< Psalm 114 >
1 Da Israel aus Ägypten zog, das Haus Jakob aus dem fremden Volk,
Wakati Israeli walipotoka Misri, nyumba ya Yakobo kutoka kwa watu wa lugha ngeni,
2 da ward Juda sein Heiligtum, Israel seine HERRSChaft.
Yuda alifanywa makao matakatifu ya Mungu, Israeli akawa milki yake.
3 Das Meer sah und floh; der Jordan wandte sich zurück;
Bahari ilitazama ikakimbia, Yordani ulirudi nyuma,
4 die Berge hüpfeten wie die Lämmer, die Hügel wie die jungen Schafe.
milima ilirukaruka kama kondoo dume, vilima kama wana-kondoo.
5 Was war dir, du Meer, daß du flohest, und du Jordan, daß du dich zurückwandtest;
Ee bahari, ni nini kilichokufanya ukakimbia, nawe, ee Yordani, ukarudi nyuma,
6 ihr Berge, daß ihr hüpfetet wie die Lämmer, ihr Hügel, wie die jungen Schafe?
enyi milima mkarukaruka kama kondoo dume, enyi vilima, kama wana-kondoo?
7 Vor dem HERRN bebete die Erde, vor dem Gott Jakobs,
Ee dunia, tetemeka mbele za Bwana, mbele za Mungu wa Yakobo,
8 der den Fels wandelte in Wassersee und die Steine in Wasserbrunnen.
aliyegeuza mwamba kuwa dimbwi la maji, mwamba mgumu kuwa chemchemi za maji.