa Merari, walipewa kutoka kabila la Zebuluni: Rimono pamoja na nchi ya malisho na Tabori pamoja na nchi ya malisho.
78 und jenseit des Jordans gegenüber Jericho, gegen der Sonne Aufgang am Jordan, aus dem Stamm Ruben: Bezer in der Wüste, Jahza,
Kwa wao pia walipewa, upande wa pili wa Yordani huko Yeriko, kwa upande wa mashariki mwa mto: Bezeri katika jangwa pamoja na nchi ya malisho, Yahzahi pamoja na nchi ya malisho,
79 Kedemoth und Mephaat mit ihren Vorstädten.
Kedemothi pamoka na nchi ya malisho, ma Mefathi pamoja na nchi ya malisho. Hizi zilitolewa kutoka kabila la Rubeni.
80 Aus dem Stamm Gad: Ramoth in Gilead, Mahanaim,
Walawi walipokea kutoka kabila la Gadi: Ramothi ya Gileadi pamoja na nchi ya malisho, Mahanaimu pamoja na nchi ya malisho,
81 Hesbon und Jaser mit ihren Vorstädten.
Heshiboni pamoja na nchi ya malisho, na Yazeri pamoja na nchi ya malisho.