< Psalm 34 >

1 Ein Psalm Davids, da er seine Gebärde verstellete vor Abimelech, der ihn von sich trieb, und er wegging. Ich will den HERRN loben allezeit; sein Lob soll immerdar in meinem Munde sein.
Zaburi ya Daudi, alipojifanya mwendawazimu mbele ya Abimeleki, ambaye alimfukuza, naye akaondoka. Nitamtukuza Bwana nyakati zote, sifa zake zitakuwa midomoni mwangu siku zote.
2 Meine Seele soll sich rühmen des HERRN, daß die Elenden hören und sich freuen.
Nafsi yangu itajisifu katika Bwana, walioonewa watasikia na wafurahi.
3 Preiset mit mir den HERRN und laßt uns miteinander seinen Namen erhöhen!
Mtukuzeni Bwana pamoja nami, naam, na tulitukuze jina lake pamoja.
4 Da ich den HERRN suchte, antwortete er mir und errettete mich aus aller meiner Furcht.
Nilimtafuta Bwana naye akanijibu, akaniokoa kwenye hofu zangu zote.
5 Welche ihn ansehen und anlaufen, deren Angesicht wird nicht zuschanden.
Wale wamtazamao hutiwa nuru, nyuso zao hazifunikwi na aibu kamwe.
6 Da dieser Elende rief, hörete der HERR und half ihm aus allen seinen Nöten.
Maskini huyu alimwita Bwana, naye akamsikia, akamwokoa katika taabu zake zote.
7 Der Engel des HERRN lagert sich um die her, so ihn fürchten, und hilft ihnen aus.
Malaika wa Bwana hufanya kituo akiwazunguka wale wamchao, naye huwaokoa.
8 Schmecket und sehet, wie freundlich der HERR ist! Wohl dem, der auf ihn trauet!
Onjeni mwone kwamba Bwana ni mwema, heri mtu yule anayemkimbilia.
9 Fürchtet den HERRN, ihr seine Heiligen; denn die ihn fürchten, haben keinen Mangel.
Mcheni Bwana enyi watakatifu wake, kwa maana wale wamchao hawapungukiwi na chochote.
10 Die Reichen müssen darben und hungern; aber die den HERRN suchen, haben keinen Mangel an irgendeinem Gut.
Wana simba wenye nguvu hutindikiwa na kuona njaa, bali wale wamtafutao Bwana hawatakosa kitu chochote kilicho chema.
11 Kommt her, Kinder, höret mir zu! Ich will euch die Furcht des HERRN lehren.
Njooni, watoto wangu, mnisikilize, nitawafundisha kumcha Bwana.
12 Wer ist, der gut Leben begehrt und gerne gute Tage hätte?
Yeyote kati yenu anayependa uzima na kutamani kuziona siku nyingi njema,
13 Behüte deine Zunge vor Bösem und deine Lippen, daß sie nicht falsch reden.
basi auzuie ulimi wake na mabaya, na midomo yake kutokana na kusema uongo.
14 Laß vom Bösen und tue Gutes, suche Frieden und jage ihm nach.
Aache uovu, atende mema, aitafute amani na kuifuatilia.
15 Die Augen des HERRN sehen auf die Gerechten und seine Ohren auf ihr Schreien.
Macho ya Bwana huwaelekea wenye haki, na masikio yake yako makini kusikiliza kilio chao.
16 Das Antlitz aber des HERRN stehet über die, so Böses tun, daß er ihr Gedächtnis ausrotte von der Erde.
Uso wa Bwana uko kinyume na watendao maovu, ili kufuta kumbukumbu lao duniani.
17 Wenn die (Gerechten) schreien, so höret der HERR und errettet sie aus all ihrer Not.
Wenye haki hulia, naye Bwana huwasikia, huwaokoa katika taabu zao zote.
18 Der HERR ist nahe bei denen, die zerbrochenes Herzens sind, und hilft denen, die zerschlagen Gemüt haben.
Bwana yu karibu na waliovunjika moyo, na huwaokoa waliopondeka roho.
19 Der Gerechte muß viel leiden; aber der HERR hilft ihm aus dem allem.
Mwenye haki ana mateso mengi, lakini Bwana humwokoa nayo yote,
20 Er bewahret ihm alle seine Gebeine, daß deren nicht eins zerbrochen wird.
huhifadhi mifupa yake yote, hata mmoja hautavunjika.
21 Den Gottlosen wird das Unglück töten, und die den Gerechten hassen, werden Schuld haben.
Ubaya utamuua mtu mwovu, nao adui za mwenye haki watahukumiwa.
Bwana huwakomboa watumishi wake, yeyote anayemkimbilia yeye hatahukumiwa kamwe.

< Psalm 34 >