< Psalm 57 >

1 Ein gülden Kleinod Davids, vorzusingen, daß er nicht umkäme, da er vor Saul floh in die Höhle. Sei mir gnädig, Gott, sei mir gnädig! Denn auf dich trauet meine Seele und unter dem Schatten deiner Flügel habe ich Zuflucht, bis daß das Unglück vorübergehe.
Kwa mwimbishaji. Mtindo wa “Usiharibu!” Utenzi wa Daudi. Baada ya kumponyoka Sauli pangoni. Unihurumie, Ee Mungu, unihurumie, kwa maana nafsi yangu inakukimbilia. Chini ya uvuli wa mbawa zako nitakimbilia mpaka maafa yapite.
2 Ich rufe zu Gott, dem Allerhöchsten, zu Gott, der meines Jammers ein Ende macht.
Namlilia Mungu Aliye Juu Sana, Mungu atimizaye makusudi yake kwangu.
3 Er sendet vom Himmel und hilft mir von der Schmach meines Versenkers. (Sela) Gott sendet seine Güte und Treue.
Hutumana kutoka mbinguni na kuniokoa, akiwakemea wale wanaonifuatilia vikali; Mungu huutuma upendo wake na uaminifu wake.
4 Ich liege mit meiner Seele unter den Löwen. Die Menschenkinder sind Flammen; ihre Zähne sind Spieße und Pfeile und ihre Zungen scharfe Schwerter.
Niko katikati ya simba, nimelala katikati ya wanyama wenye njaa kuu: watu ambao meno yao ni mikuki na mishale, ambao ndimi zao ni panga kali.
5 Erhebe dich, Gott, über den Himmel und deine Ehre über alle Welt!
Ee Mungu, utukuzwe juu ya mbingu, utukufu wako na uenee duniani kote.
6 Sie stellen meinem Gange Netze und drücken meine Seele nieder; sie graben vor mir eine Grube und fallen selbst drein. (Sela)
Waliitegea miguu yangu nyavu, nikainamishwa chini na dhiki. Wamechimba shimo katika njia yangu, lakini wametumbukia humo wao wenyewe.
7 Mein Herz ist bereit, Gott, mein Herz ist bereit, daß ich singe und lobe.
Ee Mungu, moyo wangu ni thabiti; nitaimba na kusifu kwa moyo wangu wote.
8 Wach auf, meine Ehre, wach auf, Psalter und Harfe! Frühe wille ich aufwachen.
Amka, nafsi yangu! Amka, kinubi na zeze! Nitayaamsha mapambazuko.
9 HERR, ich will dir danken unter den Völkern, ich will dir lobsingen unter den Leuten.
Nitakusifu wewe, Ee Bwana, katikati ya mataifa; nitaimba habari zako, katikati ya jamaa za watu.
10 Denn deine Güte ist, soweit der Himmel ist, und deine Wahrheit, soweit die Wolken gehen.
Kwa maana upendo wako ni mkuu, waenea hadi mbinguni, uaminifu wako unazifikia anga.
Ee Mungu, utukuzwe juu mbinguni, utukufu wako na uwe duniani pote.

< Psalm 57 >