< Sprueche 2 >

1 Mein Kind, willst du meine Rede annehmen und meine Gebote bei dir behalten,
Mwanangu, kama utayakubali maneno yangu na kuyaweka akiba maagizo yangu ndani mwako,
2 so laß dein Ohr auf Weisheit achthaben und neige dein Herz mit Fleiß dazu.
kutega sikio lako kwenye hekima na kuweka moyo wako katika ufahamu,
3 Denn so du mit Fleiß danach rufest und darum betest,
na kama ukiita busara na kuita kwa sauti ufahamu,
4 so du sie suchest wie Silber und forschest sie wie die Schätze,
na kama utaitafuta kama fedha na kuitafuta sana kama hazina iliyofichwa,
5 alsdann wirst du die Furcht des HERRN vernehmen und Gottes Erkenntnis finden.
ndipo utakapoelewa kumcha Bwana na kupata maarifa ya Mungu.
6 Denn der HERR gibt Weisheit, und aus seinem Munde kommt Erkenntnis und Verstand.
Kwa maana Bwana hutoa hekima, na kinywani mwake hutoka maarifa na ufahamu.
7 Er läßt's den Aufrichtigen gelingen und beschirmet die Frommen
Anahifadhi ushindi kwa ajili ya mwadilifu, yeye ni ngao kwa wale wasio na lawama,
8 und behütet die, so recht tun, und bewahret den Weg seiner Heiligen.
kwa kuwa hulinda mwenendo wa mwenye haki na kuhifadhi njia ya waaminifu wake.
9 Dann wirst du verstehen Gerechtigkeit und Recht und Frömmigkeit und allen guten Weg.
Ndipo utafahamu lipi lililo kweli na haki na sawa: yaani kila njia nzuri.
10 Wo die Weisheit dir zu Herzen gehet, daß du gerne lernest,
Kwa maana hekima itaingia moyoni mwako, nayo maarifa yataifurahisha nafsi yako.
11 so wird dich guter Rat bewahren und Verstand wird dich behüten,
Busara itakuhifadhi na ufahamu utakulinda.
12 daß du nicht geratest auf den Weg der Bösen noch unter die verkehrten Schwätzer,
Hekima itakuokoa kutoka njia za waovu, kutoka kwa watu ambao maneno yao yamepotoka,
13 die da verlassen die rechte Bahn und gehen finstere Wege,
wale waachao mapito yaliyonyooka wakatembea katika njia za giza,
14 die sich freuen, Böses zu tun, und sind fröhlich in ihrem bösen, verkehrten Wesen,
wale wapendao kutenda mabaya na kufurahia upotovu wa ubaya,
15 welche ihren Weg verkehren und folgen ihrem Abwege;
ambao mapito yao yamepotoka na ambao ni wapotovu katika njia zao.
16 daß du nicht geratest an eines andern Weib, und die nicht dein ist, die glatte Worte gibt
Itakuokoa pia kutokana na mwanamke kahaba, kutokana na mke aliyepotoka mwenye maneno ya kushawishi kutenda ubaya,
17 und verläßt den HERRN ihrer Jugend und vergisset den Bund ihres Gottes;
aliyemwacha mwenzi wa ujana wake na kupuuza agano alilofanya mbele ya Mungu.
18 denn ihr Haus neiget sich zum Tode und ihre Gänge zu den Verlornen;
Kwa maana nyumba yake huelekea kwenye kifo na mapito yake kwenye roho za waliokufa.
19 alle, die zu ihr eingehen, kommen nicht wieder und ergreifen den Weg des Lebens nicht:
Hakuna yeyote aendaye kwake akarudi, au kufikia mapito ya uzima.
20 auf daß du wandelst auf gutem Wege und bleibest auf der rechten Bahn.
Hivyo utatembea katika njia za watu wema na kushikamana na mapito ya wenye haki.
21 Denn die Gerechten werden im Lande wohnen, und die Frommen werden drinnen bleiben;
Kwa maana wanyofu wataishi katika nchi, nao wasio na lawama watabakia ndani yake.
22 aber die Gottlosen werden aus dem Lande gerottet, und die Verächter werden draus vertilget.
Bali waovu watakatiliwa mbali kutoka nchi, nao wasio waaminifu watangʼolewa kutoka humo.

< Sprueche 2 >